Wafahamu Mawaziri na Manaibu ‘waliotemwa’ na Rais Magufuli katika Baraza jipya la Mawaziri

Baada ya Rais Magufuli kuteua Baraza jipya la Mawaziri atakalofanya nalo kazi baada ya kuwa Rais katika muhula wa pili. Katika Baraza hilo jipya, Rais amewatema Mawaziri 7 na kuchagua wengine

Waliotemwa ni;

1. Aliyekuwa Waziri wa Maji, Prof. Makame Mbarawa


2. Aliyekuwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina

3. Aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Hamis Kigwangalla

4. Aliyekuwa Waziri wa Uchukuzi na Ujenzi, Isaac Kamwelwe

5. Aliyekuwa Waziri wa Kilimo, Josephat Hasunga

6. Aliyekuwa Waziri wa Muungano na Mazingira, Mussa Azzan Zungu


Manaibu Waziri walioachwa kwenye Baraza Jipya la Mawaziri ni;

1. Aliyekuwa Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Juliana Shonza

2. Aliyekuwa Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana na Ajira, Anthony Mavunde

3. Aliyekuwa Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhandisi Stellah Manyanya

4. Aliyekuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Masauni

5. Aliyekuwa Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo

6. Aliyekuwa Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu

7. Aliyekuwa Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Atashanta Nditiye

8. Aliyekuwa Naibu Waziri wa Muungano na Mazingira, Mussa Sima

9. Aliyekuwa Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshugulikia masuala ya Watu wenye Ulemavu, Stella Ikupa

10. Aliyekuwa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Costantine Kanyasu

11. Aliyekuwa Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji

12. Aliyekuwa Naibu Waziri wa TAMISEMI, Sinkamba Kandege
Ni jambo jema kwa mheshimiwa rais kutokumtua Juliana Shonza maana muda wote alikuwa anamuwaza Mbowe tu na kufungua wasanii badala ya kuwaza namna gani ya kuwahudumia watanzania
 
Mizengo pinda amerudi tena kufanyaje?
Au ni mwanake?

Afu lukuvi hiyo wizara mbona mnampendeleaga sana?

Sijaipenda hiyo.
 
Nini hatma ya bashite ndo kusema rashid amechukua nafasi yake ya kamati ya fundi. Mbona kasaulika?
 
Ahsantee mpenzi kwa kumuelewesha.!a
Kuna watu naanza kuwaona vile wanaanza kuingiza mambo ya dini kwenye uteuzi huu na watu wanasadiki kuandika Uzi eti anauliza viongozi wa dini(Ya kiislam) kwanini wapo kimya juu ya ubaguzi (wanavyoita wao). Ni changamoto sana Mkuu
Wanaonufaika siku zote hawajali maumivu ya wasionufaika, isipokuwa wachache waadilifu sana. Hebu geuza picha na iwe rais Mwislamu amechagua baraza hili la Mawaziri 20 Waislamu na Wakristo 3 ! Naapa ungetoa sermon Parokia wewe…..!!!
 
Wanaonufaika siku zote hawajali maumivu ya wasionufaika, isipokuwa wachache waadilifu sana. Hebu geuza picha na iwe rais Mwislamu amechagua baraza hili la Mawaziri 20 Waislamu na Wakristo 3 ! Naapa ungetoa sermon Parokia wewe…..!!!
Mi binafsi sioni ubaya wowote kusema kweli.! Zaidi nitaombea amani na upendo basi mambo ya dini kwangu hayana uzito wowote. Hata viongozi nachaguaga kwa uchapakazi wao na sio vinginevyo . Pole mkuu naona umeumizwa sana na maumivu ya mkuu
 
Mi binafsi sioni ubaya wowote kusema kweli.! Zaidi nitaombea amani na upendo basi mambo ya dini kwangu hayana uzito wowote. Hata viongozi nachaguaga kwa uchapakazi wao na sio vinginevyo . Pole mkuu naona umeumizwa sana na maumivu ya mkuu
Yawezekana wewe binafsi usiwe na inhi, lakini si Watanzania wote wako hivyo. Ndiyo maana kiongozi mwenye hekima na busara lazima afanye uwiano, hata wa kubabaisha- 23-9 hivi! Imani za kidini ni sehemu ya utu wetu. Mkristo atajihisi "easy and relaxed' anapoona anashughulikiwa ofisini na Mkristo mwenzake, na halkadhalika Mwislamu; hata kama wote wawili ni waadilifu! Sasa fikiria katika nchi zetu za Kiafrika ambapo uadilifu kama huo haupo kwa 80%, Mwislamu ana chance gani katika 'full enjoyment of service delivery' katika Baaraza la Mawaziri kama hili? Na Kama alivyochagua MKULU huko juu ndivyo itakavyokuwa' replicated' kwa walio chini…. Haiwezekani hata kidogo katika hali hii ukaona Wizara moja ina watumishi Waislamu walio wengi (of course, labda wapiga deki, waaandaaji chai) ....aidha kwa sababu za kibaguzi au kwa sababu tu Waziri anakuwa 'comfortable' na watu aliowazoea na anaowajua. Hili suala msilifanye la kipuuzi na kwamba kila anayeliibua ni 'mdini'. Ila Wakristo walipoliibua hili wakati wa Mwinyi, Kikwete………..ni Wazalendo!
 
Back
Top Bottom