Wafuasi wa CHADEMA mnapigania demokrasia gani?

Developer IOS

JF-Expert Member
Jun 20, 2017
1,457
1,409
Habari wakuu,

Wafuasi wa CHADEMA na viongozi wao wameibuka na kumshambulia Rais na Serikali yake kwa kudai Serikali inaminya demokrasia kisa wamekatazwa kufanya mikutano na maandamano yenye lengo la uvunjifu wa amani nje ya majimbo yao.

Lakini lengo langu sio kuzungumizia hilo bali ni kuzungumzia unafiki au kutojielewa kwa wafuasi na viongozi wa CHADEMA wanaodai wanapigania demokrasia.

Je, demokrasia wanayoitaka ni ipi?

Kwasababu me navyoelewa demokrasia inahusisha kuthamini mawazo ya mtu hata kama mmepishana mawazo na kubishana kwa hoja sio kejeli wala matusi.

Tumeshuhudia tukianzia kwenye bodi watu CHADEMA wakijipa legitimate kuwa wao ndo wapo sahihi na yeyote atakayepingana mawazo yake atashambuliwa kwa matusi kejeli na kuonekana anajipendekeza.

Yeyote atakayeripoti mambo mazuri ya Serikali ambayo ni mengi na yanaonekana atashambuliwa.Upinzani sio tu kukosoa Serikali upinzani dhabiti unapaswa kupongeza pale Serikali inapopatia.

Tukirudi kitaifa tujikumbushe pale Lazaro Nyalandu,Lowassa na wengine wengi walipohama chama tawala na kujiunga nao walishangilia na kuona ile ni demokrasia lakini wakina Mtolea,Waitara na wengine walipoenda chama tawala wakasema wamenunuliwa na waliwashambulia kwa matusi na kejeli.

Wakina Kakobe walipokosoa Serikali walikuwa mashujaa lakini walipoenda kumueleza matatizo yao Rais Magufuli mkawatukana.

Je, mlitaka shida na kero zao nani kama sio Rais.

Je, mlitaka wapingane na maandiko yanaowataka waheshimu mamlaka?
 
Matukio uliyoyataja hayaakisi unachokiita demokrasia. Jifunze kwanza maana ya demokrasia.

Pili, jitahidi kufuatilia jambo/mambo kwa kina kisha uweke mawazo ya utafiti au uchunguzi wako kwa kadri ya ulichokiona au kugundua wewe binafsi kuhusu hilo jambo, unaweza usifurahishe watu au usipendwe lakini itakujengea heshima.

Nikutolee mfano, ikitokea ukawekewa ushahidi kwamba hao unaowatolea mfano hawakuhama kwa maamuzi yao bali kuna aina ya biashara ilifanyika, bado utaendelea kuutetea huu uzi kwa kiwango kilekile?
 
Matukio uliyoyataja hayaakisi unachokiita demokrasia. Jifunze kwanza maana ya demokrasia.

Pili, jitahidi kufuatilia jambo/mambo kwa kina kisha uweke mawazo ya utafiti au uchunguzi wako kwa kadri ya ulichokiona au kugundua wewe binafsi kuhusu hilo jambo, unaweza usifurahishe watu au usipendwe lakini itakujengea heshima.

Nikutolee mfano, ikitokea ukawekewa ushahidi kwamba hao unaowatolea mfano hawakuhama kwa maamuzi yao bali kuna aina ya biashara ilifanyika, bado utaendelea kuutetea huu uzi kwa kiwango kilekile?

Usijaribu kupita kwenye reli aliyowahusisha mleta mada.ya kujiona sahihi wakati wote,huo nao ni udictator bila kujitambua.

Demokrasia ni nini,kama si kuheshimu mawazo ya mwingine???au kuna maana nyingine unaifahamu??

Unasema ukiletwa ushahidi!!!ushahidi upi ambao ymeshindikana kuletwa siku zote hizo watu wamebaki kubwabwaja kwa hisia zao tu!!!!

Anaehama aheshimiwe bila kuhusisha kitu chochote!!mnataka kuwashika watu akili kwamba upinzani ndio final destination!!!hakuna kwingine!!!kichaa cha wapi hiki??
 
Weka Hapa hicho kifungu cha sheria kinachosema rais anaweza kuzuia wenzie kufanya mikutano nje ya majimbo yao!

Uruhusiwe kufanya mikutano,badala ya kwenda kujadili mambo ya msingi ya maendeleo,agenda inakwenda kuwa udikteta uchwara wa rais wa awamu ya tano!!!

Unatambua kiwango cha ukichaa alichonacho mtu kwa matendo yake,utajua huyu ale na watoto au peke yake.
 
Na kwa suala la kupiga marufuku shughuli za siasa wala Rais asilaumiwe. Wanatakiwa kujilaumu wapinzani wenyewe kwa kuandaa UKUTA huku mwenyekiti akitamka hadharani kuwa yatakuwa maandamano yasiyo na kikomo nchi nzima kuhakikisha nchi haitawaliki.

Sijui alidhani mtawala ni mkwere waliyezoea kumchokoza kila uchao??
 
Usijaribu kupita kwenye reli aliyowahusisha mleta mada.ya kujiona sahihi wakati wote,huo nao ni udictator bila kujitambua.

Demokrasia ni nini,kama si kuheshimu mawazo ya mwingine???au kuna maana nyingine unaifahamu??

Unasema ukiletwa ushahidi!!!ushahidi upi ambao ymeshindikana kuletwa siku zote hizo watu wamebaki kubwabwaja kwa hisia zao tu!!!!

Anaehama aheshimiwe bila kuhusisha kitu chochote!!mnataka kuwashika watu akili kwamba upinzani ndio final destination!!!hakuna kwingine!!!kichaa cha wapi hiki??
Kupingwa nayo ni demokrasia!Nikiona mawazo yako ni ya kipuuzi nayo nimetumia demokrasia!Cha msingi tusitwangane tisasi au mapanga!
 
Na kwa suala la kupiga marufuku shughuli za siasa wala Rais asilaumiwe. Wanatakiwa kujilaumu wapinzani wenyewe kwa kuandaa UKUTA huku mwenyekiti akitamka hadharani kuwa yatakuwa maandamano yasiyo na kikomo nchi nzima kuhakikisha nchi haitawaliki. Sijui alidhani mtawala ni mkwere waliyezoea kumchokoza kila uchao??
Kabla ya huo unaoitwa UKUTA,tayari marufuku ilikuwa imeshapigwa,kwa siasa mpaka 2020!
JIWE ni JIWE tu,hata hajui siasa ni nini!
 
Ulisems wewe ni mwanasingida mashariki kwaio wakati mnamchagua Lissu ulikua unadhani anapigania demokrasia gani
 
Kupingwa nayo ni demokrasia!Nikiona mawazo yako ni ya kipuuzi nayo nimetumia demokrasia!Cha msingi tusitwangane tisasi au mapanga!

Kumpinga mtu ni demokrasia-kugundua kwamba mawazo yangu ni ya kipuuzi kisha ukanishauri kwa kuzingatia cheo na mamlaka niliyinayo,ni demokrasia iliyopevuka.

Ni kwamba uamue moja kati ya pande hizi mbili,kuwa mpinzaji(manasiasa)/au mwanaharakati(usiyemwanasiasa).

Ukichanganya hayo utakutana na vingi si risasi pekee.
 
Hivi kwa kuandika hivi ndio utalipwa bei gani ?
hii ndo demokrasia tunayoizungumzia unashindwa kuheshimu mawazo yangu eti wewe ukiandika kisa mpinzani ni mpigania haki mimi nikiandika kisa napongeza serikali kwa mambo mazuri inayofanya basi nalipwa au natumika huu upuuzi sijui mtaacha lini
 
Kumpinga mtu ni demokrasia-kugundua kwamba mawazo yangu ni ya kipuuzi kisha ukanishauri kwa kuzingatia cheo na mamlaka niliyinayo,ni demokrasia iliyopevuka.

Ni kwamba uamue moja kati ya pande hizi mbili,kuwa mpinzaji(manasiasa)/au mwanaharakati(usiyemwanasiasa).

Ukichanganya hayo utakutana na vingi si risasi pekee.
Ndio huo ufala tunaoupinga,risasi sio suluhisho!Nikiamua kuwa mwanaharakati mwanasiasa ni mimi na uamizi wangu,kama navunja sheria nipelekwe mahakamani ili sheria ichukue mkondo wake!
Wangese na vichaa ndio huona risasi kama hukumu na watoa hukumu ni wao!
 
Ndio huo ufala tunaoupinga,risasi sio suluhisho!Nikiamua kuwa mwanaharakati mwanasiasa ni mimi na uamizi wangu,kama navunja sheria nipelekwe mahakamani ili sheria ichukue mkondo wake!
Wangese na vichaa ndio huona risasi kama hukumu na watoa hukumu ni wao!

Kama unadhani ni rahisi kupeleka kila mhuni mahakamani,mpeleke na unayehisi alimpiga risasi mh lissu.

Mnapenda sana ndoto katika uhalisia.
 
Kama unadhani ni rahisi kupeleka kila mhuni mahakamani,mpeleke na unayehisi alimpiga risasi mh lissu.

Mnapenda sana ndoto katika uhalisia.
Kwa mujibu wa katiba,mahakama ndio chombo cha kutoa haki!Huu mwingine ni uhuni na ufuska unaofanyika!
 
Uruhusiwe kufanya mikutano,badala ya kwenda kujadili mambo ya msingi ya maendeleo,agenda inakwenda kuwa udikteta uchwara wa rais wa awamu ya tano!!!

Unatambua kiwango cha ukichaa alichonacho mtu kwa matendo yake,utajua huyu ale na watoto au peke yake.

Hivi haiwezekani kufanya mkutano kujadili MAMBO YA MSINGI YA MAENDELEO?
 
Habari wakuu,

Wafuasi wa CHADEMA na viongozi wao wameibuka na kumshambulia Rais na Serikali yake kwa kudai Serikali inaminya demokrasia kisa wamekatazwa kufanya mikutano na maandamano yenye lengo la uvunjifu wa amani nje ya majimbo yao.

Lakini lengo langu sio kuzungumizia hilo bali ni kuzungumzia unafiki au kutojielewa kwa wafuasi na viongozi wa CHADEMA wanaodai wanapigania demokrasia.

Je, demokrasia wanayoitaka ni ipi?

Kwasababu me navyoelewa demokrasia inahusisha kuthamini mawazo ya mtu hata kama mmepishana mawazo na kubishana kwa hoja sio kejeli wala matusi.

Tumeshuhudia tukianzia kwenye bodi watu CHADEMA wakijipa legitimate kuwa wao ndo wapo sahihi na yeyote atakayepingana mawazo yake atashambuliwa kwa matusi kejeli na kuonekana anajipendekeza.

Yeyote atakayeripoti mambo mazuri ya Serikali ambayo ni mengi na yanaonekana atashambuliwa.Upinzani sio tu kukosoa Serikali upinzani dhabiti unapaswa kupongeza pale Serikali inapopatia.

Tukirudi kitaifa tujikumbushe pale Lazaro Nyalandu,Lowassa na wengine wengi walipohama chama tawala na kujiunga nao walishangilia na kuona ile ni demokrasia lakini wakina Mtolea,Waitara na wengine walipoenda chama tawala wakasema wamenunuliwa na waliwashambulia kwa matusi na kejeli.

Wakina Kakobe walipokosoa Serikali walikuwa mashujaa lakini walipoenda kumueleza matatizo yao Rais Magufuli mkawatukana.

Je, mlitaka shida na kero zao nani kama sio Rais.

Je, mlitaka wapingane na maandiko yanaowataka waheshimu mamlaka?
Mnajitukana wenyewe kwa kukiri na kuonyesha kwa vitendo na maneno, na uzi kama huu wako, kwamba hamjui maana ya democracy.
 
Back
Top Bottom