Boeing 757
JF-Expert Member
- May 18, 2020
- 288
- 612
Unajua katika ulimwengu wa leo kuna lifestyle za kila aina. Na pia kila mmoja hupendelea kufanya kile apendacho. Ila kuna hali fulani ninaiona kwenye jamii hususan inayonizunguka.
Ipo hivi; Kama wewe ni kijana labda tuseme kuanzia 20+yrs kama huzinyoi kwa style za kisasa au kutengeneza nywele zako kama kusokota dreads, nywele zako zipo kawaida tu kama zilivyo. Yaani unaonekana mtu wa ajabu sana.
Pia kama upo single hauna muda wa kukimbizana na sketi, sio mtu wa totoz lazima watakutolea kashfa, mara ni hanithi mara ni domo zege (japo yaweza kuwa inachangia). Wanakuona kama umepitwa na wakati na ni mshamba wa mwisho.
Na pia kwa mfano ukipita hata barabarani na kitabu hata cha story labda umekiazimisha mahali unapita nacho umekibeba mkononi lazima watakushangaa kinoma kana kwamba ni kitu cha ajabu sana.
Yapo mambo mengi sana kwenye jamii inayonizunguka nayaona hayapo sawa lakini hebu nisaidieni haya machache.
JE, JAMII YETU KUNA KITU GANI HAKIPO SAWA AU NI MHUSIKA MWENYEWE KWA HAYA MASWALA HAYUPO SAWA?
Ipo hivi; Kama wewe ni kijana labda tuseme kuanzia 20+yrs kama huzinyoi kwa style za kisasa au kutengeneza nywele zako kama kusokota dreads, nywele zako zipo kawaida tu kama zilivyo. Yaani unaonekana mtu wa ajabu sana.
Pia kama upo single hauna muda wa kukimbizana na sketi, sio mtu wa totoz lazima watakutolea kashfa, mara ni hanithi mara ni domo zege (japo yaweza kuwa inachangia). Wanakuona kama umepitwa na wakati na ni mshamba wa mwisho.
Na pia kwa mfano ukipita hata barabarani na kitabu hata cha story labda umekiazimisha mahali unapita nacho umekibeba mkononi lazima watakushangaa kinoma kana kwamba ni kitu cha ajabu sana.
Yapo mambo mengi sana kwenye jamii inayonizunguka nayaona hayapo sawa lakini hebu nisaidieni haya machache.
JE, JAMII YETU KUNA KITU GANI HAKIPO SAWA AU NI MHUSIKA MWENYEWE KWA HAYA MASWALA HAYUPO SAWA?