Wafanyakazi 10 wa Mfalme wa OBC, Loliondo wapanda kizimbani

Jembe Jembe

JF-Expert Member
Jun 9, 2016
749
1,797
Wafanyakazi 10 raia wa kigeni wenye asili ya Asia wa kasri la mfalme wa Abu dhabi inayosimamiwa na Kampuni ya Ortelo Business Coparation(OBC) iliyopo eneo la Loliondo wilayani Ngorongoro,Mkoani hapa wamepandishwa kizimbani kwa kosa la kufanyakazi nchini kinyume cha sheria za ajira kwa wageni .

Wakisomewa mashtaka mapema leo mbele ya Hakimu mfawidhi wa mahakama ya hakimu mkazi Arusha, Niku Mwakatobe Mwendesha mashtaka wa Idara ya kazi mkoani hapa, Immanuel Mweta alidai kuwa mnamo Novemba 2018 hadi januari 2019 washtakiwa hao walitenda kosa la kufanya kazi kinyume na sheria ya kuratibu ajira za wageni.

Mweta aliwataja washtakiwa hao kuwa ni Darweshi Jumma,Riaz Aziz Khan,Mohammad Tayyab,Ali Bakhash,Abdulrahman Mohammed,Martin Crasta,Imtiaz Feyaz,Arshad Muhammad,hamza Sharif na Zulfiqar Ali ambao wanashitakiwa kwa kosa la kufanyakazi kinyume cha sheria za uratibu wa wageni na kutokuwa na vibali vya kufanyakazi nchini.

Washtakiwa hao ambao walikuwa hawajui lugha ya Kiswahili wa kiingereza na kutumia mkalimani aliyetambulika kwa jina la Muazamu Husein walikana makosa yao na kusema kuwa kampuni hiyo iliwaleta bila wao kujua chochote na wana uhakika na vibali walivyo navyo.

Washtakiwa hao walikuwa wakiwakilishwa na mawakili wawili Godluck Peter akisaidiana na Daud Haraka wakili haraka aliiomba mahakama kuwapatia dhamana washtakiwa hao kwani kosa linalo wakabili linastahili dhamana.

Wakili wa Upande wa mashtaka ,Mweta alidai hawana pingamizi lolote juu ya dhamana ya washtakiwa ila dhamana ifuate utaratibu wa mahakama.

Hakimu Mwakatobe alisema dhamana kwa washtakiwa wote ipo wazi na kila moja anapaswa kuwa na wadhamini wawili wenye barua za utambulisho na vitambulisho na mali kauli ya thamani ya million Tano.

Washtakiwa hao walikidhi dhamana na wapo nje na kesi hiyo imeahirishwa hadi Tarehe 22 mwezi 2 mwaka huu itakapotajwa tena.

Akiongea nje ya Mahakama,Afisa wa idara ya kazi mkoa wa Arusha, Alfred Mdumi alisema watuhumiwa hao walikamatwa juzi na maofisa wabuhamiaji mkoani hapa wakati wakijaribu kutoroka kuelekea nchini Dubai.




IMG_20190207_150549.jpeg
IMG_20190207_150600.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Copied from somewhere:

--------------------

Wafanyakazi 11 wa Mfalme watupwa rumande Arusha

Mgogoro wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Umoja wa Nchi za Falme za Kiarabu (UAE) unafukuta baada ya wafanyakazi 11, akiwamo Mkurugenzi wa kampuni ya Otterlo Business Corporation (OBC), kukamatwa na kuwekwa rumande.

Wafanyakazi hao wamekamatwa kutokana kwa agizo la Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo, na baadaye Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola.

Kampuni ya OBC inajihusisha na uwindaji wa kitalii katika Pori Tengefu la Liliondo, Ngorongoro mkoani Arusha.

Kwa miaka 20 timu ya wafanyakazi hao imekuwa ikiingia nchini kwa ajili ya kufanya maandalizi ya kiufundi kabla ya ujio wa mfalme.

Taarifa kutoka Polisi mkoani Arusha zinasema watu hao 10 walifika nchini miezi mitatu iliyopita na kupata visa halali ya kuwawezesha kufanya kazi za maandalizi ya ujio wa mfalme huyo.

Visa zao zilikuwa zinakwisha muda Fabruari 7, mwaka huu, lakini walikamatwa Februari 6 wakiwa wanaenda Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) kwa ajili ya kurejea Uarabuni.

Kumekuwapo mvutano mkali ndani ya Idara ya Kazi, Uhamiaji na Jeshi la Polisi, kwa baadhi ya watumishi kusita kuwakamata wafanyakazi hao kutokana na ukweli kuwa wameingia na kufanya kazi kulingana na masharti yaliyomo kwenye visa zao (Business Visa).

Fabruari 13 jioni, Mkurugenzi wa OBC, Isack Mollel, alikamatwa kwa agizo la Waziri Lugola, kwa kile kinachoelezwa kuwa ni maelezo ya upande mmoja aliyopewa na Gambo, aliyedai kuwa watu hao walikuwa wakifanya kazi nchini bila vibali.

Duru za uchunguzi zinaonesha kuwa mvutano juu ya kukamatwa kwa wafanyakazi hao ulifika ngazi za juu za uongozi nchini, hali iliyomlazimu Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, kuagiza wizara tatu za Mambo ya Ndani ya Nchi, Wizara ya Maliasili na Utalii; na Wizara ya Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuum, Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Watu Wenye Ulemavu, zikutane kwa lengo la kumaliza suala hilo kwa njia zitakazosaidia kulinda uhusiano kati ya Tanzania na Falme hizo.

Kutokana na maelekezo hayo, Fabruari 7, mwaka huu wizara hizo zilitaarifiwa kuhusu msimamo huo kutoka juu, lakini bado wafanyakazi hao wameendelea kunyimwa pasi zao na hivyo kuwafanya wakwame kurejea.

Licha ya kuwapo maelekezo ya kiutawala ya kuachiwa wafanyakazi hao yaliyotolewa na Waziri Mkuu, jana Waziri Lugola, aliagiza Mollel akamatwe ili aunganishwe kwenye tuhuma hizo.

Kwa upande wake, OBC wanasema kwa miaka yote wamekuwa wakiwapokea wafanyakazi hao na kupata “Business Visa” kwa dola 250 za Marekani kwa kila mmoja, kwa muda wa miezi mitatu.

“Mfalme anapokaribia kuja hutumwa wafanyakazi kwa ajili ya kuandaa mahitaji, kubainisha vitu vilivyokwisha muda, kurekebisha vifaa kwenye magari maalumu anayotumia mfalme, kuandaa masuala yote yanayohusu usalama wa vitu anavyotumia mfalme, na kadhalika.

“Kisheria, watu wanaofanya hizo kazi za muda mfupi hupewa ‘Business Visa’ zinazodumu kwa miezi mitatu tu. Ni sheria, wala hawahitaji kibali cha kufanya kazi nchini kwa sababu kazi zao ni za muda mfupi na ni za kitaalamu.

“Kukamatwa kwa watumishi hao kwa kweli ni shinikizo na tunaweza kusema ni chuki binafsi za baadhi ya wanasiasa kwa sababu hakuna hata sheria moja tuliyovunja,” amesema mmoja wa viongozi wa OBC.

Mmoja wa maofisa wa Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Arusha, aliyezungumza kwa masharti ya kutotajwa jina amesema, “Hawana kosa lolote, waliomba na kupewa business visa; kisheria kwa kazi zao wanastahili. Walifuata taratibu zote, lakini tumeambiwa sasa wawekwe rumande na wafikishwe mahakamani. Kwa upande wetu hatuna kitu cha kuwashitaki maana walifuata taratibu zote za kisheria.”

Ofisa wa Idara ya Kazi mkoani hapa, amesema wamelazimishwa kuwashitaki wageni hao licha ya kutoona kosa lao. “Hapa kuna siasa, Loliondo ina siasa nyingi, hili jambo halijakaa sawa kabisa.”

Habari zilizopatikana kutoka Wizara ya Mambo ya Nje zinasema tayari Umoja wa Falme za Kiarabu umeanza kuuliza kuhusu kutiwa ndani kwa wafanyakazi wake wenye vibali halali.

“Wanauliza, na kuna kila dalili kuwa mfalme ambaye alikuwa afike nchini tarehe 20 huenda akafuta safari yake. Hii ni hasara kubwa kwa nchi. Ugomvi binafsi unapoingizwa kwenye mambo ya nchi unakuwa na athari kubwa,” kimesema chanzo chetu cha habari.
 
Tanzania imelemewa sana na Wahamiaji haramu sanaaaa. Mbaya zaidi Mkuu wa Uhamiaji yule Madam hana amsha amsha kabisaaaaa. Ilipaswa kule Uhamiaji apewe Kamishna ambaye ni mbunifu na Hakuna kulala na Oparesheni zisizokoma. Lkn kwa Kanishna wetu wa sasa HAPANA tunafeli sana na huko RUKWA, KATAVI, TABORA, KIGOMA, TUNDUMA NK wahamiaji haramu hasa Wahutu, Wacongo na Wanyarwanda wanajimegea ardhi tuuu.
 
Kazi Zinaendelea
Muda Huu Sasa Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania, Airudishe Loliondo Tanzania
Nilisikia Iliuzwa Zamani Sana
 
Tunao makanali wastaafu wengi ambao wana nguvu, weledi, uzalendo na uaditifu, apewe mmoja hiyo Uhamiaji atunyoosheee idara. Kuna watendaji wa uhamiaji ambao uraia wao una mashaka, kuna haja, Fabio lianzie uhamiaji kwenyewe, yawezekana wanakwamisha mikakati au kuvujisha
Tanzania imelemewa sana na Wahamiaji haramu sanaaaa. Mbaya zaidi Mkuu wa Uhamiaji yule Madam hana amsha amsha kabisaaaaa. Ilipaswa kule Uhamiaji apewe Kamishna ambaye ni mbunifu na Hakuna kulala na Oparesheni zisizokoma. Lkn kwa Kanishna wetu wa sasa HAPANA tunafeli sana na huko RUKWA, KATAVI, TABORA, KIGOMA, TUNDUMA NK wahamiaji haramu hasa Wahutu, Wacongo na Wanyarwanda wanajimegea ardhi tuuu.
 
Shida tunahangaika na tulipoangukia badala ya kuondoa kisiki tunachojikwaa, hao watumishi wala sio wa kuhangaika nao
Tuangalie uwepo wa OBC kama upo kihalali mengine ni matokeo ya OBC
 
Nimefuatilia hii issue. Hawa jamaa waliingia nchini kwa Business visa ambayo inawaruhusu kufanya kazi kwa muda usiozidi siku 90. Hapa Kuna kaharufu ka matumizi mabovu ya madaraka.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapa naona kuna mkono wa kisiasa zaidi ktk kuliangalia hili jambo ,kuhusu kufanya kazi bila vibali hili lipo wasi sana kwa mataifa mengi ni kuwa kama mshitakiwa amekamatwa hamna cha mlolongo wa kesi bali anapewa faini yake kutokana na muda aliokaa hapa nchini kwa kufanya kazi bila vibali lkn pia inaonekana wana Business Visa

Tatizo lipo kwenye je hiyo kampuni inayo doc za kuifanya kuwa inaweza kuwaajiri wageni? Na je, wageni ni wangapi wanatakiwa kuajiriwa kwa mujibu wa sheria au doc alizopewa kwenye uwekezaji?

Kuanzia hapo ndiyo unaweza kuona nani mwenye makosa na nini kinatakiwa kufanyika.

Hili swala la kuhamaki na kusema tumewakamata Hapa Arusha siyo kuondoa tatizo bali tatizo lipo kwa nchi nzima kuhusu wageni kufanya kazi bila vibali mfano mkubwa na ambao upo wasi nenda kwenye hizi English Medium zetu ndiyo utashangaa

Kwa shule nzuri na ambazo zinapendwa na sisi watanzania ni wawe walimu ni kutoka Kenya au Uganda, sasa linakuja swala la vibali vya hao walimu ndy mshangao mkubwa maana wengine hata hiyo pass ya kusafiria hawana na zaidi wala hamna sehemu kumefanyika uthibitisho wa elimu yake kama inaendana na mataka ya kazi anazofanya.

So kwa hili tunaomba hawa watu wa uhamiaji waweze kufanya ukaguzi kwa nchi nzima kwenye maeneo tofautitofauti na kuwapa vibali rasmi wale wanaostahili na kuwarudisha wale ambao hawastahili.

Kuanzia hapo mnathiti mipaka na kuwabana waajiri kuhusu kutoa ajira kwa wageni ambao hawana vibali
 
Haya ndo makabi ya serikali dhaifu kabisa zilizowahi pitia nchi hii.
 
Tanzania imelemewa sana na Wahamiaji haramu sanaaaa. Mbaya zaidi Mkuu wa Uhamiaji yule Madam hana amsha amsha kabisaaaaa. Ilipaswa kule Uhamiaji apewe Kamishna ambaye ni mbunifu na Hakuna kulala na Oparesheni zisizokoma. Lkn kwa Kanishna wetu wa sasa HAPANA tunafeli sana na huko RUKWA, KATAVI, TABORA, KIGOMA, TUNDUMA NK wahamiaji haramu hasa Wahutu, Wacongo na Wanyarwanda wanajimegea ardhi tuuu.
Acha ubaguzi wewe hao wahutu sio waafrica?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapa tunaona "TATIZO" (Mkuu wa mkoa was Arusha) kama ailivyo ada yake, akilitia taifa hasara kwa mara nyingine tena.
 
Wafanyakazi 10 raia wa kigeni wenye asili ya Asia wa kasri la mfalme wa Abu dhabi inayosimamiwa na Kampuni ya Ortelo Business Coparation(OBC) iliyopo eneo la Loliondo wilayani Ngorongoro,Mkoani hapa wamepandishwa kizimbani kwa kosa la kufanyakazi nchini kinyume cha sheria za ajira kwa wageni .

Wakisomewa mashtaka mapema leo mbele ya Hakimu mfawidhi wa mahakama ya hakimu mkazi Arusha, Niku Mwakatobe Mwendesha mashtaka wa Idara ya kazi mkoani hapa, Immanuel Mweta alidai kuwa mnamo Novemba 2018 hadi januari 2019 washtakiwa hao walitenda kosa la kufanya kazi kinyume na sheria ya kuratibu ajira za wageni.

Mweta aliwataja washtakiwa hao kuwa ni Darweshi Jumma,Riaz Aziz Khan,Mohammad Tayyab,Ali Bakhash,Abdulrahman Mohammed,Martin Crasta,Imtiaz Feyaz,Arshad Muhammad,hamza Sharif na Zulfiqar Ali ambao wanashitakiwa kwa kosa la kufanyakazi kinyume cha sheria za uratibu wa wageni na kutokuwa na vibali vya kufanyakazi nchini.

Washtakiwa hao ambao walikuwa hawajui lugha ya Kiswahili wa kiingereza na kutumia mkalimani aliyetambulika kwa jina la Muazamu Husein walikana makosa yao na kusema kuwa kampuni hiyo iliwaleta bila wao kujua chochote na wana uhakika na vibali walivyo navyo.

Washtakiwa hao walikuwa wakiwakilishwa na mawakili wawili Godluck Peter akisaidiana na Daud Haraka wakili haraka aliiomba mahakama kuwapatia dhamana washtakiwa hao kwani kosa linalo wakabili linastahili dhamana.

Wakili wa Upande wa mashtaka ,Mweta alidai hawana pingamizi lolote juu ya dhamana ya washtakiwa ila dhamana ifuate utaratibu wa mahakama.

Hakimu Mwakatobe alisema dhamana kwa washtakiwa wote ipo wazi na kila moja anapaswa kuwa na wadhamini wawili wenye barua za utambulisho na vitambulisho na mali kauli ya thamani ya million Tano.

Washtakiwa hao walikidhi dhamana na wapo nje na kesi hiyo imeahirishwa hadi Tarehe 22 mwezi 2 mwaka huu itakapotajwa tena.

Akiongea nje ya Mahakama,Afisa wa idara ya kazi mkoa wa Arusha, Alfred Mdumi alisema watuhumiwa hao walikamatwa juzi na maofisa wabuhamiaji mkoani hapa wakati wakijaribu kutoroka kuelekea nchini Dubai.




View attachment 1015859View attachment 1015861

Sent using Jamii Forums mobile app
Safi kabisa, maana nchini kwao kama tungefanya hayo tungefanyiwa hivyo na zaidi...
 
Back
Top Bottom