Wafuasi wa Hayati Magufuli bado hawajaamini kikamilifu kuwa alishafariki na siasa zake nyingi zinazikwa na Rais Samia

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Nov 28, 2013
10,108
35,054
Ni miaka miwili sasa tangu Magufuli afariki dunia, huku baadhi ya wafuasi halisi wa Magufuli wakigoma kuamini katika mioyo yao au kutambua katika akili zao kuwa, kwa hakika Magufuli alishakufa na milele hataweza kurejea tena huku siasa zake mbovu taratibu zikizikwa na rais Samia Suluhu.

Hao watu wanaamini kuwa japokuwa Magufuli kimwili alishakufa lakini kiroho bado anaishi katikati yetu, hivyo anaweza kuendelea kuathiri maisha yetu au ipo siku utawala na siasa zake zitafufuliwa upya na kuendelea kuongoza Tanzania!

Wapo wanasiasa wajanja waliokuwa wafuasi kindaki ndaki wa Magufuli waliweza kutambua kiuhalisia Magufuli hayupo tena na siasa zake hazina nafasi na kwa haraka sana wakaanza kuimba nyimbo mpya za kumsifia Samia huku wakimdhihaki kimtindo Magufuli na siasa zake.

Wafuasi hao wa Magufuli hawafurahishwi na hatua yoyote ya maendeleo (kisiasa, kiuchumi, kijamii) inayopigwa na mama Samia ambayo Magufuli hakuifikia au hatua yoyote ya kufutwa kwa baadhi yq siasa za Magufuli zisizokuwa na maana kwa watanzania.

Wao wanataka kuona Magufuli akisifiwa katikati ya utawala wa Samia (wakati Magufuli alikuwa kinara wa kubeza serikali zote za Tanzania zilizomtangulia) au kuona utawala wa Samia ukianguka kwa namna yoyote.
 
Watu wanaoumizwa na kifo cha Magufuli ni hawa MAJIZI ambao wameshindwa kumshahau. Nafikiri aliwaachia aina fulani ya UJAUZITO WA KISIASA.

Wazalendo wa nchi hii waliutambua mchango wa Magufuli, na sasa wamemuachia nafasi samia ili na yeye afanye yake.

LAKINI MAJIZI HAYALALI YANAMUWAZA MAGUFULI WAKIDHANI ATAFUFUKA WAENDELEE KULA KICHAPO!

Nafikiri ni aina fulani ya MENTAL DISORDER inayosababisha MARUWERUWE, kiasi kwamba muda wote mtu anahisi kufuatwa na MIZIMU au KUNYUKWA.
 
Yer 17:5

BWANA asema hivi, Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, Amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake Na moyoni mwake amemwacha BWANA.

Makonda.
Sabaya.
Happy.
Nk......

MAGUFULI AMEKUFA, MAGUFULI AMEKUFA, NASISTIZA AMEKUFA.....

NA SISI PIA TUTAKUFA.
TUJITAHIDI KUWA NA MATENDO MEMA TUSIWE MAKATILI KAMA MAGUFULI.
 
Wewe ni miongoni mwa wale wasiokuwa na hekima au kichwanj wewe ni kichaa. Kauli zenu hizi zinamletea mazingira magumu sana kisiasa Rais Dr Samia. Kwa ufupi Rais Samia kura za kanda ya ziwa mpaka sasa hana kabisa na asikudanganye mtu.

Na kilichosababisha ni kauli za kijinga namna hii. Hakuna anayesema eti siasa za Dkt Magufuli zilikuwa nzuri sijui. Watu wanachoangalia ni umakini wake ktk kuendesha serikali, vitu vilifanyika kwa uwazi. Ni ngumu sana mtu aliyekuwa ana nunua mchele kilo.

Kwa shs 1200 leo hii 2500 umuambie eti Dkt Magufuli alikuwa mtu mbaya, labda uwe kichaa utajaribu kuongea hivyo. Ndiyo maana hata mbowe na genge lake wanatumia nguvu sana ila watu wanawaona nao wamenunuliwa na akili zao hazipo sawa. Kwa ufupi moto uliopo chini juu ya upinzani wa Dkt Samia ni mkubwa sana tena hali yake kisiasa ni mbaya sana kwa sababu ya kuwaendekeza mijitu kama wewe yenye kudhani kumdhihaki Dkt Magufuli unaongeza umaarufu wa Dkt Samia.
 
... yule mtu alikuwa na chuki kupitiliza; sijui alikuwa na matatizo gani. Anaweza kuvunja rekodi kama mtanzania mwenye chuki zaidi kuwahi kutokea.
Huwa ninajiuliza, na sipati jibu kuwa, angekuwepo mpaka leo hii, sijui tungekuwa kwenye hali gani! Na kwa unafiki, sijui uoga, nina uhakika kuwa, mkoa mmoja baada ya mwingine ingekuwa ni maandamano yamepamba moto ya kutaka AONGEZEWE MUDA, baada ya muda wake kuisha!
 
Afu nao watamsahau tu..... time will tell
Ukitaka asaulike vyunja daraja la kijazi, stand zote iringa,sumbawanga, Singida, Dodoma, Mwanza, Njombe, masoko mikoa yote, hospital zote za wilayaa, machinjio ya ng'ombe, barabara zote, umeme mpaka vijijini, kidume kilivyosimamia Bwawa la Nyerere wakati wakina zito ,mbowe waliufyata Kwa wazungu kidume kikalianzisha, SGR, Daraja la Tanzanite, Daraja la Musisi , elimu bure nk app tutamsaau
 
Back
Top Bottom