Makanyaga
JF-Expert Member
- Sep 28, 2007
- 10,323
- 6,848
Moshi. Watu sita wanaoaminika ni wafuasi wa vyama vya upinzani vya Chadema na ACT- Wazalendo, wamefikishwa mahakamani katika kesi mbili tofauti jana Jumatatu Novemba 11,2019 ikiwamo ya kuchoma ofisi ya mtendaji wa kata ya Soweto katika Manispaa ya Moshi.
Katibu wa Chadema mkoa Kilimanjaro, Basil Lema alithibitisha watuhumiwa watano kati ya sita ni wafuasi wao na mmoja ambaye hakumtaja kwa jina ni mwanachama wa chama cha ACT- Wazalendo.
Hata hivyo, hati ya mashitaka iliyosomwa mahakamani na mawakili wa Serikali kutoka Divisheni ya Taifa ya Mashitaka (NPS), Kassim Nassir na Ignas Mwinuka haikuwataja watuhumiwa kama wafuasi wa vyama hivyo vya siasa.
Waliofikishwa mbele ya Hakimu mkazi Moshi, Jullieth Mawolle kwa kuchoma ofisi ya Afisa mtendaji wa Kata ya Soweto ni pamoja na Diwani wa Kata hiyo kwa tiketi ya Chadema, Collins Mayuta (40), ambaye pamoja na wenzake wanne walikana mashitaka dhidi yao.
Watuhumiwa wengine ni Mohamed Bakari(27), Paulo Lyimo(37), Priscus Kayanda (44) na Juma Ally (27), ambao hawakuweza kutimiza masharti ya dhamana ya kuwa na wadhamini watakaosaini bondi ya Sh2 milioni isipikuwa Mayuta pekee aliweza kudhaminiwa.
Chanzo: Mwananchi
Katibu wa Chadema mkoa Kilimanjaro, Basil Lema alithibitisha watuhumiwa watano kati ya sita ni wafuasi wao na mmoja ambaye hakumtaja kwa jina ni mwanachama wa chama cha ACT- Wazalendo.
Hata hivyo, hati ya mashitaka iliyosomwa mahakamani na mawakili wa Serikali kutoka Divisheni ya Taifa ya Mashitaka (NPS), Kassim Nassir na Ignas Mwinuka haikuwataja watuhumiwa kama wafuasi wa vyama hivyo vya siasa.
Waliofikishwa mbele ya Hakimu mkazi Moshi, Jullieth Mawolle kwa kuchoma ofisi ya Afisa mtendaji wa Kata ya Soweto ni pamoja na Diwani wa Kata hiyo kwa tiketi ya Chadema, Collins Mayuta (40), ambaye pamoja na wenzake wanne walikana mashitaka dhidi yao.
Watuhumiwa wengine ni Mohamed Bakari(27), Paulo Lyimo(37), Priscus Kayanda (44) na Juma Ally (27), ambao hawakuweza kutimiza masharti ya dhamana ya kuwa na wadhamini watakaosaini bondi ya Sh2 milioni isipikuwa Mayuta pekee aliweza kudhaminiwa.
Chanzo: Mwananchi