Zanzibar-ASP
JF-Expert Member
- Nov 28, 2013
- 10,108
- 35,054
Ni miaka miwili sasa tangu Magufuli afariki dunia, huku baadhi ya wafuasi halisi wa Magufuli wakigoma kuamini katika mioyo yao au kutambua katika akili zao kuwa, kwa hakika Magufuli alishakufa na milele hataweza kurejea tena huku siasa zake mbovu taratibu zikizikwa na rais Samia Suluhu.
Hao watu wanaamini kuwa japokuwa Magufuli kimwili alishakufa lakini kiroho bado anaishi katikati yetu, hivyo anaweza kuendelea kuathiri maisha yetu au ipo siku utawala na siasa zake zitafufuliwa upya na kuendelea kuongoza Tanzania!
Wapo wanasiasa wajanja waliokuwa wafuasi kindaki ndaki wa Magufuli waliweza kutambua kiuhalisia Magufuli hayupo tena na siasa zake hazina nafasi na kwa haraka sana wakaanza kuimba nyimbo mpya za kumsifia Samia huku wakimdhihaki kimtindo Magufuli na siasa zake.
Wafuasi hao wa Magufuli hawafurahishwi na hatua yoyote ya maendeleo (kisiasa, kiuchumi, kijamii) inayopigwa na mama Samia ambayo Magufuli hakuifikia au hatua yoyote ya kufutwa kwa baadhi yq siasa za Magufuli zisizokuwa na maana kwa watanzania.
Wao wanataka kuona Magufuli akisifiwa katikati ya utawala wa Samia (wakati Magufuli alikuwa kinara wa kubeza serikali zote za Tanzania zilizomtangulia) au kuona utawala wa Samia ukianguka kwa namna yoyote.
Hao watu wanaamini kuwa japokuwa Magufuli kimwili alishakufa lakini kiroho bado anaishi katikati yetu, hivyo anaweza kuendelea kuathiri maisha yetu au ipo siku utawala na siasa zake zitafufuliwa upya na kuendelea kuongoza Tanzania!
Wapo wanasiasa wajanja waliokuwa wafuasi kindaki ndaki wa Magufuli waliweza kutambua kiuhalisia Magufuli hayupo tena na siasa zake hazina nafasi na kwa haraka sana wakaanza kuimba nyimbo mpya za kumsifia Samia huku wakimdhihaki kimtindo Magufuli na siasa zake.
Wafuasi hao wa Magufuli hawafurahishwi na hatua yoyote ya maendeleo (kisiasa, kiuchumi, kijamii) inayopigwa na mama Samia ambayo Magufuli hakuifikia au hatua yoyote ya kufutwa kwa baadhi yq siasa za Magufuli zisizokuwa na maana kwa watanzania.
Wao wanataka kuona Magufuli akisifiwa katikati ya utawala wa Samia (wakati Magufuli alikuwa kinara wa kubeza serikali zote za Tanzania zilizomtangulia) au kuona utawala wa Samia ukianguka kwa namna yoyote.