Wafanyabiashara Kariakoo: Jengo lililoanguka Kariakoo halikubeba tani 850. Hii inamaanisha Rais alipewa taarifa zisizo sahihi?

The Watchman

JF-Expert Member
Nov 7, 2023
508
968
Wafanyabiashara wa Soko la Kariakoo wamehoji juu ya usahihi wa takwimu alizopewa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa jengo la ghorofa lililoanguka Kariakoo Novemba 16, 2024 lilikuwa limebeba mizigo ya tani 850.

Akizungumza leo Februari 04, 2025 katika uzinduzi wa Balozi Jengo, Fredrick Lutindi ambaye ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Jumuiya ya Wafanyabiashara wa Kariakoo amesema “wakati Mheshimwa Rais anaongea kuna takwimu alizitaja mimi na wafanyabiashara wengi tulishtuka kidogo kwamba jengo lile lililodondoka lilikuwa limebeba tani 850 sasa tani mia nane kwa kawaida Kariakoo hatuna jengo lenye uwezo wa kubeba tani hizo”

Wafanyabiashara hao wamemuomba Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Yusuph Mwenda kusaidia kufuatilia ili Rais apewe taarifa zilizo sahihi hasa hizo za kiwango cha mizigo kilichobebwa kwenye jengo lililoanguka.

 
Kuna investigation zengine hatuwezi sema tupo ofisini.Mfano kama ajali za ndege,magorofa,majanga ya dunia na teknolojia.
Yani dokta silahaa kaongea tu lakini alivyo fatwa utazani jambazi.
Acha hiyo juzi TRA kariakoo jengo linaungua kuna watu sijui akili zikoje gari wanavunja kioo cha mbele kisa funguo.
Yani hata mwizi wa vipuri kawazidi akili.
 
Kwa msongamano huo wa bidhaa, hata wangesema tani 1000 bado ingeweza kuwa sawa!
Screenshot_20250204_153948_Google.jpg
 
Tatizo sio gorofa mantiki inakosekana maana gorofa ina floor tatu pekeake!
Ndo maana wafanya biashara wamepinga maana wao ndo wana uzoefu na kwa mtu yeyote anayejua tani hawezi kukubali huo ujinga!
Mimi pia mfanyabiashara nimewahi weka container 8 nusu floor, ghorofa 3 yenye basement inaingia zaidi ya container 40 hasa kwa viwanja vya kkoo ambavyo ni vikubwa.
 
Kariakoo nina uzoefu napo sana tuu,tani 850 maana yake uwe na gunia 8500 za korosho!!!
Maana yake ghorofa moja inakuwa na mzigo wa kutosha gari 30 zinazobeba tani 30 kila moja!!!
Hahaaa.....Wadanganyeji Wadanganyika ambao hata wao sasa wamechoka kudanganywa na CCM.
Hivi unajua mizigo inayowekwa huko!?..store moja tu kwenye ghorofa kumi mchina ana mzigo wa tani 10,tshet,sendo sijui vitu gani
 
Kukaa kimya sio solution, tani hata 2000 zinaweza kuingizwa kwenye hilo jengo...inategemea na uzito wa mizigo sio ujazo.
Yani umejiunga JF kitambo sana nikiwa mdogo, ila bado huna uwezo wa kukadiria mzigo wa tani 2000 unaweza fit wapi.

Lile jengo chakavu nilifika halina hata uwezo wa kubeba tani 850, hata majengo mapya yanayojengwa mitaa ya Masasi bado hayawezi jaza tani 1000 sembuse elfu mbili.
 
Back
Top Bottom