Eeka Mangi
JF-Expert Member
- Jul 27, 2008
- 3,173
- 481
Pamoja na na utetezi wake wa jinsi Mramba na Yona walivyoletwa mahakamani jumatatu bila removal order, Mkuu wa magereza nchini Ndugu Nanyaro (kama sijakosea jina leke) alikiri kuwa ni kweli wafungwa katika gereza moja hapa nchini waliongea kwa njia ya simu na chombo kimoja cha habari na kutoa taarifa mbalimbali zinazowahusu. Katika mahojiano hayo na radio ya Taifa jana usiku, nanyaro anakiri kuwa hajui ni nani aliyewapa simu watu hao. Je katika hali hii, si ni kweli kuwa usalama katika kitengo cha Magereza nchini ni kitu ambacho hakipo. Tutaamini vipi kuwa hawajui wakati hawa jamaa wako mikononi mwao. Tena hakuongea mfungwa mmoja, ni kama 3 au 4 hivi. Kwa nini Nanyaro na team yake wasiwajibishwe kwa uzembe huu?
Nawasilisha
Nawasilisha