Wafahamu wakala wa usalama na afya mahala pa kazi (OSHA) - Tanzania

clion dismas

Senior Member
Aug 6, 2017
185
170
Wanabodi
Naomba niwaletee kwenu hawa wataalam kwenu, dondoo juu ya wakifanyacho na umuhimu wao kwa wale wote wanaofanya kazi, karibuni.

OSHA, kwa kirefu ni Occupational Safety and Health Authority. Ni taasisi ya kujitegemea, iliyoko chini ya ofisi ya waziri mkuu, sera,bunge,kazi,ajira,vijana na walemavu.

download.png
images.jpeg


Taasisi hii iliundwa chini ya sheria ya wakala wa serikali Na.30 ya mwaka 1997 ambayo majukumu yake yamechanganuliwa katika sheria ya usalama na afya mahala pa kazi Na.5 ya mwaka 2003.

Rasmi ilianzishwa tangu tarehe 31/08/2001 chini ya shwria ya wakala Na.30 ya 1997 kwa minajili ya :-

1. Kuboresha hali ya usalama na afya mahala pa kazi, ikijumuisha;

2.Kufanya kaguzi za afya na usalama;

3. Kufanya chunguzi za afya kwa wafanyakazi mahala pa kazi;

4. Kufanya mapiyio ya tathmini za athari za kiafya na kiusalama mahala pa kazi;

5. Kutoa leseni baada ya kukidhi matakwa ya sheria ya afya na usalama mahala pa kazi;

6. Kusajili mahala pote pa kazi na kuwasaidia kupata lesini na kufikia viwango vya kukidhi kupata leseni ya ubora;

7. Kuhakiki ramani na michoro yote ya majengo sehemu za kazi kabla ya ujenzi kufanyika;( kwa mujibu ya sheria Na.5, ibara ya 16 ibara ndogo ya 1 ya mwaka 2003, " mtu yeyote anapaswa kusajili kiwanda/eneo la kufanyia kazi kabla ya kuanza kufanya kazi hapo".;

8. Kutoa ushauri wa kitaalam kuhusiana na maswala ya afya kazini pamoja na kutia elimu juu ya umuhimu wa usalama mahala pa kazi.

Jambo jema ni hili, usajili wa eneo la kazi ni bure kabisa, hakuna tozo yoyote ile. Punde unaposajili eneo lako la kazi utapewa cheti cha osha.(mfano wa cheti ni hiki hapa)
download.jpeg


Aidha, OSHA inatoa huduma ya kozi mbalimbali ambazo ni lazima kwa mujibu wa sheria Na.5 ya 2003 ili kurahisisha usalama mahala pa kazi kwa wafanyakazi kama vile:-
1. Huduma ya kwanza na kamati za afya na usalama mahala pa kazi(Industrial first aid, safety and health representative respectively). Mafunzo mengine kwa ajili ya afya na usalama uhusisha;

2. OHS Risk assesment
3. OHS in construction industry
4. Accident investigation
5. Workplace exposure assesment strategy
6. Safe use of chemicals at work place and
7. Working at height.

Haya yote yanafanyika ili mfanyakazi mahala pa kazi awe katika usalama na ajali au hatari yoyote ambayo kwa namna moja au nyingine inaweza kuzuiliwa au kupunguza madhara pale itakapotokea.

Kaguzi zinazofanya na wataalamu wa osha ni pamoja na:-
1. General safety inspection
2. Electrical inspection
3. Plant inspection
4. Medical inspection
5. Industrial hygiene
6. Ergonomics inspection

Kila kaguzi tajwa juu hapo ina gharama zake.

Zaidi ifahamike kwamba OSHA inafanya kazi karibu sana na shirika la kazi la kimataifa (ILO).

KUMBUKA

NI HARAMU KUFANYA KAZI BILA KUISAJILI KAZI KWA MUJIBU WA SHERIA NA. 5 YA MWAKA 2003, IBARA YA 16 IBARA NDOGO YA KWANZA.
20190604_144151.jpg


Ofisi za osha zimejengwa katika kanda tofauti tanzania, zikihusisha:-

1.Kanda ya ziwa
2.Kanda ya pwani
3.Kanda ya kaskazini
4.Kanda ya kati
5.Kanda ya ndanda ya juu kusini
6. Kanda ya kusini
( zaidi tembelea, www.osha.go.tz)

SAJILI LEO ENEO LAKO LA KAZI KUEPUKA USUMBUFU BAADAYE UKIBAINIKA ULIKWEPA KIUJANJA. WENYE VITAMBULISHO KWA UMACHINGA HAWAJISAJILI NA OSHA, YAANI, MWENYE MTAJI CHINI YA MILIONI 4 KWA MWAKA.


"USALAMA NA AFYA NA MSTAKABALI WA KAZI KUELEKEA UCHUMI WA VIWANDA".

Barikiwa
 
Asante! Naomba msaada ktk haya:
1. Ni hatua gani nifuate ili niweze kufanya registration ya sehemu yangu ya kazi?
2. Ni gharama gani zilizoondolewa na serikali upande wa OSHA hivi karibuni?
Week chache zilizopita nilimsikia Mh. rais wa JMT akiagiza kuwa gharama fulani zilizokuwa zikitozwa na OSHA ziondolewe. Naomba kujuzwa.
 
Asante! Naomba msaada ktk haya:
1. Ni hatua gani nifuate ili niweze kufanya registration ya sehemu yangu ya kazi?
2. Ni gharama gani zilizoondolewa na serikali upande wa OSHA hivi karibuni?
Week chache zilizopita nilimsikia Mh. rais wa JMT akiagiza kuwa gharama fulani zilizokuwa zikitozwa na OSHA ziondolewe. Naomba kujuzwa.

Kulikua na gharama nyingi , mfano consultation fee uliyokua ukilipa kwa lisaa, ilikua ikirange 100K plus, kulikua na gharama ya usajili, 100K plus kulikua na gharama nyingi kwakweli kama vile:-

1. OHS Consultancy and expert services shall be charged TShs. 450,000 per expert per day. Reimbursable expenses, travelling and
accommodation expenses shall be charged as per the actual expenses incurred.


2. Scrutiny of workplace drawings/ plans shall be charge Tsh.300, 000 per hour per drawing.

3. Application fee for private service provider 100,000/=

4. Duplicate certificate 50,000/=

5. Safety material per piece 15,000/=

etc
Rejea tozo zote za osha kwenye huu muongozo na ambazo nimeziainisha hapo juu.
 

Attachments

  • Osha fee.pdf
    66.3 KB · Views: 63
Vizuri...

Ila unaelezea OSHA lakini picha naona ya WCF... hizo ni taasisi mbili tofauti...


Cc: mahondaw

Malengo ya kuweka picha iyo nilimlenga waziri aliyeko kwenye kimbweta hapo na sikulenga maneno hayo.

By the way, WCF( WORKERS COMPENSATION FUND) PAMOJA NA OSHA ZOTE NI TAASISI MBILI ZILIZO CHINI YA WAZIRI HUYO MMOJA.
 
Hawa osha wanakula hela ya Burr tu, sijaona kazi yao! Ni saws na maafisa kilimo, nyuki na misitu ambao wako mijini. Ebu nuambie majiji na manispaa mali2 utawakuta. Nimesahau maafisa umwagiliaji! Nashauri mamlaka husika walifanyie kazi hill.
 
Osha na fire kwenyw suala la Moto mnatofauti gani?
Mbona mnaingiliana majukumu?
Fire nao wanakagua umeme, mipangilio ya mitambo na ishu z8bgine za usalama.

Osha kuna ishu za kure-new cheti, hii ina maana gani?

Hizo pesa mnazochukua, mnatoa huduma gani nje ya kukagua?

Ofisi ya waziri mkuu ilikuwa ina pambana na miingiliano ya taasisi lakini kwenye taasisi zake alikuwa hagusi
 
Kulikua na gharama nyingi , mfano consultation fee uliyokua ukilipa kwa lisaa, ilikua ikirange 100K plus, kulikua na gharama ya usajili, 100K plus kulikua na gharama nyingi kwakweli kama vile:-

FEES FOR OTHER SERVICES
Description Fees in TShs

1. Application fee for private service provider 100,000

2. Duplicate certificate 50,000

3. Workplace general register 50,000

4. Safety sign materialper piece 15,000

5. Abstract 50,000

Zaidi, kama 500K zimeondolewa. Kuomba kufanyiwa usajili ni bure na baada ya usajili ndipo kuna gharama elekezi za ukaguzi ambazo unaweza ziangalia kwenye tovuti yao.
Great!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Osha na fire kwenyw suala la Moto mnatofauti gani?
Mbona mnaingiliana majukumu?
Fire nao wanakagua umeme, mipangilio ya mitambo na ishu z8bgine za usalama.

Osha kuna ishu za kure-new cheti, hii ina maana gani?

Hizo pesa mnazochukua, mnatoa huduma gani nje ya kukagua?

Ofisi ya waziri mkuu ilikuwa ina pambana na miingiliano ya taasisi lakini kwenye taasisi zake alikuwa hagusi


Kimsingi osha haihusiki kabisa na mambo ya fire ni miaka mingi sasa tangu fire ilipopewa mamlaka kamili na mitungi yao ya moto. Osha inachokifanya ni kuhakikisha ajali haitokei mahala pa kazi muda wote lakini endapo ikitokea, basi miundombinu ya kupambana na dhahama ya moto iwepo eneo lake.

Zaidi ya yote, kabla ya fire kuwa na mamlaka kamili juu ya hili, osha isingrlikukuta na fire extinguisher au iwe ime expire ilikua inakupiga fine, now days utakua enforced bila ya fine, ukishindwa ku abide with liberty ya safety utashurutishwa.
 
Nataka kujua Ni wapi nitapata course ya rigger ,muongoza operator wa crean na gharama zake na masharti ya kujiunga...Nia na madhumuni nipate certificateView attachment 1325125

Sent using Jamii Forums mobile app

Kimsingi osha sio taasisi ya elimu ila ni mamlaka ya usalama na afya maala pa kazi. Pale utakapotembelea eidha veta au vyuo ya ufundi watakupa mwongozo wa kozi kama iyo unayotaka kuisomea ili uwe professional.

Osha ikifanyacho ni kwamba, baada ya wewe kuwa na iyo elimu unayotaka kuisoma, itaku-train namna ya kufanya operation ya mtambo au kifaa chako cha moto free from accident.
 
Back
Top Bottom