Baada ya miaka mingi ya mfumo wa vyama vya wafanyakazi kuonekana kushindwa kabisa kutetea maslahi ya wafanyakazi wa kada mbali mbali hususan katika kipindi hikli cha mfumuko mkubwa wa bei; hivi karibuni wafanyakzi wa kada mbali mbali wamejitokea kudai haki zao ikiwemo kutumia migomo nje ya utaratibu wa vyama vya wafanyakazi.
Mifano hai ya hali hiyo ni madereva wa magari makubwa ambaokwa mingi wamekuwa wakinyanyswa kwa kufanya kazi pasipo mikataba, kulipwa ujira na posho ndogo za kujikimu wawapo nje ya vituo vyo vya kazi, kunyanyaswa na waajiri n.k.
Katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita madereva hawa wamewahi kugoma mara mbali chini ya asasi ya kiraia (NGO) Chama cha Madereva wa Magari makubwa Tanzania (CHAMAMATA) badala ya kutumia Chama cha wafanyakzi sekta ya usafirishaji (COTWU). Aidha hivi sasa madakatari wapo katika mgomo chini ya chama cha Madakatari (MAT) kilichounda kamati ya mpito kusimamia mgomo huo badala ya kutumia Chama cha wafanyakazi sekta ya afya (TUGHE).
Badala ya wadau ndani ya vyama vya wafanyakazi kukaa chini na kutafakari hali hii mpya ina maana gani kwa mustakabali wa vyama vya wafanyakazi hapa nchini, Shirikisho a Vyama vya wafanyakazi (TUCTA) lilikurupuka na kupitia Katibu Mkuu wake Ndg Nicholas Mgaya na kutangaza kuwa mgomo wa madaktari ni batili.
Je ni nini kimepelekea wafanyakazi nchini Tanzania kupoteza imani ya mfumo rasmi wa vyama vya wafanyakazi kiasi cha kutumia njia na majukwaa mbadala kudai haki zao?
Je kama ambavyo wafanyakazi wameonyesha kupoteza imani ya mfumo wa vyama vya wafanyakazi, wananchi nao wanaweza kupoteza imani na mhimili wa bunge ikizingatiwa kuwa kadrisiku zinzvyoongezeka mhimili huo unonyesha kuwa kushindwa majukumu yake ya kuwa wawakilishi wa wananchi katika kuisimamia serikali na badala yake wanaungana na wafujaji wa fedha na raslimali za umma walioko katika mhimili wa serikali kwa kujitwalia mikopo mikubwa mikubwa kwa kutumia dhamana zitokanazo na kodi za wananchi, kujilundikia kiasi kikubwa cha posho ya kukaa kutenda kazi ambzo wanalipwa mishahra kuzitenda n.k
Tukifika hapo nini hatma ya Tanzania?
Mifano hai ya hali hiyo ni madereva wa magari makubwa ambaokwa mingi wamekuwa wakinyanyswa kwa kufanya kazi pasipo mikataba, kulipwa ujira na posho ndogo za kujikimu wawapo nje ya vituo vyo vya kazi, kunyanyaswa na waajiri n.k.
Katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita madereva hawa wamewahi kugoma mara mbali chini ya asasi ya kiraia (NGO) Chama cha Madereva wa Magari makubwa Tanzania (CHAMAMATA) badala ya kutumia Chama cha wafanyakzi sekta ya usafirishaji (COTWU). Aidha hivi sasa madakatari wapo katika mgomo chini ya chama cha Madakatari (MAT) kilichounda kamati ya mpito kusimamia mgomo huo badala ya kutumia Chama cha wafanyakazi sekta ya afya (TUGHE).
Badala ya wadau ndani ya vyama vya wafanyakazi kukaa chini na kutafakari hali hii mpya ina maana gani kwa mustakabali wa vyama vya wafanyakazi hapa nchini, Shirikisho a Vyama vya wafanyakazi (TUCTA) lilikurupuka na kupitia Katibu Mkuu wake Ndg Nicholas Mgaya na kutangaza kuwa mgomo wa madaktari ni batili.
Je ni nini kimepelekea wafanyakazi nchini Tanzania kupoteza imani ya mfumo rasmi wa vyama vya wafanyakazi kiasi cha kutumia njia na majukwaa mbadala kudai haki zao?
Je kama ambavyo wafanyakazi wameonyesha kupoteza imani ya mfumo wa vyama vya wafanyakazi, wananchi nao wanaweza kupoteza imani na mhimili wa bunge ikizingatiwa kuwa kadrisiku zinzvyoongezeka mhimili huo unonyesha kuwa kushindwa majukumu yake ya kuwa wawakilishi wa wananchi katika kuisimamia serikali na badala yake wanaungana na wafujaji wa fedha na raslimali za umma walioko katika mhimili wa serikali kwa kujitwalia mikopo mikubwa mikubwa kwa kutumia dhamana zitokanazo na kodi za wananchi, kujilundikia kiasi kikubwa cha posho ya kukaa kutenda kazi ambzo wanalipwa mishahra kuzitenda n.k
Tukifika hapo nini hatma ya Tanzania?