Wadau naomba wazo la biashara, nina mtaji wa 10M-15M

Habari wanajukwaa.

Lengo la kuleta uzi huu ni kuomba wazo la biashara ambayo ninaweza kufanya kwa DSM au kwingine, ila pia iweze kuajiri watu wanaonitegemea, kama 4 hivi kwa kuwa maswala ya ajira yamekuwa pia ngumu. Kama nilivyosema mtaji kwa sasa ninayo 10-15milion, lakini pia biashara kama itaanza vizuri naweza kukopa kuongezea mtaji.

Ningependelea biashara ambayo inaweza kuwa na mzunguko wa haraka lakini pia kwa usimamizi sioni tatizo kwa kuwa tayari ninao watu. Nimefikiria muda mrefu kidg sijapata wazo zuri na productive.

Kama kuna sehemu naweza kupata hata maelekezo ya namana kuanzisha biashara kwa vitendo naweza kwenda.

Naombeni msaada jamani kweli hili nipo serious siyo utani. Samahani pia pengine wazo langu sijaliweka vizuri kwa kuwa mie si mwandishi mzuri pia.

Natanguliza shukrani!
Njoo tukae baa hapa tupate akili ya biashara
 
Hizo pesa umezipata katika mazingira gan
Kamali
Biko
Kubet au
Mikopo kwenye taasis za fedha
Ukifungua biashara mwanzoni kama huna kazi ni vizur ukasimamia mwenywe usimuamini MTU lengo la kufany hivyo ni kujua loss and profits and how to control the business
Kama umechukua mkopo na hauna MTU wa kukufanyia close supervission weka pesa yako kwa fixed account mpaka utakpo pata MTU mwelewa mtakae gawana nae faida
Biashara aichukulie kama yake
 
!
!
Hao wategemezi usiwape Samaki, wafundishe kuvua. Wajengee uwezo wa kutafuta wenyewe.
Kwa Milioni kumi, nunua pikipiki 4 zikatie Bima comprehensive kaa kijijini zikodishe. Kwa siku kila moja ikileta angalau 5,000 ni mauzo ya 20,000 kwa siku. Jilipe 5,000 fanya matumizi ya 5,000 utaingiza 300,000 kwa mwezi. Komaa
 
!
!
Hao wategemezi usiwape Samaki, wafundishe kuvua. Wajengee uwezo wa kutafuta wenyewe.
Kwa Milioni kumi, nunua pikipiki 4 zikatie Bima comprehensive kaa kijijini zikodishe. Kwa siku kila moja ikileta angalau 5,000 ni mauzo ya 20,000 kwa siku. Jilipe 5,000 fanya matumizi ya 5,000 utaingiza 300,000 kwa mwezi. Komaa

asante kwa mawazo
 
Mkuu, fungua biashara ya mgahawa wa chakula, uwe msafi na chakula kizuri, customer care iwe mzuri. Jina ulite Dr.Shika best food, Dr. Shika uramchangia 30 kila mwezi za kutumia jina lake. Ukitoka unikumbuke kwenye mafanikio yako
Ahaha anaweza pia akamuomba aende kwenye Restaurant kuzungumza na wateja
Sahani iwe Tsh.900
 
Chukua milioni kumi tu, nunua dagaa wa mwanza na bukoba walete dar, nakuhakikishia kwa mwezi utakuwa na faida si chini ya milion 5 na hao wadogo zako wataneemeka sana, siwez andika maelezo mengi unafanyaje, ni pm nkupe A to Z ila na mie itabid unikope mil 2 nizungushe ndani ya miez miwili
 
Chukua milioni kumi tu, nunua dagaa wa mwanza na bukoba walete dar, nakuhakikishia kwa mwezi utakuwa na faida si chini ya milion 5 na hao wadogo zako wataneemeka sana, siwez andika maelezo mengi unafanyaje, ni pm nkupe A to Z ila na mie itabid unikope mil 2 nizungushe ndani ya miez miwili

Mhh mil 5... hivi hizi details mnazoleta hapa za kweli jamani au story tu.
 
Mkuu, fungua biashara ya mgahawa wa chakula, uwe msafi na chakula kizuri, customer care iwe mzuri. Jina ulite Dr.Shika best food, Dr. Shika uramchangia 30 kila mwezi za kutumia jina lake. Ukitoka unikumbuke kwenye mafanikio yako
I love the idea
 
Fungua kiwanda cha kuzalisha mayai,nunua vifaranga wako wa kuku wa mayai "layers" kifaranga kimoja 2400/2500 haizidi hapo mtafute mtaalam asimamie haokuku hadi watakapo anzakutaga na ww utakua ushejua kila kitu kwenye ufugaji kwahuo mtaji wako utapiga bao.
 
Alaf kitu kingine wadau ivi hadi mtu unashika mil 15 hujui kweli ni biashara gani ufanye? Kwamba hujawahi kifanya biashara au?ulizipataje ela zote kwa mkupuo.na kama ulifanya biashara ukapata izo mil 15 hukupata changamoto yyte katika biashara adi ujue ni biashara gani unatakiwa uiendelezee kwa ela utayoipata..kama ulikua umeajiliwa kwa adi mtu kufikisha izo mil 15 bado swali kubwa sana bila kujaribu ata vibusiness vidogo...mtu mwenye mil 15 mkononi akiniomba wazo la biashara bado nna maswali mengi sana ya kumuuliza..unaweza kukuta jamaa anatupasua vichwa tu apa..
Mkuu kuna kitu umekosea kidogo, ata matajiri kama bakhresa na Mengi huwa wanaomba ishauri na kushauriwa na wataalum, umahiri wao ni selection of best alternative decision.
 
Mkuu kuna kitu umekosea kidogo, ata matajiri kama bakhresa na Mengi huwa wanaomba ishauri na kushauriwa na wataalum, umahiri wao ni selection of best alternative decision.
Me nnavyoamini utafanikiwa kufanya kitu kwa mapenzi na kama una idea nacho.ata kama kakilipi kitalipa baadae..ila kitu kama kinalipa umeambiwa tu kinalipa na huna idea nacho na interest nacho pia..utafanya kwa mda mfupi na utaquit kwenye changamoto ndogo sana..hao wakina bakresa sio kama ni wenyewe wanafanya kwa mapenzi..walishafanya kwa mapenzi enzi wanaanza.hizi products mpya zinakuwa managed na management yenye ujuzi mkubwa sana ndio maana they keep on moving..

Lets say kwa sasaivi busn inayolipa ni duka la spear za magari...hajui masoko yake anataftaje,hajui product gani inatakiwa na kwa bei gani ili kukompete.hajui filters zinaingilianaje ktk gari as a substitute example ukikosa filter ya nissan navara utafunga filter ya gari ipi kama mbadala..izo ni changamoto sana..

Cha msingi kama una mda take a train.ila ukifata ushauri tu na ukaanza pupa pupa kisa biashara hii inalipa utashangaa ata kodi itashindwa kujilipa..kumbuka kuna pango, serikali inataka chake,halmashauri,na ww upate faida ya kujikimu kama sio ujiendeleze.maana nia ya busn ni maendeleo..

Achukue ideas kama chachu na sio kila idea unayoambiwa inalipa ndio ya kufata maana oportunities zingine ni mitego ya kukuangusha..

Nawasilisha mkuu.
 
Me nnavyoamini utafanikiwa kufanya kitu kwa mapenzi na kama una idea nacho.ata kama kakilipi kitalipa baadae..ila kitu kama kinalipa umeambiwa tu kinalipa na huna idea nacho na interest nacho pia..utafanya kwa mda mfupi na utaquit kwenye changamoto ndogo sana..hao wakina bakresa sio kama ni wenyewe wanafanya kwa mapenzi..walishafanya kwa mapenzi enzi wanaanza.hizi products mpya zinakuwa managed na management yenye ujuzi mkubwa sana ndio maana they keep on moving..

Lets say kwa sasaivi busn inayolipa ni duka la spear za magari...hajui masoko yake anataftaje,hajui product gani inatakiwa na kwa bei gani ili kukompete.hajui filters zinaingilianaje ktk gari as a substitute example ukikosa filter ya nissan navara utafunga filter ya gari ipi kama mbadala..izo ni changamoto sana..

Cha msingi kama una mda take a train.ila ukifata ushauri tu na ukaanza pupa pupa kisa biashara hii inalipa utashangaa ata kodi itashindwa kujilipa..kumbuka kuna pango, serikali inataka chake,halmashauri,na ww upate faida ya kujikimu kama sio ujiendeleze.maana nia ya busn ni maendeleo..

Achukue ideas kama chachu na sio kila idea unayoambiwa inalipa ndio ya kufata maana oportunities zingine ni mitego ya kukuangusha..

Nawasilisha mkuu.
Maelezo yako siyakatai ila elewa sio kila anayeomba ushauri hapa JF hana idea au hizo traits ulizozitaja ila wengine wana ongeza knowledge and information. Usishangae mtu kuomba ushauri wa biashara ya kufanya wengine wanafanya online intelligence in terms of product market, suitable locations, machinery and the like. Anyway tupo pamoja mkuu kwa maoni yako muhimu.
 
Maelezo yako siyakatai ila elewa sio kila anayeomba ushauri hapa JF hana idea au hizo traits ulizozitaja ila wengine wana ongeza knowledge and information. Usishangae mtu kuomba ushauri wa biashara ya kufanya wengine wanafanya online intelligence in terms of product market, suitable locations, machinery and the like. Anyway tupo pamoja mkuu kwa maoni yako muhimu.
Nimekuelewa mkuu upo vzuri..tupo pamoja.
 
Hizo nakupa eneo ujenge green house hapa tabata maji ya kisima uhakika faida tutapigiana asilimia chache I interested come pm
 
Maelezo yako siyakatai ila elewa sio kila anayeomba ushauri hapa JF hana idea au hizo traits ulizozitaja ila wengine wana ongeza knowledge and information. Usishangae mtu kuomba ushauri wa biashara ya kufanya wengine wanafanya online intelligence in terms of product market, suitable locations, machinery and the like. Anyway tupo pamoja mkuu kwa maoni yako muhimu.

Saute mkuu! ndo maana ya uwepo wa JF na wadau wake, shule tosha.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom