mambomoto1
New Member
- Nov 24, 2021
- 4
- 15
Ni kwa masikitiko kuwa wafanyakazi wa Baa ya New Sideway iliyoko Bunju A Kinondoni DSM hasa wanaohudumia vinywaji wamekuwa na tabia mbaya sana ya ubaguzi katika kuwahudumia wateja.
Kama wewe hutoi offer au huna urafiki na wahudumu jua imekula kwako. Unaweza kufika unakaa unasubiri mhudumu akusikilize haji na unawaona wapo tu karibu wamekaa makundi makundi wakipiga soga ila cha kushangaza akija mshikaji wao wataamka fasta kumkimbilia na kwenda kumsikiliza. Inakubidi usubiri au uite kwa kulazimisha ndo atakuja kukusikiliza na akishakuhudumia anapotea jumla kwenda kukaa na washkaji wao.
Ukweli ni kuwa wahudumu wa hii baa ni wapuuzi wakubwa hawajielewi na wataua hii baa muda si mrefu, watu wengi hawaridhishwi na tabia hizi wanaenda tu kwa vile hakuna namna ila endapo patatokea Bar mbadala basi wajiandae kufa kifo cha mende.
Nimehama rasmi hii baa nakunywa zangu maeneo ya Boko, au Tegeta au Mbezi.
Najua watajitetea ni wivu au vita za kibiashara ila huo ndo ukweli. Meneja naye hajielewi kabisa kwanza anawaogopa wahudumu.
Ni hayo tu
Kama wewe hutoi offer au huna urafiki na wahudumu jua imekula kwako. Unaweza kufika unakaa unasubiri mhudumu akusikilize haji na unawaona wapo tu karibu wamekaa makundi makundi wakipiga soga ila cha kushangaza akija mshikaji wao wataamka fasta kumkimbilia na kwenda kumsikiliza. Inakubidi usubiri au uite kwa kulazimisha ndo atakuja kukusikiliza na akishakuhudumia anapotea jumla kwenda kukaa na washkaji wao.
Ukweli ni kuwa wahudumu wa hii baa ni wapuuzi wakubwa hawajielewi na wataua hii baa muda si mrefu, watu wengi hawaridhishwi na tabia hizi wanaenda tu kwa vile hakuna namna ila endapo patatokea Bar mbadala basi wajiandae kufa kifo cha mende.
Nimehama rasmi hii baa nakunywa zangu maeneo ya Boko, au Tegeta au Mbezi.
Najua watajitetea ni wivu au vita za kibiashara ila huo ndo ukweli. Meneja naye hajielewi kabisa kwanza anawaogopa wahudumu.
Ni hayo tu