BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,011
Date::9/19/2008
Wafanyakazi nane wa BoT kortini Dar kwa kughusi vyeti
Baadhi ya wafanyakazi wa Benki Kuu (BoT) wakificha nyuso zao baada ya kufikishwa mahakamani Dar es Salaam, Ijumaa wakikabiliwa na makosa ya kughushi vyeti vya shule.
Ramadhan Semtawa na Nora Damiani
Mwananchi
TUHUMA za kuwepo kwa upendeleo wa watoto wa vigogo kwenye ajira za Benki Kuu ya Tanzania (BoT), zimesimamisha kizimbani wafanyakazi wanane ambao wameshtakiwa kwa kosa la kughushi vyeti.
Tuhuma dhidi ya watoto 16 wa vigogo ziliibuka wakati kashfa ya wizi wa fedha za Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), ikiwa imeshamiri kiasi cha kusababisha aliyekuwa gavana, Daud Ballali kusitishwa mkataba wake na kufanyika kwa mabadiliko kadhaa kwenye uongozi wa chombo hicho nyeti cha fedha.
Na Gavana wa BoT, Profesa Benno Ndulu, aliahidi kuzishughulikia tuhuma hizo wakati huo baada ya tuhuma hizo kushikiwa bango.
Jana, wafanyakazi wanane wa BoT, baadhi yao wakiwa wamejifunika nyuso kwa nguo na nywele za bandia, walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakishtakiwa kwa tuhuma za kughushi vyeti na kutoa hati za uongo.
Wafanyakazi hao, wengi wao wakiwa wanawake, ni Justina J Mungai, ambaye imeelezwa kuwa ni mtoto wa Joseph Mungai, ambaye amewahi kushika wizara tofauti ikiwemo ya elimu, Christina G Ntemi, Siamini Eddie Kombakono, Janeth John Mahenge, Beatha Constantine Massawe, Jacquiline David Juma, Philimina Philibert Mutagurwa na Amina Mohamed Mwinchumu.
Wafanyakazi hao walifikishwa katika mahakama hiyo saa 4.00 asubuhi na kusomewa shtaka mbele ya Hakimu Neema Chusi. Wakili wa serikali, Edgar Luoga, akisaidiana na Mwendesha Mashtaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Abubakar Msangi, ndio walioongoza mashtaka hayo.
Washtakiwa hao kwa pamoja wanadaiwa kughushi vyeti vya kuhitimu kidato cha nne na kutoa hati za uongo kwa mwajiri wao, ambaye ni BoT.
Washtakiwa Mungai, Massawe na Mwinchumu, wanadaiwa kughushi vyeti hivyo mwaka 2001, wakati Ntemi, Kombakono, Mahenge na Mutagurwa wanadaiwa kughushi vyeti hivyo mwaka 2002.
Wanadaiwa kughushi vyeti vya kuhitimu kidato cha nne na kutoa BoT hati za uongo, wakionyesha kuwa vimetolewa na Baraza la Mitihani la Taifa, wakati si kweli.
Ilidaiwa kuwa, Mutagurwa alighushi cheti hicho mwaka 2000.
Washtakiwa wote walikana kufanya makosa hayo na upande wa serikali ulisema upelelezi wa kesi hiyo umekamilika na kuomba tarehe nyingine kwa ajili ya kuwasomea maelezo ya awali.
Hakimu Chusi alitoa masharti ya dhamana na kila mshtakiwa alitakiwa awe na wadhamini wawili, ambao ni watumishi wa serikali watakaosaini dhamana ya Sh5milioni. Pia wadhamini hao walitakiwa wawe na barua za waajiri wao na kwamba, hawatakiwi kusafiri nje ya Mkoa wa Dar es Salaam bila kibali maalumu cha mahakama.
Mshtakiwa wa saba Mutagurwa, alitimiza masharti ya dhamana na kuachiwa nje kwa dhamana, wakati washtakiwa wengine walirudishwa rumande hadi Oktoba 6 watakaposimamishwa tena kizimbani.
Habari zilizopatikana nje ya mahakama na kuthibitishwa na mmoja wa mawakili wa serikali, zilisema kuwa, washtakiwa hao wote wanafanya kazi ya kuhesabu fedha BoT.
Wakati tayari baadhi ya watoto wa vigogo wakiwa wamefikishwa mahakamani, Gavana wa BoT, Prof Ndulu alisema, benki hiyo itahakikisha wote walioghushi vyeti wanachukuliwa hatua za kiutawala.
Hatua ya BoT kuhakiki majina ya watoto wa vigogo na watumishi wote, kwa mara ya kwanza iliripotiwa na gazeti hili Mei 29 baada ya kuzungumza na Gavana Ndulu.
Akifafanua operesheni hiyo, Profesa Ndulu alisema, kazi kubwa ya BoT katika mchakato huo ni kuchukua hatua za kinidhamu na za kiutawala huku zile za kinidhamu zikichukuliwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru).
Gavana Profesa Ndulu alifafanua kwamba, kwa sasa BoT iko katika hatua za mwisho za kukamilisha zoezi zima la uhakiki wa watumishi wake wote ambao wametajwa katika kipindi husika.
"Operesheni itaendelea. Sisi tunafanya kazi yetu na kuchukua hatua za kinidhamu, lakini wenzetu Takukuru wanafanya kwa upande wa jinai," alisema Profesa Ndulu.
Akifafanua sehemu ya hatua iliyofikiwa, Profesa Ndulu alisema, baadhi ya wafanyakazi wanaoghushi wameshachunguzwa na benki na kuonekana kuwa wameongeza sifa zao.
"Utakuta kipindi kile mtu alikuwa na sifa fulani, lakini watu wamesoma na baadhi hata kufikia katika viwango husika vya elimu. Lakini bado mchakato unaendelea vizuri na uko katika hatua za mwisho, sisi kila taarifa tunayopata tunawapa Takukuru," alisisitiza.
Miongoni mwa watoto ambao majina yao yanatajwa ni pamoja na watoto wa Rais Mstaafu Benjamin Mkapa, aliyekuwa Waziri Mkuu, Frederick Sumaye, Edward Lowassa na gavana wa zamani, marehemu Daud Ballali.
Ajira za watoto hao zinahusishwa na ushawishi wa nafasi za baba zao, wakati wakiwa madarakani.
Wafanyakazi nane wa BoT kortini Dar kwa kughusi vyeti
Baadhi ya wafanyakazi wa Benki Kuu (BoT) wakificha nyuso zao baada ya kufikishwa mahakamani Dar es Salaam, Ijumaa wakikabiliwa na makosa ya kughushi vyeti vya shule.
Ramadhan Semtawa na Nora Damiani
Mwananchi
TUHUMA za kuwepo kwa upendeleo wa watoto wa vigogo kwenye ajira za Benki Kuu ya Tanzania (BoT), zimesimamisha kizimbani wafanyakazi wanane ambao wameshtakiwa kwa kosa la kughushi vyeti.
Tuhuma dhidi ya watoto 16 wa vigogo ziliibuka wakati kashfa ya wizi wa fedha za Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), ikiwa imeshamiri kiasi cha kusababisha aliyekuwa gavana, Daud Ballali kusitishwa mkataba wake na kufanyika kwa mabadiliko kadhaa kwenye uongozi wa chombo hicho nyeti cha fedha.
Na Gavana wa BoT, Profesa Benno Ndulu, aliahidi kuzishughulikia tuhuma hizo wakati huo baada ya tuhuma hizo kushikiwa bango.
Jana, wafanyakazi wanane wa BoT, baadhi yao wakiwa wamejifunika nyuso kwa nguo na nywele za bandia, walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakishtakiwa kwa tuhuma za kughushi vyeti na kutoa hati za uongo.
Wafanyakazi hao, wengi wao wakiwa wanawake, ni Justina J Mungai, ambaye imeelezwa kuwa ni mtoto wa Joseph Mungai, ambaye amewahi kushika wizara tofauti ikiwemo ya elimu, Christina G Ntemi, Siamini Eddie Kombakono, Janeth John Mahenge, Beatha Constantine Massawe, Jacquiline David Juma, Philimina Philibert Mutagurwa na Amina Mohamed Mwinchumu.
Wafanyakazi hao walifikishwa katika mahakama hiyo saa 4.00 asubuhi na kusomewa shtaka mbele ya Hakimu Neema Chusi. Wakili wa serikali, Edgar Luoga, akisaidiana na Mwendesha Mashtaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Abubakar Msangi, ndio walioongoza mashtaka hayo.
Washtakiwa hao kwa pamoja wanadaiwa kughushi vyeti vya kuhitimu kidato cha nne na kutoa hati za uongo kwa mwajiri wao, ambaye ni BoT.
Washtakiwa Mungai, Massawe na Mwinchumu, wanadaiwa kughushi vyeti hivyo mwaka 2001, wakati Ntemi, Kombakono, Mahenge na Mutagurwa wanadaiwa kughushi vyeti hivyo mwaka 2002.
Wanadaiwa kughushi vyeti vya kuhitimu kidato cha nne na kutoa BoT hati za uongo, wakionyesha kuwa vimetolewa na Baraza la Mitihani la Taifa, wakati si kweli.
Ilidaiwa kuwa, Mutagurwa alighushi cheti hicho mwaka 2000.
Washtakiwa wote walikana kufanya makosa hayo na upande wa serikali ulisema upelelezi wa kesi hiyo umekamilika na kuomba tarehe nyingine kwa ajili ya kuwasomea maelezo ya awali.
Hakimu Chusi alitoa masharti ya dhamana na kila mshtakiwa alitakiwa awe na wadhamini wawili, ambao ni watumishi wa serikali watakaosaini dhamana ya Sh5milioni. Pia wadhamini hao walitakiwa wawe na barua za waajiri wao na kwamba, hawatakiwi kusafiri nje ya Mkoa wa Dar es Salaam bila kibali maalumu cha mahakama.
Mshtakiwa wa saba Mutagurwa, alitimiza masharti ya dhamana na kuachiwa nje kwa dhamana, wakati washtakiwa wengine walirudishwa rumande hadi Oktoba 6 watakaposimamishwa tena kizimbani.
Habari zilizopatikana nje ya mahakama na kuthibitishwa na mmoja wa mawakili wa serikali, zilisema kuwa, washtakiwa hao wote wanafanya kazi ya kuhesabu fedha BoT.
Wakati tayari baadhi ya watoto wa vigogo wakiwa wamefikishwa mahakamani, Gavana wa BoT, Prof Ndulu alisema, benki hiyo itahakikisha wote walioghushi vyeti wanachukuliwa hatua za kiutawala.
Hatua ya BoT kuhakiki majina ya watoto wa vigogo na watumishi wote, kwa mara ya kwanza iliripotiwa na gazeti hili Mei 29 baada ya kuzungumza na Gavana Ndulu.
Akifafanua operesheni hiyo, Profesa Ndulu alisema, kazi kubwa ya BoT katika mchakato huo ni kuchukua hatua za kinidhamu na za kiutawala huku zile za kinidhamu zikichukuliwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru).
Gavana Profesa Ndulu alifafanua kwamba, kwa sasa BoT iko katika hatua za mwisho za kukamilisha zoezi zima la uhakiki wa watumishi wake wote ambao wametajwa katika kipindi husika.
"Operesheni itaendelea. Sisi tunafanya kazi yetu na kuchukua hatua za kinidhamu, lakini wenzetu Takukuru wanafanya kwa upande wa jinai," alisema Profesa Ndulu.
Akifafanua sehemu ya hatua iliyofikiwa, Profesa Ndulu alisema, baadhi ya wafanyakazi wanaoghushi wameshachunguzwa na benki na kuonekana kuwa wameongeza sifa zao.
"Utakuta kipindi kile mtu alikuwa na sifa fulani, lakini watu wamesoma na baadhi hata kufikia katika viwango husika vya elimu. Lakini bado mchakato unaendelea vizuri na uko katika hatua za mwisho, sisi kila taarifa tunayopata tunawapa Takukuru," alisisitiza.
Miongoni mwa watoto ambao majina yao yanatajwa ni pamoja na watoto wa Rais Mstaafu Benjamin Mkapa, aliyekuwa Waziri Mkuu, Frederick Sumaye, Edward Lowassa na gavana wa zamani, marehemu Daud Ballali.
Ajira za watoto hao zinahusishwa na ushawishi wa nafasi za baba zao, wakati wakiwa madarakani.