Wafuasi wa Magufuli muelewe, siasa zenu hazina nafasi tena nchi hii, ila wapinzani nao wana wajibu

Johnny Sack

JF-Expert Member
Jan 21, 2017
8,814
18,808
Pamoja na matatizo mengi Tanzania ilyokuwa nayo kabla ya mwaka 2016 lakini ilikuwa katika njia nzuri na ilikuwa inapiga hatua, Then akaingia Magufuli ambaye wengi, ikiwemo mimi nilidhani atatatua matatizo mengi ya nchi yetu kwa kipindi kile

Lakini Magufuli alikuja na siasa mpya ambazo ziliongeza matatizo ambayo hayakuwepo, siasa za kugombana na majirani na kufungiana mipaka, kugombana na jamii ya kimataifa, siasa za kupika takwimu, siasa za kuua sekta binafsi na kufilisi wafanyabishara, siasa za kufungia vyombo vya habari na kuvitisha visiandike habari fulani, siasa za kuhonga na kulazimisha wapinzani wakuunge mkono, siasa za kuteka na kuua watu wanaokukosoa kubambikiza kesi n.k

Uongozi wa Samia hautakuwa perfect, utakuwa na mabaya yake lakini angalau ameonyesha nia ya kuachana na siasa hizi zilizoturudisha nyuma sana, Samia alionyesha nia hii tangia hotuba yake ya kwanza lakini akapelekwa chaka na elements za Magufuli zilizokuwa zimesalia Serikalini na kwenye chama

Wapinzani nao wana wajibu wa kufanya compromise zao, wana madai mengi ya msingi lakini hayawezi kutekelezwa yote kwa wakati mmoja

Kuna yale ya msingi kama watu waliofungwa au wenye kesi za kubambikizwa hawa wafutiwe tu mara moja

Pia waachane na watu wa siasa za kali za matusi, wanaojifanya wana uchungu sana na nchi, waliona jinsi akina Kigogo na Mange walivyowageuka, watu wa siasa hizi sio wa kuwaamini na wanawaharibia taswira ya upinzani, kama kuna wanachama wao wenye tabia hizi wawafundishe pia

Upinzani kazi yake ni kutafuta mapungufu ya serikali na ku offer alternative, sio kazi yao kusifia, kwa hiyo serikali isitegemee wala isilazimishe kusifiwa na wapinzani
 
Samia alikuja vizuri, Mbowe akawatuma akina mdude nyagali wamtukane eti wembe walioutumia kumnyoa magufuli watamnyolea SSH, moto waliopelekewa hawatausahau
 
CDM hawahitaji ku'compromise na utawala wa CCM kama zambarau, KARATA ya kucheza nayo ni kupigania KATIBA MPYA ambayo imekuwa mwiba mkali kwa watawala mafisadi.
Mbowe aliishiwa Hela za kulipa mawakili, akaitisha mchango mitandaoni akapata chini ya milioni tano, alijiaminisha Chadema Ina watu watamchangia, hawakuchanga, alivyoona wanachadema wamemtelekeza, akaamua kuomba radhi kwa SSH.

Akaona hana haja ya kujiumiza kukaa gerezani kwa ajili ya Wana Chadema wenye roho ya ubinafsi
 
CDM hawahitaji ku'compromise na utawala wa CCM kama zambarau, KARATA ya kucheza nayo ni kupigania KATIBA MPYA ambayo imekuwa mwiba mkali kwa watawala mafisadi.
Jana Mbowe kala ugali na samaki pale ikulu, samaki mkubwa, mama ni mama tu, akapewa na posho
 
Pamoja na matatizo mengi Tanzania ilyokuwa nayo kabla ya mwaka 2016 lakini ilikuwa katika njia nzuri na ilikuwa inapiga hatua, Then akaingia Magufuli ambaye wengi...
Mmehamia tena kwa Magufuli mshasahau Katiba na Tume huru?
Kila ajenda za CCM ni kudandia tu...
 
  • Thanks
Reactions: nao
Ungejua huyo unayemsifu anavyokudharau anakuona kama takataka haujui tu na siajabu hautakuja kujua!
 
Hapo kwenye kuhonga wapinzani, hapo mwenye tatizo ni aliehongwa ama aliehonga?

Matatizo ya wapinzani wetu kua wenye njaa na wasio na msimamo ni kosa la Magufuli?

Kugombana na majirani ni kitu cha kawaida pale unapoona maslahi ya nchi yanaingiliwa. Kazi ya rais ni kulinda maslahi ya nchi, rais akiona majirani wanaingilia maslahi yetu lazima akomae, hata Putin ndio maana ameivamia Ukraine kulinda maslahi ya nchi yake, Kikwete aligombana na Kagame kulinda masilahi ya nchi yetu.

Hoja kwamba Magufuli aligombana na majirani haina msingi wowote, hata Nyerere aligombana na Iddy Amin kulinda maslahi ya Tanzania. Ama ulitaka Magufuli awachekee wakenya wanavyoiba nchini kwetu?

Sekta binafsi ipi iliyokufa? Sekta binafsi ingekua imekufa banks zisingekua zinaogelea kwenye faida, ama husomi hata machapisho ya mapato ya mabenki nchini? Banks zisingekua zinafungua matawi kila kona. Hakuna sekta binafsi iliyokufa, huo ni uongo na uzushi.

Mapato ya Kodi yasingefik 2T kama sekta binafsi ingekua imekufa. Hoja ya sekta binafsi kufa haina mashiko.

Vyombo gani vya habari vilifungiwa? Hivi bijigazeti uchwara vinavyopika habari kina Tanzania Daima, Machweo sijui mawio? Hebu kua serious basi. Hakuna taifa linaweza kua na vyombo vya habari ambavyo kazi yake ni kutunga stori na kuzusha uongo na uzandiki kwenye jamii, hakuna Duniani.
 
Kuna wanaotukana wengi sana lakini kama kuna mtu kichwa chake hakina maneno yenye hekima ni MDUDE CHADEMA au Nyagali.

Naushauri uongozi wa CDM huyu MDUDE asipande kwenye majukwaa ya kisiasa.

Amewagharimu sana kwa yale matusi aliyotoa Tabata Barracuda mwaka Jana mwezi June immediately baada ya kuachiwa toka rumande ya Mbeya
 
Kuna wanaotukana wengi sana lakini kama kuna mtu kichwa chake hakina maneno yenye hekima ni MDUDE CHADEMA au Nyagali.

Naushauri uongozi wa CDM huyu MDUDE asipande kwenye majukwaa ya kisiasa.

Amewagharimu sana kwa yale matusi aliyotoa Tabata Barracuda mwaka Jana mwezi June immediately baada ya kuachiwa toka rumande ya Mbeya
Ccm mnajifanya kustaarabika baada ya mwendazake kufa, mlikuwa mnatukana mpaka bendera za cdm
 
Back
Top Bottom