Wafuasi wa CHADEMA na kauli tata kuhusu Ben Saanane

Frey Cosseny

JF-Expert Member
Feb 4, 2015
1,984
1,405
UNAJIFUNZA NINI KUTOKANA NA HAYA MATUKIO?

Magoiga SN-Mwanza

Yerriko Nyerere - Ben ni kijana mwenye IQ kubwa hata ku'challenge' PhD ya Rais. Nitampata Ben ndani ya siku 7. Mara tukasikia Kuanzia leo akaunti yangu ya facebook haitapost mambo ya siasa mpaka 2020.

Malisa GJ na UTG - Tumetoa taarifa polisi kuhusu kupotea kwa Ben, lakini polisi hawajamtafuta Ben ndiyo maana hajapatikana, Ukimya wa Chadema unatuhuzunisha, tunawataka watoe tamko.

Lissu/Chadema - Ben alitumiwa meseji ya vitisho, tunajua mahali ambapo vijana wanaoipinga serikali hii wanapotesewa. Tunaitaka serikali imtafute Ben Saanane.

Polisi - Ben alipotea tar 18 Nov, ila taarifa za kupotea kwake ziliwasilishwa na marafiki zake tar 5 Dec. Tunaendelea na uchunguzi.

Mbowe - Ben ametekwa, na sijazungumzia hilo maana kwa kufanya hivyo inaweza kuwafanya watekaji wamuue.

Bavicha - Baadabya Mbowe kujitokeza, Tunaipa serikali siku 7 ben awe amepatikana

Malisa GJ na UTG - Kuhusu kauli ya Mbowe Kimyaaa kama wamemwagiwa maji.

Kubenea/Mwanahalisi - Ben anaonekana ktk vijiwe vya kahama na marafiki zake, na amejificha kutafuta umaarufu wa kisiasa ili mwakani agombee uongozi wa ndani ya chama. Pata ukweli wa hili ktk tokeo la Jumatatu. Gacmzeti la mwanahalisi linamilikiwa na Mkurugenzi wa fedha wa Chadema(Komu) na Kubenea

Malisa GJ na UTG- Kubenea ni muongo, na polisi imkamate, Kubenea ana ugomvi na Ben Saanane. Anasema bila kufikiri, Ben ajifiche ili iweje?? Tuna Ushahidi kwamba wana ugomvi na Ben kwa muda mrefu ila mengine hatuwezi kuyaweka hadharani (Msema kweli anashindwa nini kuweka mambo hadharani)

Wafuasi wa Msafara wa Kibwetere Mitandaoni - - msituambie kitu, sisi tunajua CCM ndiyo imemfanyia hivyo Ben, Chadema ni chama cha Malaika wa Mungu

#My_Take

Ukitafakari kwa kina utagundua kuwa ule utafiti uliosema kuwa kati ya watanzania 4, mmoja ni kichaa- itakuwa hawa ndiyo waliohojiwa.

Magoiga SN-Mwanza
 
Iliporipotiwa Ben kapotea niliandika uzi ya kuwa "Ben kajiteka kutimiza operesheni katafunua"..nilionekana sina huruma ona sasa hii aibu Mbowe na vifaranga hawawezi kukwepa.

#mbowemletebenakiwahai#
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom