Mtoboasiri
JF-Expert Member
- Aug 6, 2009
- 5,101
- 1,946
Wafuasi wa CCM wampiga m/kiti wao Send to a friend Mwananchi: Monday, 15 November 2010
Joyce Joliga, Songea
MWENYEKITI wa CCM wa Kata ya Bombambili, katika Manispaa ya Songea, Alphonce Haule (51) amejeruhiwa vibaya kwa kupigwa na mawe, fimbo na makopo.
Habari zilisema kitendo hicho kimefanywa na wafuasi na wanachama wa chama hicho, ambao pia walimkimbiza Katibu wa tawi hilo, Athuman Ngangilo.
Tukio hilo lilitokea saa 4:00 asubuhi ya jana na habari zilisema wanachama na wafuasi hao, wamekerwa na matokeo ya uchaguzi, katika eneo hilo.
Kwa mujibu wa habari zilizopatikana katika eneo hilo, wanachama na wafuasi wa chama hicho, wanawatuhumu viongozi hao kuwa wamekisaliti chama chao na kushiriki katika kuipigia kampeni Chadema.
Wakizungumza na waandishi wa habari katika eneo la tukio, wanachama hao waliokuwa na jazba, walisema kuwa kitendo kimesababisha kata hiyo kuchukuliwa na upinzani.
Walisema viongozi hao ni wasaliti wakubwa na ambao walikuwa na lengo la kukuhujumu chama, ili kukose ushindi kama ilivyojitokeza.Mmoja wa wanachama hao, Apronia Miti, ambaye ni mkazi wa Bombambili, aliwaambia waandishi wa habari kuwa haiji akilini kwa kata hiyo kuchukuliwa na Chadema kwa urahisi mno.
Alisema kitendo kilichofanywa na viongozi hao, kimewaudhi na kuwakera wanachama na wafuasi wa CCM na ndiyo maana wameamua kuwashambulia kwa mawe.
Kwa Mary Komba, alisema kimsingi wanachama wa CCM katika kata hiyo, wamechoshwa na uongozi wa kuanzia ngazi ya wilayani hadi katika kata yo hata baada ya kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi.
Alisema mara kadhaa wamewasilisha wilayani, malalamiko kuhusu watu wanaokihujumu chama, lakini viongozi wa wilaya, walishindwa kuchukuwa hatua.
Kwa upande wake, Haule alikiri kutokea kwa vurugu zilizoambatna na kumshambulia na kwamba tayari ametoa taarifa polisi.Alisema amejeruhiwa kichwani na kwamba alikwenda katika hospitali ya mkoa kwa matibabu.
hatua za kisheria.atibu Msaidizi wa CCM wa Wilaya ya Songea Mjini, Zongolobe Zongo, alikiri kupokea taarifa za vurugu hizo .
Joyce Joliga, Songea
MWENYEKITI wa CCM wa Kata ya Bombambili, katika Manispaa ya Songea, Alphonce Haule (51) amejeruhiwa vibaya kwa kupigwa na mawe, fimbo na makopo.
Habari zilisema kitendo hicho kimefanywa na wafuasi na wanachama wa chama hicho, ambao pia walimkimbiza Katibu wa tawi hilo, Athuman Ngangilo.
Tukio hilo lilitokea saa 4:00 asubuhi ya jana na habari zilisema wanachama na wafuasi hao, wamekerwa na matokeo ya uchaguzi, katika eneo hilo.
Kwa mujibu wa habari zilizopatikana katika eneo hilo, wanachama na wafuasi wa chama hicho, wanawatuhumu viongozi hao kuwa wamekisaliti chama chao na kushiriki katika kuipigia kampeni Chadema.
Wakizungumza na waandishi wa habari katika eneo la tukio, wanachama hao waliokuwa na jazba, walisema kuwa kitendo kimesababisha kata hiyo kuchukuliwa na upinzani.
Walisema viongozi hao ni wasaliti wakubwa na ambao walikuwa na lengo la kukuhujumu chama, ili kukose ushindi kama ilivyojitokeza.Mmoja wa wanachama hao, Apronia Miti, ambaye ni mkazi wa Bombambili, aliwaambia waandishi wa habari kuwa haiji akilini kwa kata hiyo kuchukuliwa na Chadema kwa urahisi mno.
Alisema kitendo kilichofanywa na viongozi hao, kimewaudhi na kuwakera wanachama na wafuasi wa CCM na ndiyo maana wameamua kuwashambulia kwa mawe.
Kwa Mary Komba, alisema kimsingi wanachama wa CCM katika kata hiyo, wamechoshwa na uongozi wa kuanzia ngazi ya wilayani hadi katika kata yo hata baada ya kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi.
Alisema mara kadhaa wamewasilisha wilayani, malalamiko kuhusu watu wanaokihujumu chama, lakini viongozi wa wilaya, walishindwa kuchukuwa hatua.
Kwa upande wake, Haule alikiri kutokea kwa vurugu zilizoambatna na kumshambulia na kwamba tayari ametoa taarifa polisi.Alisema amejeruhiwa kichwani na kwamba alikwenda katika hospitali ya mkoa kwa matibabu.
hatua za kisheria.atibu Msaidizi wa CCM wa Wilaya ya Songea Mjini, Zongolobe Zongo, alikiri kupokea taarifa za vurugu hizo .