DOKEZO Wafanyakazi Hospitali ya K's - Mbeya wana hali mbaya, Wamiliki nao hawajali na wanawajibu kwa nyodo

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

BigTall

JF-Expert Member
Mar 9, 2022
422
1,049
Nakumbuka mwaka jana niliona kuna memba mmoja wa JF aliandika kuhusu huduma mbovu zinazotolewa na Hospitali ya K’s iliyopo Mbeya, sikuwa nimeweka umakini sana lakini kilichotokea wiki hii ndio nimeona kweli hiyo hospitali ni ya kidwanzi.

Wiki moja iliyopita nilifika hospitalini hapo si kwa lengo la kutibiwa bali kumsalimia ndugu yangu ambaye ni mtumishi wa Hospitali ya K’s kwa miaka kadhaa sasa.

Baada ya stori zetu za hapa na pale nikabaini kuwa mshkaji hana furaha na sura yake ni kama imekosa nusu, nikamdadidi tatizo nini hakuweza kuniambia, akasema tutazungumza baadaye, kwa kuwa nilikuwa ni mwenyeji wake kwa wiki nzima haikuwa tabu.

aadaye jamaa alinisimulia mambo mengi hasa jinsi watumishi wa hospitali hiyo wanavyopata tabu hasa kiuchumi na kunyanyasika.
2020-01-26.jpg
Nadhani litakuwa jambo zuri nikimnukuu yeye mwenyewe japokuwa naweza kutoandika moja kwa moja kwa maana ya neno kwa neno alilosema lakini ukimaliza kusima ujumbe utakuwa umeeleweka na kama ni hatua basi Serikali au taasisi husika ziingilie kati kuwasaidia ndugu zetu hao.

“Hospitali ya K’s ina jina kubwa hapa Mbeya lakini ukweli ni kuwa kinachoendelea ndani ni aibu sana, kwanza hapa ninavyokwambia tunadai mishahara ya miezi 9 na huu Juni unaenda kuwa wa 10.

“Mara ya mwisho tulilipwa Februari 2023 lakini nyuma ya haoo kuna mishahara mingine ambayo tunadai, tukiuliza wanatuambia watalipa, mara NHIF hawajalipa, kwa ufupi blabla zinakuwa nyingi.

“Kuna kipindi madaktari waligoma kwa kutolipwa stahiki zao, lakini wakapewa majibu ya shombo kutoka kwa viongozi wa juu wakiwemo wamiliki wenyewe.

“Ilifika hatua jamaa wakaanza kujibu kwa nyodo kuwa hata tukiondoka wao wanaweza kubaki na watoto wao ambao ni madaktari tuko nao hapa, watafanya kazi kama kawaida.

“Kuna muda inafikia watu wanafukuzwa kazi kwa makosa ya ajabuajabu ilimradi tu wasiweze kudai maslahi yao, pia kuna washkaji wengi tu wameacha kazi hapa kutokana na mambo kutoeleweka.

“Kwa ufupi Wafanyakazi tuna hali mbaya na sisi ndio tunaodili na afya za watu, unadhani hapo kuna umakini kweli?”

Hiyo ni sehemu ya maelezo ya ndugu yangu, naomba Serikali iingiilie kati kuwasaidia wana hali mbaya ndugu zetu ambao wanadili na afya za watu, unadhani hapo tutegemee nini?

==================

Updates...
Walipotafutwa kujibu madai hayo kwa nyakati tofauti, Afisa Uhusiano wa Hospitali ya K’s, Suma Kabuje na Meneja wa K’s wote walisikiliza hoja kisha wakaomba muda kabla ya kujibu lakini bado hawajapatikana kutoa ufafanuzi.

Pia soma : Hospitali ya K’s Mbeya mna huduma mbovu
 
Nakumbuka mwaka jana niliona kuna memba mmoja wa JF aliandika kuhusu huduma mbovu zinazotolewa na Hospitali ya K’s iliyopo Mbeya, sikuwa nimeweka umakini sana lakini kilichotokea wiki hii ndio nimeona kweli hiyo hospitali ni ya kidwanzi.

Wiki moja iliyopita nilifika hospitalini hapo si kwa lengo la kutibiwa bali kumsalimia ndugu yangu ambaye ni mtumishi wa Hospitali ya K’s kwa miaka kadhaa sasa.

Baada ya stori zetu za hapa na pale nikabaini kuwa mshkaji hana furaha na sura yake ni kama imekosa nusu, nikamdadidi tatizo nini hakuweza kuniambia, akasema tutazungumza baadaye, kwa kuwa nilikuwa ni mwenyeji wake kwa wiki nzima haikuwa tabu.

aadaye jamaa alinisimulia mambo mengi hasa jinsi watumishi wa hospitali hiyo wanavyopata tabu hasa kiuchumi na kunyanyasika.
Nadhani litakuwa jambo zuri nikimnukuu yeye mwenyewe japokuwa naweza kutoandika moja kwa moja kwa maana ya neno kwa neno alilosema lakini ukimaliza kusima ujumbe utakuwa umeeleweka na kama ni hatua basi Serikali au taasisi husika ziingilie kati kuwasaidia ndugu zetu hao.

“Hospitali ya K’s ina jina kubwa hapa Mbeya lakini ukweli ni kuwa kinachoendelea ndani ni aibu sana, kwanza hapa ninavyokwambia tunadai mishahara ya miezi 9 na huu Juni unaenda kuwa wa 10.

“Mara ya mwisho tulilipwa Februari 2023 lakini nyuma ya haoo kuna mishahara mingine ambayo tunadai, tukiuliza wanatuambia watalipa, mara NHIF hawajalipa, kwa ufupi blabla zinakuwa nyingi.

“Kuna kipindi madaktari waligoma kwa kutolipwa stahiki zao, lakini wakapewa majibu ya shombo kutoka kwa viongozi wa juu wakiwemo wamiliki wenyewe.

“Ilifika hatua jamaa wakaanza kujibu kwa nyodo kuwa hata tukiondoka wao wanaweza kubaki na watoto wao ambao ni madaktari tuko nao hapa, watafanya kazi kama kawaida.

“Kuna muda inafikia watu wanafukuzwa kazi kwa makosa ya ajabuajabu ilimradi tu wasiweze kudai maslahi yao, pia kuna washkaji wengi tu wameacha kazi hapa kutokana na mambo kutoeleweka.

“Kwa ufupi Wafanyakazi tuna hali mbaya na sisi ndio tunaodili na afya za watu, unadhani hapo kuna umakini kweli?”

Hiyo ni sehemu ya maelezo ya ndugu yangu, naomba Serikali iingiilie kati kuwasaidia wana hali mbaya ndugu zetu ambao wanadili na afya za watu, unadhani hapo tutegemee nini?


Pia soma : Hospitali ya K’s Mbeya mna huduma mbovu
Haya ni majungu .
Msimuliaji si mfanyakazi hapo K, halafu anahadithia alichoambiwa
Junguzzzzz!!!
 
Itakua na wewe ni miongoni mwa watu waliofukuzwa kwa wizi so umeona ulete majungu,ks hospital mbeya is the best,maabara yao ni kati ya maabara mora kabisa katika vipimo
 
Huyu ni mfanyakazi wa pale Male's kutolipwa kwako mshahara kunamuhusu nn mgonjwa si uache kazi tu kuliko kuhatarisha maisha ya watu wasokuwa na hatia na hawajui nn utapitia hapo kazini kwako..kwa nn usipambane na muajiri wako ..hapo ndo.mnapofeli kama unaona hawalipi acha kazi kama unaweza kusurvive miezi yote hiyo bila mshahara unashindwa nn kusepa ondoka hapo sio sehemu sahihi kwako kayafute palipo na green pasture utulize komwe...uvivu wa kufikiri ndo umewambia gundi mbaki hapo fanyeni maamuzi maisha yaendelee
 
Yani mmeajiriwa na mnafanya kazi hamlipwi bado mpo tu mnaendelea kufanya kazi? Hii si inathibitisha kwamba mmekubali kufanya kazi bila malipo?

Halafu, hapa ni sehemu sahihi pa kuleta malalamiko yenu?

Hii nchi masifuri mengi ni wale watu tunaodhani walienda shule.
 
Mzee ukiwa kwenye ajira unaweza kupata michongo mingine hata kama haulipwi, inawezekana anapata michongo mingine kupitia jina la taasisi hiyo
Wizi mtupu.

Nini maana ya "michongo" kwenye ajira?

Tajiri aliyemuajiri na halipi siyo mjinga kutofahamu hilo.
 
Hiyo mbinu alio tumia kuishi miezi yote hiyo bila kulipwa mshahara, aitumie mbinu hiyohiyo kuishi baada ya kuacha kazi na kisha akawashtaki CMA
Hawa k'S Wana ajiri watu ambao hawana professional yeyote

Kuna jamaa alisoma HKL lakini ni doctor pale

Unategemea huyu akiacha kazi ataajirika wapi?
 
Back
Top Bottom