kibogo
JF-Expert Member
- Apr 1, 2012
- 9,739
- 4,732
Huyu ni Amina kisangi
Huyu ni miongoni mwa wabunge waliochangia hoja ya ESCROW alhamisi jioni. Kwanza alijisahau kama pale alikuwa bungeni na kuishia kutoa mipasho inayoonyesha dhahiri kuwa alikuwa amelewa pombe!
Hata pale alipopewa taarifa na Deo Filikunjombe alisema haipokei na kuishia kusema eti Deo na wenzake wa PAC wachunguzwe kama wanafaa kuwepo CCM na kuwa kamati ya PAC ni UKAWA.
Baadhi ya maneno yake namnukuu "Mheshimiwa mwenyekiti, hawa watu wa PAC wachunguzwe kama ni wana CCM kweli.Hii ripoti ya PAC inaonyesha kuwa PAC ni UKAWA. Hizo pesa za ESCROW ni za IPTL wakila au wakigawa nyie inawauma nini?"
Huyu ni ASUMPTA Mshana ni kati ya wabunge waliongoza kwa kuongea mambo ya siyo ya msingi ndani wakati wa mjadala wa EScrow yeye bila aibu alisimama na kuwatetea wezi wa Escrow lakini cha kusikitisha jimbo analoongoza la NKENGE huko mkoani kagera ni jimbo ambalo linakabiliwa na umasikini mkubwa sana tena wa kutisha lakini yeye bila mshipa wa aibu anasimama na kuwatetea watumiwa waliyochota mabilion ya fedha.wabunge kama hawa ni mizingo mitupu isiyokuwa na faida kwa wananchi !!!! wakati wananchi wake wanakunywa maji machafu huko jimboni kwake yeye yupo bungeni anatetea wezi kwa nguvu zote
Anaitwa Mhe Simbachawene huyu mbunge alikuwa anawtetea watuhumia kwa kutumia akili sana na wakati mwingine kujenga hoja ili watuhumiwa waweze kupenya mfano alikuwa yupo mstari mbele kupendekeza maazimio dhaifu ambayo yasinge toa adhabu kali kwa watuhumiwa hao wa ESCROW ,Tunaweza kusema kuwa ametumia fani yake ya sheria kutetea wezi wakati wa mjadala wa Escrow ndani ya bunge
Huyu anaitwa Lusinde ni kati ya wabunge waliongoza kwa kuongea mambo yasiyokuwa na maana ndani ya bunge kwa kiswahili kizuri aliongoza kwa kuongea pumba zaidi bila kujali kuwa kulikuwa na watu wengi wanamtazama siku hiyo!!!! huyu LUSINDE kwa upande fulani alitetea watuhumiwa wa ESCROW kwa kupitia hoja dhaifu sana bila kuweka uzalendo mbele
Huyu anaitwa Richad Ndasa wakati wananchi wake wanakabiliwa na umasikni mkubwa kutokana na ufisadi unaofanywa na baadhi ya viongozi yeye bila mshipa wa aibu anasimama na kuwatetea mafisadi bungeni!!!!!
ndugu wasomaji wabunge kama hawa tusiwe tunawapa nafasi ya kwendaa bungeni kwasababu hawana faida yoyote kwa wananchi maana ya kazi ya mbunge ni kutetea wananchi na siyo kutetea viongozi wezi kama wanavyofanywa hakika wametia aibu sana na wamesaliti wananchi wao ambao ndiyo masikini zaidi