Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,883
- 6,884
SHEREHE ZA MIAKA 35 YA CCM IRINGA NI MKOSI MTUPU,
WAFANYABIASHARA WAMKIMBIA PINDA
SHEREHE za miaka 35 ya kuzaliwa kwa chama cha mapinduzi (CCM) mkoa wa Iringa ni mkosi mtupu ni baada ya wabunge waliokuwemo katika msafara wa waziri mkuu Mizengo Pinda magari yao kugongana eneo la Kinyanambo Mafinga pamoja na baadhi ya wafanyabiashara katika Manispaa ya Iringa kukwepa kukabidhiwa vyeti vya pongezi na waziri mkuu Mizengo Pinda katika sherehe fupi ya iliyoandaliwa na CCM wilaya ya Iringa mjini kwa lengo la kuwakabidhi vyeti hivyo kutokana na misaada yao mbali mbali ambayo wamekuwa wakijitolea kwa ajili ya kusaidia kufanikisha shughuli za chama mjini Iringa.
Hatua ya wafanyabiashara hao kususia sherehe hiyo jana ambayo awali ilipangwa kufanyika Ikulu ndogo ya mkoa wa Iringa na kubadilishwa ghafla kwenda kufanyika katika viwanja vya ndege Nduli ilijitokeza muda mufupi baada ya uongozi wa CCM wilaya ya Iringa mjini kubadili ratiba na kuwataka wafanyabiashara waliokuwa wamekusanyika eneo hilo kuendesha magari yao kwenda uwanja wa ndege Nduli suala ambalo lilionekana kuwa gumu kutekelezwa kwa baadhi ya wafanyabiashara hao.
Mmoja kati ya wafanyabiashara hao ambaye hakupenda jina lake kutajwa ktk mtandao alisema kuwa uamuzi huo wa CCM kuwaandalia sherehe ya kukabidhiwa vyeti vya pongezi ulikuwa mzuri kwa maana ya kuthamini mchango wao kwa chama ila hawakupendezwa na hatua ya chama kuwakalisha kwa muda mrefu katika viwanja vya Ikulu na baadae kuwataka kwenda uwanja wa ndege nduli.
"Tulichokiona hapa ni kama kupotezeana muda zaidi kwani haiwezekani CCM wilaya ya Iringa mjini ikafanya sherehe hizo bila kuwasiliana na uongozi wa mkoa na kupanga ratiba ya pamoja......kweli zaidi ya wafanyabiashara 30 hawakuweza kufika kupokea vyeti hivyo vya pongezi "
Hata hivyo alisema kuwa iwapo CCM itaendelea na ubabaishaji huo katika shughuli zake upo uwezekano mkubwa wa baadhi ya wadau wa chama ambao wamekuwa mbele kujitolea kwa ajili ya kazi za chama kuvunjika moyo kufanya hivyo.
Msafara wa Picha wapata ajalli, Magari ya Wabunge yagongana.
Wakati huo huo Magari ya wabunge wa CCM waliopo katika msafara wa waziri mkuu Mizengo Pinda yaligongana mjini Mafinga eneo la Kinyanambo ,wakati msafara huu ukielekea Iringa ukitoka katika Sherehe za miaka 35 ya CCM zilizofanyika kimkoa kijiji cha Ifwagi kata ya Ifwagi wilaya ya Mufindi .
Wabunge walionusurika ni Ritta Kabati ,Lediana Mng,ong,o wote wa viti maalum mkoa wa Iringa ,mwenyekiti wa wabunge wa CCM mkoa wa Iringa na mbunge wa jimbo la Kalenga Dr wiliam Mgimwa na mbunge wa jimbo la Mufindi kusini Mendrady Kigolla pamoja na waandishi wahabari wa Chanel Tena Daud Mwangosi na mwandishi wa habari hizi Francis Godwin ambao wote wamenusurika kifo hakuna aliyejeruhiwa wala kupoteza maisha katika ajali hiyo iliyotokea sasa saa 10 .00 jioni .
Chanzo cha ajali hiyo ni mmoja kati ya magari yaliyokuwemo katika msafara huo kusimama gafla katika eneo hilo lenye mteremko mkali huku upande wa kulia kukiwa na msululu mrefu wa mabasi ya abiria ,malori na magari madogo ambayo yalikuwa yamezuiliwa ili kupisha msafara huo wa waziri mkuu.
Katika ajali hiyo gari la mbunge Mng'ong'o lenye namba za usajili T 758 APJ Toyota Land Cruse lililigonga kwa nyuma gari la mbunge wa jimbo la Kalenga lenye namba za usajili T 162 AHN Nisani gari ambalo wabunge wawili mbunge Kabati na Kigolla pia walikuwemo.
Awali msafara huo wa waziri mkuu wakati ukielekea mjini Mafinga gari la katibu wa CCM mkoa wa Iringa ambalo pia lilibeba waandishi wa habari ,viongozi wa jumuiya za CCM mkoa ,katibu mwenezi wa CCM mkoa na mbunge wa jimbo la Njombe Kaskazini ambaye ni mwenyekiti wa CCM mkoa Deo Sanga liliangusha begi la mbunge huyo eneo la Ihemi ,begi ambalo lilikuwa limewekwa juu ya kelia ya gari hilo bila kufungwa .