Wafanyakazi sasa wambana Mbunge Chitalilo

Mag3

Platinum Member
May 31, 2008
13,064
22,756
Mwananchi
Date::7/1/2008

SAKATA la Mbunge wa Buchosa, Samwel Mchele Chitalilo, kuwaita wapiga kura wake waliotoa maoni yao na kumtaka anyamaze kuwa ni wahuni, limeingia hatua mpya baada ya Katibu wa Chama cha Wafanyakazi wa Taasisi za Elimu ya Juu, Sayansi, Teknolojia, Habari na Utafiti (RAAWU) Kanda ya Ziwa, kumtaka awaheshimu wapiga kura.

Akizungumza jana na gazeti hili, katibu wa Raawu Kanda ya Ziwa ambaye pia ni Katibu wa Shirikisho la Vyama vya wafanyakazi Tanzania (TUCTA) Mkoa wa Mwanza, Ramadhani Mwendwa, alisema wao kama wafanyakazi wamesikitishwa na kauli ya mbunge huyo kuwaita wapiga kura wake wahuni kwa kitendo cha kutoa maoni yao.

Alisema kauli aliyoitoa Chitalilo bungeni kutetea ufisadi inatia mashaka na wao wanaona jinsi baadhi ya wabunge wao wasivyo wazalendo kwa nchi yao.

Mwendwa alisema kauli kama za Chitalilo na wabunge wengine zinazotoka bungeni ni hatari kwa vile zitaifikisha nchi hii pabaya siku wananchi watakapoamua kutafuta haki yao kwa vita ama njia nyingine baada ya kuchoshwa na ufisadi ambao umeonekana kukumbatiwa na serikali na baadhi ya wabunge.

''Mbunge amefikia hatua ya kuwaita wapiga kura wake wahuni, hii ni hatari, lakini siku nchi hii ikiamka kutoka katika ujinga na wananchi wakaamua kuitafuta haki yao, vita itaibuka hapa nchini nadhani wabunge wanaweza kujifunza kwa mfano wa Kenya,'' alieleza Mwendwa.

Alisema kukomaa kwa kiburi kwa wabunge wengi dhidi ya wananchi wao ambao ndiyo wapiga kura wao kunatokana na wabunge wengi kuingia bungeni kwa fedha na kuwaonya wabunge

akitumia mfano wa CHitalilo kuwa wanapaswa kuwaheshimu wapiga kura wao kwa vile ndiyo mabosi wao.

''Haya ni matokeo ya wabunge kushinda kwa fedha, dawa yao ni wapiga kura, wakulima kwa wafanyakazi kuwaondoa wabunge kama hawa. Wanajivuna kwa fedha ambazo zimewaingiza madarakani na matokeo yake wamekuwa vinara wa kusimamia ufisadi bungeni na kuutetea badala ya matatizo ya wananchi,'' alisema Mwendwa.

Hata hivyo, katibu huyo amesemaa lawama za wafanyakazi zinaelekezwa kwa serikali kwa vile alidai kuwa ndiyo imeshindwa kuonyesha dhamira ya kweli kwa kupambana na

Ufisadi, hatua ambayo imesababisha serikali kushindwa kutoa ufafanuzi wa suala zima la ufisadi bungeni.
 
nimependa maneno haya niliyotilia rangi

''Mbunge amefikia hatua ya kuwaita wapiga kura wake wahuni, hii ni hatari, lakini siku nchi hii ikiamka kutoka katika ujinga na wananchi wakaamua kuitafuta haki yao, vita itaibuka hapa nchini nadhani wabunge wanaweza kujifunza kwa mfano wa Kenya,'' alieleza Mwendwa

Mwaka jana katika uwanja huu nilitumia maneno ya aina hiyo hiyo, lakini nilishikishwa adabu kweli kweli kwa kusema wanachi wetu wana ujinga (wa kutojua haki na wajibu wao kama raia); ilibidi nibadilishe nitumie neno la kiingereza "ignorance." Nimefurahi kuona kumbe kuna viongozi wengine wanaojua ukweli huo.

Ujinga wa watu wetu ndicho chanzo cha kukua kwa ufisadi nchini; hilo tatizo kubwa sana. Inafikia fisadi mmoja anatumia pesa alizopata kifisadi ku-exploit ujinga wa watu wetu eti ng'ombe wanachinjwa kila kijiji cha walaya ya Bariadi alikopitia fisadi huyo.
 
nimependa maneno haya niliyotilia rangi



Mwaka jana katika uwanja huu nilitumia maneno ya aina hiyo hiyo, lakini nilishikishwa adabu kweli kweli kwa kusema wanachi wetu wana ujinga (wa kutojua haki na wajibu wao kama raia); ilibidi nibadilishe nitumie neno la kiingereza "ignorance." Nimefurahi kuona kumbe kuna viongozi wengine wanaojua ukweli huo.

Ujinga wa watu wetu ndicho chanzo cha kukua kwa ufisadi nchini; hilo tatizo kubwa sana. Inafikia fisadi mmoja anatumia pesa alizopata kifisadi ku-exploit ujinga wa watu wetu eti ng'ombe wanachinjwa kila kijiji cha walaya ya Bariadi alikopitia fisadi huyo.


Ni kweli kabisa.
Sasa kuna ndugu zangu wanaoona matokeo ya huo ujinga tu na kudhani kwamba ndio shida iliko kumbe kuna haja ya kuangalia outside the box na sio ku-discourage wengine. Moja ya matokeo ya ujinga ni FEAR.

Nilibishana sana kazini siku moja ila nilizidiwa kwa maneno maana nilishindwa kueleza kile nilichotaka kusema. Jamaa walisema "watanzania ni waoga", niling'aka vibaya sana. Ukiangalia kuna ukweli lakini FEAR is just a symptom and not something to dwell upon maana that is not an issue.

Kwa bahati siku mbili baadae nikiwa nasoma kitabu cha Dale Carnegie "How to develop self-confidence & Influence people by public speaking" nikaona haya ambayo ningependa ku-share nanyi:

"Fear is begotten of ignorance and uncertainty", says Professor Robinson in (The Mind in the Making). To put it another way: it is the result of not knowing what you can really do. And not knowing what you can do is caused by a lack of experience. When you get a record of successful experience behind you, your fears will vanish; they will melt like night mists under the glare of a July sun.



.
 
Ningefurahi Kama Vikundi Vingine, Kama Tamwa, Vikundi Vya Dini, Ngo , Vyama Vya Siasa Vingemlaani Fedhulio Huyu!

Ee Bwana Usiwaache Wanyonge Wako, Bali Uwe Upande Wao. Kamwe Bwana Usiwakumbatie Hawa Wanaokula Vya Yatima Na Wajane, Bali Uwe Mtetezi Wao Wale Wanaokemea Na Kuwaanika Mafedhuli Hawa

Kwa Kuwa Ee Bwana, Usipokuwa Upande Wetu , Watu Hawa Na Ufedhuli Wao Watajitangazia Ushindi, Nao Watatupuuza Na Kusema Tazama Hawa Wanamwabudu Asiye Na Msaada Kwao

Bwana Ulilnde Taifa Hili, Wape Watu Wako Ari Ya Kukemea Mbwa Mwitu Hawa. Uwajaze Katika Magereza Wale Wanajishibisha Jasho La Wavuja Jasho, Ee Bwana Twakuomba
 
Nilikuwa siamini kuwa kuna wabunge wenye uwezo mdogo hadi pale nilipoweza kumsikia huyu akichangia na kusema mambo ya ajabu.

Kuna haja sasa ya kupitishwa kwa sheria ambayo itawawezesha wananchi kumpigia kura ya kukosa imani naye mbunge kama akifanya matendo ya kuudhi kama huyu jamaa.

wananchi wapewe mamlaka ya kumwajibisha mbunge now.
 
....walitegemea nini walipomchagua huku wakijua hana hata darasa moja na kafoji vyeti? walipokuwa wanasaidiana kwa kutumia pesa za EPA kushinda ubunge haukuwa uhuni ila sasa kuitwa wahuni na muhuni mwenzao ndio kosa...wahuni tuu hao hawana mpya ila najua 2010 watashinda tena!
 
....walitegemea nini walipomchagua huku wakijua hana hata darasa moja na kafoji vyeti? walipokuwa wanasaidiana kwa kutumia pesa za EPA kushinda ubunge haukuwa uhuni ila sasa kuitwa wahuni na muhuni mwenzao ndio kosa...wahuni tuu hao hawana mpya ila najua 2010 watashinda tena!

Tusiwahukumu wananchi hawa huenda walikuwa hawana taarifa kwani kwenye taifa hili idara ya usalama huwa haifanyi verting ya viongozi wake kabla .
 
Tusiwahukumu wananchi hawa huenda walikuwa hawana taarifa kwani kwenye taifa hili idara ya usalama huwa haifanyi verting ya viongozi wake kabla .

...hakuna excuse hapo,na kumbe unaelewa umuhimu wa verting...haya tunapoomba BIO za hawa watu tuna maana nzuri!
 
Tusiwahukumu wananchi hawa huenda walikuwa hawana taarifa kwani kwenye taifa hili idara ya usalama huwa haifanyi verting ya viongozi wake kabla .

Mkuu, hapa sikuelewi.

Yaani ukitaka kugombea ubunge ni wajibu wa usalama wa taifa kukufanyia "vetting"?

Tafwadhali mkuu!
 
Mimi nadhani huyu mbunge ndiye mjinga kwa kuwaita wapiga kura wake kuwa ni wajinga.
Ningekuwa maeneo ya Mwanza wakati wa kampeni zijazo ningewakumbusha watu kuwa itakuwa ni ujinga kumpigia tena kura mtu aliyewaita wao wajinga.
 
nimependa maneno haya niliyotilia rangi



Mwaka jana katika uwanja huu nilitumia maneno ya aina hiyo hiyo, lakini nilishikishwa adabu kweli kweli kwa kusema wanachi wetu wana ujinga (wa kutojua haki na wajibu wao kama raia); ilibidi nibadilishe nitumie neno la kiingereza "ignorance." Nimefurahi kuona kumbe kuna viongozi wengine wanaojua ukweli huo.

Ujinga wa watu wetu ndicho chanzo cha kukua kwa ufisadi nchini; hilo tatizo kubwa sana. Inafikia fisadi mmoja anatumia pesa alizopata kifisadi ku-exploit ujinga wa watu wetu eti ng'ombe wanachinjwa kila kijiji cha walaya ya Bariadi alikopitia fisadi huyo.

Heshima mbele mkuu Kichuguu!
You're absolutely right to use term ujinga! Ni mtu tu asiyetaka kukubali ukweli na hali halisi ya watanzania walio wengi kwamba wako gizani kifikra, na huo ndio ujinga wenyewe. Kutokukubaliana na ukweli huu kwamba wengi wetu ni wajinga, hakutusaidii kitu zaidi ya kufanya tatizo kuwa sugu! Imefika wakati sasa transparency inahitajika ili tusonge mbele, na mojawapo ni kukubali mapungufu yetu, kama hilo la kuwa na wajinga wengi.
Ahsante mkuu.
 
Inafikia fisadi mmoja anatumia pesa alizopata kifisadi ku-exploit ujinga wa watu wetu eti ng'ombe wanachinjwa kila kijiji cha wilaya ya Bariadi alikopitia fisadi huyo.

Masikini wee, Ng'ombe wa Bariadi,
Yaani nyie ndugu zangu wa Bariadi mkawatoa ng'ombe kibao KAFARA kama Ibrahim na mwanae Issac? Ving'ombe vya watu si kuwa vilichinjwa kwa ili watu wagange njaa, la hasha. Vilichinjwa ili mtu ASAFISHE DHAMBI ZAKE. Ila dhambi hizi badala ya kusafishwa, zilitapakaa mwili mzima wa FISADI na matokeo yake "Damu hiyo SAFI ya ng'ombe" ikamuumbua HEKALUNI mwa Siasa (Bunge). Don't mess up with BLOOD, for sure itakutokea PUANI.
 
Nilikuwa siamini kuwa kuna wabunge wenye uwezo mdogo hadi pale nilipoweza kumsikia huyu akichangia na kusema mambo ya ajabu.

Kuna haja sasa ya kupitishwa kwa sheria ambayo itawawezesha wananchi kumpigia kura ya kukosa imani naye mbunge kama akifanya matendo ya kuudhi kama huyu jamaa.

wananchi wapewe mamlaka ya kumwajibisha mbunge now.

  • .........Kwani hujui kuwa wabunge wetu wengi wameupata kwa kuununua siyo kwa kujinadi kulingana na uwezo wao?
  • .........Kwani ulikuwa hujui kuwa kuna wabunge wengi sana wenye elimu za kubabaisha huku wakitembea na vyeti vya kununua, wengine wao wana madaraka hadi serikalini?
  • .........Kwani ulikuwa hujui kuwa Mbunge huyu alighushi veyti vha shule? lakini kwa vile anatoka chama chenye serikali, hakuchukuliwa hatua yoyote ya kisheria mpaka mtukufu rais naye akampigia debe kuwa Kelele za wanachi hazimzuii kupata usingizi
  • .........Kwani hujui kuwa wabunge wetu wengiu sana huwa hawasomi kabisa ripoti wanazopewa bungeni?
  • .........Kwani ulikuwa hujui kuwa wakati wa vikao vya bunge, sehemu kubwa ya wabunge wetu huwa ama wamelala usingizi au wamekwenda gest na changudoa?
  • Ni kweli, na niliwahi kulizungumzia hili hapa kijiweni mwaka jana: tunahitaji kuwepo na sheria chini ya katiba kuwa mbunge au rais wakilegea na kushindwa majukumu waliyopewa na wanachi, basi wananchi wawe na mechanism ya kuwaondoaa madarakani hata klabla ya miaka mitano kupita. Kuna rafiki yangu mmoja huwa anasema "Time has no mercy on sluggish movers;" tukienda mwendo wa kusuasua na kuwasubiri wapuuzi hawa hadi wamalize miaka mitano yao, tutajikuta tunamaliza karne ya uhuru bila kuwa na maendeleo yoyote yale.
 
Back
Top Bottom