Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,991
Ati leo wanatishia kuandamana kwa sababu wataondolewa misamaha ya kodi! Leo wamecharuka na kugundua kuwa serikali inaweza kuwafanyizia wakiendelea kupiga kelele. Ati, kwa vile sasa misamaha ya kodi itafutwa kwa taasisi za kidini ukiondoa vitu vya ibada (Biblia, Qurani, tasbihi n.k) ndio wachungaji na mashehe wetu wamecharuka!
Niliwaandikia karibu mara mbili kuwa wamelala kitanda kimoja na watawala na wamefurahia mahaba ya ufisadi. Ni wao wamekuwa wakiwaalika kila kukicha kwenye tafrija zao na kwenye matembezi yao hawakosi. Sasa leo wameanza kupiga kelele dhidi ya ufisadi na dhidi ya uongozi wanatarajia watawala wacheze chioda?
Leo wachungaji na mashehe wanaanza kusimama na kunyoshea kidole ufisadi waziwazi wanatarajia kweli misamaha ya kodi iendelee?
Walichofanya watawala ni kuwabeep hawa! Kwamba wakiendelea na kelele zao dhidi ya viongozi na kunyoshea kidole watawala wajue serikali ina uwezo na ubavu wa kuwafanya walipe!
Sasa uchaguzi ni wao:
a. Wapige magoti kwa viongozi wa serikali na kuwaahidi kuwa wakirudishiwa misamaha ya kodi hawatapiga kelele dhidi ya viongozi (a.k.a kujihusisha na siasa)
b. Waamue kupandisha gharama za huduma zao za kijamii ili waanze kutengeneza faida kama taasisi nyingine za kibiashara na hivyo kuchangia kwenye pato la taifa. Baadhi ya huduma ambazo inabidi waongeze gharama ni pamoja na hospitali, kliniki, mashule na vyuo mbalimbali.
c. Wafunge baadhi ya huduma zao ambazo ni ngumu kujiendesha na kuziunganisha baadhi ya huduma zao kama wafanyavyavyo wafanyabiashara wengine na hivyo kupunguza gharama za uendeshaji.
d. Huduma zile za misaada (charity works) zisitishwe na kuacha serikali ifanye shughuli hizo kwa ufanisi vinginevyo wataweza vipi kutoa misaada ambayo wanaigharimia kama bidhaa nyingine. Nani ata offset gharama ya kuingiza, kutunza na kusambaza misaada hiyo. Of course, serikali ina uwezo huo! Sudan walijaribu!!
Upande mwingine ni kuwa serikali isilegeze uzi bali ing'ang'anie msimamo wake tuone hawa wachungaji na mashehe watafanya nini zaidi ya kupiga mikwara. Najua jambo moja msitarajie Pengo kuandamana mitaani!!! Hata kina Kilaini msifikirie wanaweza kusimama na mabango!
I know however, rafiki yangu Khalifa Khamisi wa Kwamtoro na wengine wanaweza kuonekana mitaani! Hawa kina Rev. Whoever hawana ujasiri wa kufanya hivyo!
===========================================
Habari Leo
Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Methodius Kilaini ameishauri serikali kupitia upya uamuzi wa kuyafutia msamaha mashirika ya dini na asasi za kiraia. Akizungumza jana na gazeti dada la Daily News, alisema taasisi hizo hazitengenezi faida na badala yake, zipo kwa ajili ya kuwainua watu wa kawaida ambao ni masikini. Alitoa mfano wa huduma za afya zinazotolewa hususan maeneo ya vijijini, ambazo nyingi hutolewa na taasisi za dini.
"Serikali ilipaswa kukaa na wadau kwa ajili kupata ushauri juu ya hasara na faida ya kuondoa msamaha huo kabla ya kutangaza bajeti yake," alisema Kilaini. Wakati huo huo, Naibu Katibu Mkuu (masuala ya dini) wa Baraza Kuu la Waislamu wa Tanzania (BAKWATA), Mohamed Khamis alisema uamuzi huo unakwamisha sera ya Taifa ya kuwapa maisha bora wananchi.
Alisema taasisi za dini hazitengenezi faida na nyingi zinategemea wafadhili. Alisema inapaswa itoe ruzuku kwa taasisi hizo, ili kuziwezesha kuendesha shughuli zake za kila siku. Kwa upande wake, Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Dodoma, Dk peter Mwamasika, alisema maaskofu wako tayari kuandamana kupinga hatua ya serikali ya kuziondolea taasisi za dini misamaha ya kodi.
Akizungumza jana Dodoma, Askofu Mwamasika alisema hatua hiyo ya Serikali ni ya hatari na inaweza kuleta mtafaruku usio na sababu za msingi na kuendelea kuwapa ugumu wa maisha wananchi wanaopata huduma kupitia shule na hospitali zinazomilikiwa na mashirika hayo ya kidini.
Aliishangaa Serikali ya CCM inavyoanza kubadilisha mwelekeo wa utawala wake ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakishirikiana nayo kuhudumia Watanzania. Aliongeza kuwa KKKT ikiwa sehemu jumuiya ya Kikristo Tanzania, inatambua wajibu wake wa kuhudumia mtu mzima yenye maana ya kiroho na kimwili na ndiyo maana inahudumia kwenye elimu, afya, vituo vya watoto yatima, walemavu na walioko katika mazingira magumu.
Askofu huyo alisema wabunge na mawaziri na hata marais waliotangulia, akiwamo Rais Jakaya Kikwete, watambue kwamba elimu waliyo nayo na afya walizonazo, zimetokana na vituo vya mashirika ya kidini, hivyo si vyema kudai kuwa ndio wanaochangia kuyumba kwa uchumi wa nchi.
Alihoji: "Iweje leo kwenye karne ya 21 ionekane kwamba mashirika ya dini ndiyo yanayosababisha upungufu wa bajeti ya Serikali wakati mashirika ya dini yanachangia sehemu kubwa ya afya, elimu na huduma zote za jamii?" Alisema kupuuza mchango huo wa mashirika ya dini ni kuanzisha mtafaruku, "kwa hiyo tunawasihi wabunge, mawaziri, wanasheria, Rais watafakari kwa makini jambo hilo."
Askofu Mwamasika alisema serikali kabla ya kutoa uamuzi kama huo ilistahili kwanza kukutana na viongozi wa dini na wazee kama ambavyo alivyokuwa akifanya Rais Julius Nyerere wakati alipotaka kufanya uamuzi mkubwa kama huo. Hata hivyo alisema hotuba ya Rais Jumatano wiki hii alipozungumza na wazee wa Dodoma, ililenga kuwaondolea shida Watanzania na kuinua uchumi wa nchi.
Alisema Taifa liliipokea hotuba ya Rais kwa furaha, kwani ililenga kumkomboa mwananchi wa chini; lakini ya Waziri wa Fedha na Uchumi, iliona namna ya kunusuru uchumi ni kufuta msamaha wa kodi uliokuwa unatolewa kwa mashirika ya dini. "Kwa kweli Waziri wa Fedha amevuruga." Alisema KKKT inapinga hatua hiyo.
"Nasema tunapinga na sisi maaskofu tumekubaliana kuwa kama Serikali haitabatilisha uamuzi wake tutaandamana hadi kwa Rais Kikwete, kwani hatuwezi kukubali watu wetu waendelee kupata shida wakati kaulimbiu ya Rais ni Maisha Bora kwa kila Mtanzania." KKKT ina hospitali 23, zahanati 139 na vituo vya udiakonia 19.
Askofu Mwamasika alisema iwapo serikali itaendelea na uamuzi wake wa kutotoa msamaha wa kodi kwa mashirika ya kidini ina maana hospitali hizo zinaweza kufungwa. Naye Msaidizi wa Katibu wa Jumuiya ya Kikristo (CCT), John Mapesa, alisema alipokea simu nyingi kutoka kwa maaskofu wa madhehebu yanayounda jumuiya hiyo, wakitaka kujua kama jumuiya ifanye nini kuhusu bajeti iliyosomwa na Waziri.
Mapesa alisema kitendo cha serikali kufuta msamaha wa kodi kwa taasisi za kidini kinarudisha nyumba juhudi zinazofanywa na mashirika hayo kuisaidia jamii wajibu ambao unastahili kufanywa na serikali.
"Madhehebu ya kidini yanachofanya ni kuisaidia serikali, kwa hiyo ni lazima ikubali kuwa taasisi hizi za kidini ni wadau wakubwa wa maendeleo, hivyo ni lazima waendelee kuzilea," alisema Mapesa.
Alisema anaamini serikali itafikiria upya uamuzi huo kwani unalenga kuvunja moyo hata wahisani ambao wamekuwa wanatoa fedha na vifaa vyao kwa ajili ya kuzisaidia taasisi za kidini ili ziweze kutoa huduma mbalimbali kama afya na elimu kwa jamii.
Aliongeza kuwa huduma nyingi za makanisa zina mafanikio makubwa kuliko hata ambazo zinasimamiwa na Serikali, hivyo kuna umuhimu wa kuendelea kuzipa taasisi hizo misamaha ili ziendelee kutoa huduma zao kikamilifu.
Alisema haamini kuwa misamaha inayotolewa kwa mashirika ya dini ndio imesababisha uchumi wa nchi kuyumba au mapato kushuka, bali yawezekana kuna mahali ambako misamaha hiyo inatolewa kwa wingi na sasa kusingizia taasisi za kidini.
"Nawaomba wabunge waliangalie jambo hili pale wanapokuwa wanajadili hotuba hiyo ya bajeti, kama wao wanajua na wanaona huduma zinazotolewa na zahanati au hospitali za kidini katika maeneo yao nadhani watapinga jambo hili," alisema.
Mbunge wa Karatu, Dk. Wilbroad Slaa, alisema yeye aliwahi kuwa kiongozi wa dini na anajua kuwa sehemu ambako kuna hospitali ya misheni, serikali haina huduma katika eneo hilo, hivyo kitendo cha kuzifutia misamaha taasisi za kidini ni kuleta umasikini kwa Watanzania.
"Nchi hii ni kubwa, lakini kuna taasisi za kidini zimepeleka huduma kila kona, leo hii unazifutia misamaha ya kodi, si unataka zitoze fedha zaidi kwenye matibabu na kwenye shule, kwa hili hatukubali," alisema Dk Slaa. Juzi akiwasilisha bajeti ya Serikali, Mkulo alisema Serikali inapendekeza kufuta misamaha ya kodi kwa taasisi za kidini na mashirika yasiyokuwa ya kiserikali.
Ila alisema vifaa ambavyo vinaagizwa kwa ajili ya huduma za kiroho vitaendelea kupata msamaha wa kodi. Hata hivyo maaskofu wanasema mambo ya kiroho ni elimu, afya na akili, hivyo serikali inapaswa kufafanua vifaa vya kiroho inavyojua, "yawezekana wanasema Kurani na Biblia tu."
Niliwaandikia karibu mara mbili kuwa wamelala kitanda kimoja na watawala na wamefurahia mahaba ya ufisadi. Ni wao wamekuwa wakiwaalika kila kukicha kwenye tafrija zao na kwenye matembezi yao hawakosi. Sasa leo wameanza kupiga kelele dhidi ya ufisadi na dhidi ya uongozi wanatarajia watawala wacheze chioda?
Leo wachungaji na mashehe wanaanza kusimama na kunyoshea kidole ufisadi waziwazi wanatarajia kweli misamaha ya kodi iendelee?
Walichofanya watawala ni kuwabeep hawa! Kwamba wakiendelea na kelele zao dhidi ya viongozi na kunyoshea kidole watawala wajue serikali ina uwezo na ubavu wa kuwafanya walipe!
Sasa uchaguzi ni wao:
a. Wapige magoti kwa viongozi wa serikali na kuwaahidi kuwa wakirudishiwa misamaha ya kodi hawatapiga kelele dhidi ya viongozi (a.k.a kujihusisha na siasa)
b. Waamue kupandisha gharama za huduma zao za kijamii ili waanze kutengeneza faida kama taasisi nyingine za kibiashara na hivyo kuchangia kwenye pato la taifa. Baadhi ya huduma ambazo inabidi waongeze gharama ni pamoja na hospitali, kliniki, mashule na vyuo mbalimbali.
c. Wafunge baadhi ya huduma zao ambazo ni ngumu kujiendesha na kuziunganisha baadhi ya huduma zao kama wafanyavyavyo wafanyabiashara wengine na hivyo kupunguza gharama za uendeshaji.
d. Huduma zile za misaada (charity works) zisitishwe na kuacha serikali ifanye shughuli hizo kwa ufanisi vinginevyo wataweza vipi kutoa misaada ambayo wanaigharimia kama bidhaa nyingine. Nani ata offset gharama ya kuingiza, kutunza na kusambaza misaada hiyo. Of course, serikali ina uwezo huo! Sudan walijaribu!!
Upande mwingine ni kuwa serikali isilegeze uzi bali ing'ang'anie msimamo wake tuone hawa wachungaji na mashehe watafanya nini zaidi ya kupiga mikwara. Najua jambo moja msitarajie Pengo kuandamana mitaani!!! Hata kina Kilaini msifikirie wanaweza kusimama na mabango!
I know however, rafiki yangu Khalifa Khamisi wa Kwamtoro na wengine wanaweza kuonekana mitaani! Hawa kina Rev. Whoever hawana ujasiri wa kufanya hivyo!
===========================================
Habari Leo
Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Methodius Kilaini ameishauri serikali kupitia upya uamuzi wa kuyafutia msamaha mashirika ya dini na asasi za kiraia. Akizungumza jana na gazeti dada la Daily News, alisema taasisi hizo hazitengenezi faida na badala yake, zipo kwa ajili ya kuwainua watu wa kawaida ambao ni masikini. Alitoa mfano wa huduma za afya zinazotolewa hususan maeneo ya vijijini, ambazo nyingi hutolewa na taasisi za dini.
"Serikali ilipaswa kukaa na wadau kwa ajili kupata ushauri juu ya hasara na faida ya kuondoa msamaha huo kabla ya kutangaza bajeti yake," alisema Kilaini. Wakati huo huo, Naibu Katibu Mkuu (masuala ya dini) wa Baraza Kuu la Waislamu wa Tanzania (BAKWATA), Mohamed Khamis alisema uamuzi huo unakwamisha sera ya Taifa ya kuwapa maisha bora wananchi.
Alisema taasisi za dini hazitengenezi faida na nyingi zinategemea wafadhili. Alisema inapaswa itoe ruzuku kwa taasisi hizo, ili kuziwezesha kuendesha shughuli zake za kila siku. Kwa upande wake, Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Dodoma, Dk peter Mwamasika, alisema maaskofu wako tayari kuandamana kupinga hatua ya serikali ya kuziondolea taasisi za dini misamaha ya kodi.
Akizungumza jana Dodoma, Askofu Mwamasika alisema hatua hiyo ya Serikali ni ya hatari na inaweza kuleta mtafaruku usio na sababu za msingi na kuendelea kuwapa ugumu wa maisha wananchi wanaopata huduma kupitia shule na hospitali zinazomilikiwa na mashirika hayo ya kidini.
Aliishangaa Serikali ya CCM inavyoanza kubadilisha mwelekeo wa utawala wake ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakishirikiana nayo kuhudumia Watanzania. Aliongeza kuwa KKKT ikiwa sehemu jumuiya ya Kikristo Tanzania, inatambua wajibu wake wa kuhudumia mtu mzima yenye maana ya kiroho na kimwili na ndiyo maana inahudumia kwenye elimu, afya, vituo vya watoto yatima, walemavu na walioko katika mazingira magumu.
Askofu huyo alisema wabunge na mawaziri na hata marais waliotangulia, akiwamo Rais Jakaya Kikwete, watambue kwamba elimu waliyo nayo na afya walizonazo, zimetokana na vituo vya mashirika ya kidini, hivyo si vyema kudai kuwa ndio wanaochangia kuyumba kwa uchumi wa nchi.
Alihoji: "Iweje leo kwenye karne ya 21 ionekane kwamba mashirika ya dini ndiyo yanayosababisha upungufu wa bajeti ya Serikali wakati mashirika ya dini yanachangia sehemu kubwa ya afya, elimu na huduma zote za jamii?" Alisema kupuuza mchango huo wa mashirika ya dini ni kuanzisha mtafaruku, "kwa hiyo tunawasihi wabunge, mawaziri, wanasheria, Rais watafakari kwa makini jambo hilo."
Askofu Mwamasika alisema serikali kabla ya kutoa uamuzi kama huo ilistahili kwanza kukutana na viongozi wa dini na wazee kama ambavyo alivyokuwa akifanya Rais Julius Nyerere wakati alipotaka kufanya uamuzi mkubwa kama huo. Hata hivyo alisema hotuba ya Rais Jumatano wiki hii alipozungumza na wazee wa Dodoma, ililenga kuwaondolea shida Watanzania na kuinua uchumi wa nchi.
Alisema Taifa liliipokea hotuba ya Rais kwa furaha, kwani ililenga kumkomboa mwananchi wa chini; lakini ya Waziri wa Fedha na Uchumi, iliona namna ya kunusuru uchumi ni kufuta msamaha wa kodi uliokuwa unatolewa kwa mashirika ya dini. "Kwa kweli Waziri wa Fedha amevuruga." Alisema KKKT inapinga hatua hiyo.
"Nasema tunapinga na sisi maaskofu tumekubaliana kuwa kama Serikali haitabatilisha uamuzi wake tutaandamana hadi kwa Rais Kikwete, kwani hatuwezi kukubali watu wetu waendelee kupata shida wakati kaulimbiu ya Rais ni Maisha Bora kwa kila Mtanzania." KKKT ina hospitali 23, zahanati 139 na vituo vya udiakonia 19.
Askofu Mwamasika alisema iwapo serikali itaendelea na uamuzi wake wa kutotoa msamaha wa kodi kwa mashirika ya kidini ina maana hospitali hizo zinaweza kufungwa. Naye Msaidizi wa Katibu wa Jumuiya ya Kikristo (CCT), John Mapesa, alisema alipokea simu nyingi kutoka kwa maaskofu wa madhehebu yanayounda jumuiya hiyo, wakitaka kujua kama jumuiya ifanye nini kuhusu bajeti iliyosomwa na Waziri.
Mapesa alisema kitendo cha serikali kufuta msamaha wa kodi kwa taasisi za kidini kinarudisha nyumba juhudi zinazofanywa na mashirika hayo kuisaidia jamii wajibu ambao unastahili kufanywa na serikali.
"Madhehebu ya kidini yanachofanya ni kuisaidia serikali, kwa hiyo ni lazima ikubali kuwa taasisi hizi za kidini ni wadau wakubwa wa maendeleo, hivyo ni lazima waendelee kuzilea," alisema Mapesa.
Alisema anaamini serikali itafikiria upya uamuzi huo kwani unalenga kuvunja moyo hata wahisani ambao wamekuwa wanatoa fedha na vifaa vyao kwa ajili ya kuzisaidia taasisi za kidini ili ziweze kutoa huduma mbalimbali kama afya na elimu kwa jamii.
Aliongeza kuwa huduma nyingi za makanisa zina mafanikio makubwa kuliko hata ambazo zinasimamiwa na Serikali, hivyo kuna umuhimu wa kuendelea kuzipa taasisi hizo misamaha ili ziendelee kutoa huduma zao kikamilifu.
Alisema haamini kuwa misamaha inayotolewa kwa mashirika ya dini ndio imesababisha uchumi wa nchi kuyumba au mapato kushuka, bali yawezekana kuna mahali ambako misamaha hiyo inatolewa kwa wingi na sasa kusingizia taasisi za kidini.
"Nawaomba wabunge waliangalie jambo hili pale wanapokuwa wanajadili hotuba hiyo ya bajeti, kama wao wanajua na wanaona huduma zinazotolewa na zahanati au hospitali za kidini katika maeneo yao nadhani watapinga jambo hili," alisema.
Mbunge wa Karatu, Dk. Wilbroad Slaa, alisema yeye aliwahi kuwa kiongozi wa dini na anajua kuwa sehemu ambako kuna hospitali ya misheni, serikali haina huduma katika eneo hilo, hivyo kitendo cha kuzifutia misamaha taasisi za kidini ni kuleta umasikini kwa Watanzania.
"Nchi hii ni kubwa, lakini kuna taasisi za kidini zimepeleka huduma kila kona, leo hii unazifutia misamaha ya kodi, si unataka zitoze fedha zaidi kwenye matibabu na kwenye shule, kwa hili hatukubali," alisema Dk Slaa. Juzi akiwasilisha bajeti ya Serikali, Mkulo alisema Serikali inapendekeza kufuta misamaha ya kodi kwa taasisi za kidini na mashirika yasiyokuwa ya kiserikali.
Ila alisema vifaa ambavyo vinaagizwa kwa ajili ya huduma za kiroho vitaendelea kupata msamaha wa kodi. Hata hivyo maaskofu wanasema mambo ya kiroho ni elimu, afya na akili, hivyo serikali inapaswa kufafanua vifaa vya kiroho inavyojua, "yawezekana wanasema Kurani na Biblia tu."