Johnny Sack
JF-Expert Member
- Jan 21, 2017
- 8,814
- 18,808
Pamoja na matatizo mengi Tanzania ilyokuwa nayo kabla ya mwaka 2016 lakini ilikuwa katika njia nzuri na ilikuwa inapiga hatua, Then akaingia Magufuli ambaye wengi, ikiwemo mimi nilidhani atatatua matatizo mengi ya nchi yetu kwa kipindi kile
Lakini Magufuli alikuja na siasa mpya ambazo ziliongeza matatizo ambayo hayakuwepo, siasa za kugombana na majirani na kufungiana mipaka, kugombana na jamii ya kimataifa, siasa za kupika takwimu, siasa za kuua sekta binafsi na kufilisi wafanyabishara, siasa za kufungia vyombo vya habari na kuvitisha visiandike habari fulani, siasa za kuhonga na kulazimisha wapinzani wakuunge mkono, siasa za kuteka na kuua watu wanaokukosoa kubambikiza kesi n.k
Uongozi wa Samia hautakuwa perfect, utakuwa na mabaya yake lakini angalau ameonyesha nia ya kuachana na siasa hizi zilizoturudisha nyuma sana, Samia alionyesha nia hii tangia hotuba yake ya kwanza lakini akapelekwa chaka na elements za Magufuli zilizokuwa zimesalia Serikalini na kwenye chama
Wapinzani nao wana wajibu wa kufanya compromise zao, wana madai mengi ya msingi lakini hayawezi kutekelezwa yote kwa wakati mmoja
Kuna yale ya msingi kama watu waliofungwa au wenye kesi za kubambikizwa hawa wafutiwe tu mara moja
Pia waachane na watu wa siasa za kali za matusi, wanaojifanya wana uchungu sana na nchi, waliona jinsi akina Kigogo na Mange walivyowageuka, watu wa siasa hizi sio wa kuwaamini na wanawaharibia taswira ya upinzani, kama kuna wanachama wao wenye tabia hizi wawafundishe pia
Upinzani kazi yake ni kutafuta mapungufu ya serikali na ku offer alternative, sio kazi yao kusifia, kwa hiyo serikali isitegemee wala isilazimishe kusifiwa na wapinzani
Lakini Magufuli alikuja na siasa mpya ambazo ziliongeza matatizo ambayo hayakuwepo, siasa za kugombana na majirani na kufungiana mipaka, kugombana na jamii ya kimataifa, siasa za kupika takwimu, siasa za kuua sekta binafsi na kufilisi wafanyabishara, siasa za kufungia vyombo vya habari na kuvitisha visiandike habari fulani, siasa za kuhonga na kulazimisha wapinzani wakuunge mkono, siasa za kuteka na kuua watu wanaokukosoa kubambikiza kesi n.k
Uongozi wa Samia hautakuwa perfect, utakuwa na mabaya yake lakini angalau ameonyesha nia ya kuachana na siasa hizi zilizoturudisha nyuma sana, Samia alionyesha nia hii tangia hotuba yake ya kwanza lakini akapelekwa chaka na elements za Magufuli zilizokuwa zimesalia Serikalini na kwenye chama
Wapinzani nao wana wajibu wa kufanya compromise zao, wana madai mengi ya msingi lakini hayawezi kutekelezwa yote kwa wakati mmoja
Kuna yale ya msingi kama watu waliofungwa au wenye kesi za kubambikizwa hawa wafutiwe tu mara moja
Pia waachane na watu wa siasa za kali za matusi, wanaojifanya wana uchungu sana na nchi, waliona jinsi akina Kigogo na Mange walivyowageuka, watu wa siasa hizi sio wa kuwaamini na wanawaharibia taswira ya upinzani, kama kuna wanachama wao wenye tabia hizi wawafundishe pia
Upinzani kazi yake ni kutafuta mapungufu ya serikali na ku offer alternative, sio kazi yao kusifia, kwa hiyo serikali isitegemee wala isilazimishe kusifiwa na wapinzani