stunna
JF-Expert Member
- Nov 7, 2013
- 258
- 146
- Thread starter
- #121
So kwa mada yako ya wachawi unaonyesha wazi unataka tuwe malokole sio? Kwani ulokole ndio njia pekee ya kupambana na uchawi? Na maombi ya usiku wanafanya walokole tuu waislam awafanyi? Achana na izo mambo wewe mwenyewe mchawi tuu ulijuaje siri za uchawi ikiwa vitabu vyote vya mungu amna ata kitabu kimoja kinachosema kuwa njia inayopita mchawi akiwa anapaa ndio njia anayorudia au kuna kitabu gani cha mungu kinasema kuna wachawi wanaotembea na fagio kijiko au ungo? Mrudie mungu wako wewe achana na izo habari mchawi mkubwa wee
Mkuu mimi nimeokoka kitambo tu na nina roho mtakatifu,lakini pia nataka kushare na wewe hii kitu kwamba mtu akiokoka maana yake amekuwa kiumbe kipya na kabla hajaokoka alikuwa mtenda dhambi ndo maana wapo wengi leo hii unawaona walikuwa wachawi,waganga,wazinzi,walevi,n.k lakini waliamua kumpa yesu maisha yao kwhyo hao pia wanakuwa na ushuhuda mwngi wa maisha yao ya nyuma kwhyo hata hicho nlichokiandika najua namaanisha nn so ukiamua kukiamini au usipoamini hiyo ni juu yako maana hakuna sehemu niliyosema nataka watu wawe walokole au nimejaribu kucompare na kitabu chochote cha dini lakini pia nashkuru kwa kuniita mchawi maana biblia imesema atambariki atakayekubariki na atamlaani atakayekulaani ,kwahyo mkuu nakuombea Mungu aimulike neema yake kwako ili injili ya wokovu ikuzukie maana shetani amewaseta wale wote ambao ni wafuasi wake (ambao hawajaokoka) katika gereza lake na amewapofusha fikra ili injili ya yesu kristo isiwazukie.