tpaul
JF-Expert Member
- Feb 3, 2008
- 21,476
- 17,674
Katika hali isiyokuwa ya kawaida huko mkoani Mbeya, marafiki wawili waliofumaniana guest house walifikia makubaliano ya kubadilisha wake zao. Hii ilitokea baada ya marafiki hao walioshibana kufumaniana kila mmoja akiwa na mke wa mwenzake lakini badala ya kulaumiana au kudhuriana wakakubaliana wabadilishane wake.
Mabadilishano hayo yalifanyika kwa maandishi mbele ya Afisa Mtendaji na baada ya tukio hilo kila mmoja aliondoka zake akiwa na furaha baada ya kumpata mke wa ndoto yake.
Hii story nimeipata leo kupitia Redio Clouds wakati wanapitia magazeti asubuhi hii ila sikufanikiwa kupata jina la gazeti. Nikifanikiwa kupata jina la gazeti nitashusha taarifa nzima hapa jukwaani.
MAONI YANGU
Mimi nawaunga mkono marafiki hao kwa ubunifu huo kwani hata kama wasingebadilishana wake bado wangeendelea kuibiana na wangeweza kuja kuumizana siku moja. Haya mabadilishano yamesaidia sana kuepusha figisufigisu zozote ambazo zingeweza kuja kujitokeza siku za usoni.
Mabadilishano hayo yalifanyika kwa maandishi mbele ya Afisa Mtendaji na baada ya tukio hilo kila mmoja aliondoka zake akiwa na furaha baada ya kumpata mke wa ndoto yake.
Hii story nimeipata leo kupitia Redio Clouds wakati wanapitia magazeti asubuhi hii ila sikufanikiwa kupata jina la gazeti. Nikifanikiwa kupata jina la gazeti nitashusha taarifa nzima hapa jukwaani.
MAONI YANGU
Mimi nawaunga mkono marafiki hao kwa ubunifu huo kwani hata kama wasingebadilishana wake bado wangeendelea kuibiana na wangeweza kuja kuumizana siku moja. Haya mabadilishano yamesaidia sana kuepusha figisufigisu zozote ambazo zingeweza kuja kujitokeza siku za usoni.