Wafuasi wa CCM tambueni hili, Uongozi Bora si suala la chama, ni utashi wa kiongozi husika, Raisi awamu ya tano alizingua kuliko Marais wote wa JMT

PASCAL mayalla....unachodhani wewe si lazima kiwe ambacho huyu MTU wako angefanya......na unapopatia Jambo moja kwa prediction haimaanishi kuwa kila uki- predict itakuwa. Mimi ninasimamia kuwa asingetupatia katiba mpya kwa kuwa alitamka rasmi"SIKUNADI KATIBA MPYA KWENYE KAMPENI".
Hakuna ushahidi wowote wala vikao vyovyote vya siri, bali mimi ni a good trends reader, nimekuwa nikimfuatilia Magufuli very closely, hivyo nikasoma trends zake nikajua, angetuachia katiba mpya.
Angalia tarehe ya bandiko hilo na uone hoja zake
P
 
Wasalaaaam!

Ni ukweli usiopingika kuwa, pamoja kwamba Rais Samia alikua Makamu wa Rais awamu ya tano, lakin hawakuwa kitu kimoja na Raisi wa awamu hiyo inangawa Rais Samia amejaribu kutuaminisha mara kadhaa akisema wao ni kitu kimoja!
Lakini kauli hiyo haiendani na matendo yake!

Kumekuwa na porojo nyingi eti Rais Bora ni yule anayetokana na CCM, ila kwa maoni yangu utashi wa Raisi husika ndio unatoa mwangaza wa ubora wa serikali anayoiongoza!

Mathalani, awamu ya tano ilikua ya kibabebabe, isiyosikiliza vilio vya wananchi kwa ujumla , ilitoa mamlaka kwa yeyote mwenye cheo kufanya akitakacho kwa wakat wowote mfano hai akiwa ni Makonda na Sabaya!

Lakini awamu ya sita imeonekana kuwa sikivu, inazingatia misingi ya utawala wa sheria, maovu yaliyofanyika awamu ya tano yanakatiliwa mbali huku Neema ikitangazwa haswa kwa wale waliodhulumiwa!

Nadhan Wana CCM Kuna Jambo la kujifunza hapa, mnapochagua mtu wa kumpa kiti Cha Uraisi, zingatieni utashi wa mtu mwenyewe, sio kuleta mtu anayesimamia misimamo yake hata Kama haina tija, sio kuteuwa mtu ambaye atakomoa upande wa pili wa Vyama pinzani nakati wote ni wanadamu safar yetu ni moja!

Mwisho kabisa!
Ashukuriwe Mungu anayejua mawazo ya watu, maana kwa akili ya kawaida sidhan Kama kungefanyika uchaguzi mngempendekeza Mama Samia kigombea kiti Cha urais, ila ni Mungu tu aliemjua toka mwanzo kuwa anaweza, na ameonesha dira kuwa Tanzania itakuwa na utawala unaozingatia misingi ya haki za Binadamu na sheria tofauti kabisa na mtangulizi wake!
Big brain discuss ideas, fool mind discuss people😂😂😂😂😂😂😂
 
Amechemka kidogo kwaajili ya furaha , huenda ni mwana chadema.

Mleta mada amezingatia uhalisia uliopo sasa ambapo mifumo haifanyi kazi bali masuala yote ya kitaifa hutegemea uamuzi wa Rais ambaye ndiye Mwenyekiti wa CCM.

Hoja ya umuhimu wa mifumo makini badala ya kutegemea mtu iko pale pale. Hii ndio hoja ya kudai katiba mpya. LAKINI, kabla ya hapo, inabidi CCM washauriwe kuteua watu makini hasa katika ngazi ya uRais. Wakipuuza, ni maumivu kwa wote. Somo limeshasomeka.
 
Back
Top Bottom