Wachungaji/mapadre hamwogopi mungu kufungisha ndoa zikiwa na mimba makanisani

ni Kujamiiana

Nilivyoelewa MIMBA ni MATOKEO TU ya KUJAMIIANA
 
Mhhhhhh hapooooooooooo nnaona NDOA NI CHACHE SANA

HASA UPANDE WA DAR ES SALAAM KARIBU KILA NDOA MAKANISANI KAMA HAWANA MIMBA BASI WANAISHI PAMOJA NA KAMA HAWAISHI PAMOJA BASI WALIKUWA WANAZINI KABLA YA NDOA....
 
ni Kujamiiana

Nilivyoelewa MIMBA ni MATOKEO TU ya KUJAMIIANA

Sasa Kama ni Kujamiiana ni kwa nini Basi washikiwe Bango wenye Mimba ilhali wako wengi tu waliojamiiana kabla lakini hawakupata Mimba. Kwani yule Mwenye Mimba kabla ya Ndoa hana haki katika Ufalme wa Mungu hata kama akitubu hiyo dhambi yake ambayo haina tofauti na Mzinzi yeyote ambaye hakunasa Mimba?
 
Mtowa maoni inaelekea unasoma Bible iyokwisha pitwa na wakati ambayo hakidhi mahitaji ya wafuwasi wake katika karne hii pia unasahau kuwa Bible imekuwa ik upgrade kwa kudhi maisha ya kile na ndio maana makanisa mengi kwa sasa yamekubali kuwa Gays na Lisbia wanaweza kuwa wachungaji wa makanisa kwani wanachokifanya kanisani ni kumtumikia Mungu wao,pia katika ukatoliki kulikuwahakuna Ngono kabla ya ndowa lakini kwa sasa hilo limepanguswa ,binafsi naliona hilo halina matatizo pia angalau wao wanafunga ndowa wazungu walioleta Hii dini hapa Tz wao sikuhizi hata haya mambo ya ndowa hayana nguvu wewe zalisha tu .
 
Deuteronomy 22:20-21 NAB

LAKINI IKIWA NI KWELI NENO HILI..LA KUTOONEKANA KWAKE YULE KIJANA ALAMA ZA UBIKIRA; NA WAMTOE NJE YULE KIJANA MLANGONI PA NYUMBA YA BABAKE WAMPIGE MAWE MPAKA AFE..KWA ALIVYOFANYA UPUMBAFU WAKE...KWA KUFANYA UKAHABA KATIKA NYUMBA YA BABA YAKE......

SO UKIWA UNAZINI UKIWA BADO KWA WAZAZI WAKO HAKUNA SABABU YA WEWE KUTOPIGWA MAWE...MNALIJUA HILI...SO UTAONA MIMBA NI KAMA MATOKEO TU NA DHANA ZAIDI NI KUZINI .....YAANI UZINZI..MMMHHH TOPIC NJEMA

Na wanaofanya kazi Jumamosi nao wapigwe mawe? Yesu si alisema asiye na dhambi awe wa kwanza kutupa jiwe, sasa wewe unayetaka kupiga watu mawe huna dhambi?

Na vipi kuhusu contradictions hizi katika biblia? Agano la kale linakwambia piga mawe, yesu katika agano jipya anakwambia asiye na dhambi awe wa kwanza kupiga jiwe.

Hivi haya ni maneno ya an omnipotent omniscient godhead kweli au tunadanganyana kwa hadithi za wayahudi tu? Maana hata kama mimi ndiye ningepewa kazi ya kuandika kitabu cha neno la mungu ningeona hii inconsistency.
 
Mtowa maoni inaelekea unasoma Bible iyokwisha pitwa na wakati ambayo hakidhi mahitaji ya wafuwasi wake katika karne hii pia unasahau kuwa Bible imekuwa ik upgrade kwa kudhi maisha ya kile na ndio maana makanisa mengi kwa sasa yamekubali kuwa Gays na Lisbia wanaweza kuwa wachungaji wa makanisa kwani wanachokifanya kanisani ni kumtumikia Mungu wao,pia katika ukatoliki kulikuwahakuna Ngono kabla ya ndowa lakini kwa sasa hilo limepanguswa ,binafsi naliona hilo halina matatizo pia angalau wao wanafunga ndowa wazungu walioleta Hii dini hapa Tz wao sikuhizi hata haya mambo ya ndowa hayana nguvu wewe zalisha tu .

SOma michango ya Bluray labda itakusaidia kupanua mawazo yako.
 
Tatizo la Watu hapa wakiona Kichwa cha Habari kina neno Padre/Mchungaji basi wanaacha kabisa kushirikia akili zao, mambo mengine ni Common sense tu jamani

Kwa Yesu hakuna dhambi isiyosameheka ilimradi mtendaji amemwendea Mungu na Kuomba Msamaha!

Kama unammega Mchumba wako halafu ukatubu hiyo dhambi yako, siku ya ndoa Mungu hakuhesabu wewe kama Mzinzi maana yeye husamehe na kusahau
 
Pdidy sio makanisa yote, makanisa ya kiprotestant ndio yako hivi, nayo hutegemea aina ya pastor wa mahali hapo,

Mimba ni alama ya kuwa hawa watu walikutana kimwili, Bible hairuhusu kukutana kimwili kabla ya ndoa, na hatujui namna ya kujua hawa walikutana kimwili au la, Mimba ni moja ya kithibitisho kuwa hawa watu walikiuka maadili ya biblia, kuruhusu watu kuoana na mimba ni kuhalalisha tendo lifanyike kabla ya ndoa!

Huwa nasema kila siku there is no compromise katika kumfuata Mungu,so as there is no compromise kufuata katiba zetu za organisations, taifa, n.k

Kushindwa kulinda na kusimamia kile kinachopaswa kufuatwa kwa gharama yeyote ni ushahidi tosha wa dini za kuletewa na kurithishwa, NDIO tunatka hapo tunaenda CCM,CHADEMA , kwenye makampuni tunayafisadi hili hali tukijua katiba na miiko!

Hii ni makosa, I am pastor though!

Ndugu Waberoya kama wanavyojadili wengine hususan Bluray, kimsingi hapa wote tunakubaliana kuwa kufunga ndoa ni mimba kanisani ni kosa na assumption ni kuwa hawa wawili walishashiriki tendo la ndoa. (mimi mmojawapo). suala ni kuwa mtu akitenda dhambi jamii na kanisa havipaswi kumlaani bali ni kumsaidia atubu arudi kundini. katika vifungu vya biblia (ukristo) inasisitizwa sana kuhusu kutubu na kumrudia Muumba.
mimi nilimuona Padri na tulielezana ukweli kwa kirefu, tukatubu mimi na mwezangu pale kanisani na tukaruhusiwa kufunga ndoa.
Biblia inaonyesha udhaifu tulionao na inatufundisha kumrudia Muumba kila tunapoenda nje ya njia yake.
mtu akitubu na kusamehewa na kuruhusiwa kufunga ndoa si kuharalisha uzinzi bali ni kuwarudisha kundini wazinzi hawa. hivi ukizuia watu wasifunge ndoa unaondoa tatizo au ndiyo unaongeza tatizo?
 
Mhhhhhh hapooooooooooo nnaona NDOA NI CHACHE SANA

HASA UPANDE WA DAR ES SALAAM KARIBU KILA NDOA MAKANISANI KAMA HAWANA MIMBA BASI WANAISHI PAMOJA NA KAMA HAWAISHI PAMOJA BASI WALIKUWA WANAZINI KABLA YA NDOA....

Utawajua tu! mkuu, mimi nimeoa mwaka 2006, sikuwahi kukutana kimwili na mke wangu kabla ya ndoa, wala aina ya tendo lolote linaloweza kutafsirika ni mapenzi! Yet I live in DSM! Ndio nikauliza ni aina ya makanisa gani hayo?? sio wote mkuu, trust me wako wengi, japo hawavumi. ni sawa na walewale kuwa bila nyumba ndogo hakuna maisha, simply kwa sababu yeye ana udhaifu huo!

Wakuu kwani tatizo ni Kujamiiana kabla ya Ndoa au Mimba kabla ya Ndoa?

Tatizo kubwa hapa ndugu ni kujamiiana kabla ya ndoa. Mimba ni matokeo na only indicator kuwa hawa watu walikutana kimwili, kwa hiyo NI KITU AMBACHO wachungaji wana uwezo wa ku-control, kwa maana ya kukemea, ukikubali matokeo maana yake umekubali source(umehalalisha practise). na hata watoto ndani ya nyumba tunawaonya kwa makosa wanayofanya, then tunakuwa tumerekebisha tabia yake,

Majaji wanawahukumu waliopelekwa mahakamani, japo wezi wako wengi, polisi hukamata wanaowaona, japo wezi wako wengi, tunaowaita mafisadi tutawaita tu wezi kwa sababu tumewajua, lakini nyuma ya pazia wako wezi, mafisadi na wakosaji wengi.

Wachungaji wangedeal na haya matokeo, ni rahisi kuzuia chanzo,just imagine watoto wanaopevuka miaka wanaambiwa ngono haina makosa, maana hata ukipata mimba unakaribishwa, otherwise what is religion then??

Tuite spedi spedi, japo ni wazuri kutetea haya mambo, mbona the same makanisa zamani haya yalikuwa hayatokei? na yakitokea wachungaji walikuwa wanakataa? kwa nini imeanza kuanzia miaka ya 1990, na imekithiri miaka ya 2000, miaka 50 ijayo, si tutaenda ngazi nyingine ya immoral?? au zamani hawakuwa na viungo active vya uzazi??

Lazima tujue chanzo cha hili tatizo, tuliseme, tujadili, bila kujitetea hata kama sisi wakosaji! then tujue ikiwa hili LA MIMBA LINATETEWA HIVI JE YA UFISADI?

ARE OUR CHURCHES IS REAL CHURCHES OR JUST A SOCIAL CLUBS?? ARE THEY REAL FOLLOWING WHATS WRITTEN IN THE BIBLE?

Lets go to the basics??
 
Unajua tatizo tunalolalamikia hapa ni si haki kufungisha ndoa za wenye mimba na wasio na mimba at the same tyme lazima tuwaheshimu hawa wanaokuja kanisani hawajakutana kimwili......ukisoma kwenye biblia
Mama Mia hili swala siku hizi gumu sana, watu wengi siku hizi wanafunga ndoa wameshakutana kimwili, ni asilimia chache sana wanafunga ndoa takatifu.
Sema hao wengine wanakosea wanakutana kimwili wanasahau hadi mimba inaingia, hivyo wanaona bora kufunga ndoa kabla mtoto hajazaliwa ili mtoto aje kuzaliwa ndani ya ndoa.
 
Mtumishi waberoya tuko pamoja
swala kubwa ni kujua jamani chanzo cha haya nini??na je tutaanzaje kulitatua...ni kweli tazama wote wamefanya dhambi na kupungukiwa na utukufu wa mungu..sasa uwezi sema kwa saababu wote tumefanya dhambi basi tuendelee na dhambi;NOP....tunaitaji kuwa serious na watu watakaoweza kusaidia ni hawa watumishi wa MUNGU WACHUNGAJI/MAPADRE ...KAMA KANISA LINAFUNGISHA MTU MWENYE MIMBA UNATARAJIA NINI KWA MTOTO ATAKAEZALIWA UTAMWAMBIA NGONO NJE YA NDOA NI DHAMBI.????????sawa wakati tukijitetea tuangalie wapi tutarekebisha..kila la kheri kwa wale walioko njiani kuelekea kwenye ndoa...
 
wanakutana kimwili wanasahau hadi mimba inaingia, hivyo wanaona bora kufunga ndoa kabla mtoto hajazaliwa ili mtoto aje kuzaliwa ndani ya ndoa.

imetulia hiyooooooooooooooooooooo
 
Utawajua tu! mkuu, mimi nimeoa mwaka 2006, sikuwahi kukutana kimwili na mke wangu kabla ya ndoa, wala aina ya tendo lolote linaloweza kutafsirika ni mapenzi! Yet I live in DSM! Ndio nikauliza ni aina ya makanisa gani hayo?? sio wote mkuu, trust me wako wengi, japo hawavumi. ni sawa na walewale kuwa bila nyumba ndogo hakuna maisha, simply kwa sababu yeye ana udhaifu huo!



Tatizo kubwa hapa ndugu ni kujamiiana kabla ya ndoa. Mimba ni matokeo na only indicator kuwa hawa watu walikutana kimwili, kwa hiyo NI KITU AMBACHO wachungaji wana uwezo wa ku-control, kwa maana ya kukemea, ukikubali matokeo maana yake umekubali source(umehalalisha practise). na hata watoto ndani ya nyumba tunawaonya kwa makosa wanayofanya, then tunakuwa tumerekebisha tabia yake,

Majaji wanawahukumu waliopelekwa mahakamani, japo wezi wako wengi, polisi hukamata wanaowaona, japo wezi wako wengi, tunaowaita mafisadi tutawaita tu wezi kwa sababu tumewajua, lakini nyuma ya pazia wako wezi, mafisadi na wakosaji wengi.

Wachungaji wangedeal na haya matokeo, ni rahisi kuzuia chanzo,just imagine watoto wanaopevuka miaka wanaambiwa ngono haina makosa, maana hata ukipata mimba unakaribishwa, otherwise what is religion then??

Tuite spedi spedi, japo ni wazuri kutetea haya mambo, mbona the same makanisa zamani haya yalikuwa hayatokei? na yakitokea wachungaji walikuwa wanakataa? kwa nini imeanza kuanzia miaka ya 1990, na imekithiri miaka ya 2000, miaka 50 ijayo, si tutaenda ngazi nyingine ya immoral?? au zamani hawakuwa na viungo active vya uzazi??

Lazima tujue chanzo cha hili tatizo, tuliseme, tujadili, bila kujitetea hata kama sisi wakosaji! then tujue ikiwa hili LA MIMBA LINATETEWA HIVI JE YA UFISADI?

ARE OUR CHURCHES IS REAL CHURCHES OR JUST A SOCIAL CLUBS?? ARE THEY REAL FOLLOWING WHATS WRITTEN IN THE BIBLE?

Lets go to the basics??

Mkuu wangu Waberoya ( Mhandisi na Mchungaji) wewe ni Mchungaji kama status yako inavyoonyesha!

Jee unataka Wachungaji wa control vipi hii ishu? Kwa Kutaa kufungisha Ndoa zao?

Imagine wamekuja watu with round belled stomach ( Namaanisha wajawazito) kwako wewe Mchungaji, watu hawa walishatubu dhambi yao ya Uzinzi na Mungu aliyesirini amewasamehe. Sasa kama Mungu mwenyewe amewasamehe wewe mchungaji unapata wapi mamlaka ya Kukataa kutumika na Mungu kuwaunganisha Wawili hawa?

Labda ungeeleza ni namna gani wachungaji na Mapadre wanavyoweza kuli control hili jambo pasipo kumkwaza mungu aliyesamehe na kuvitakasa Viumbe hivi!
 
Hivi ndoa nini haswa? Je kama mmefanya mambo yote ya kimila kwa mfano mwanaume amepeleka posa na mahari upande wa mwanamke. Na pande zote za kike na kiume wamejua kwamba watu hawa ni wachumba. Je hapo kama mkiamua kula tunda kuna dhambi au tayari imekuwa halali kwa kuwa ndoa ya kimila imefanyika?
 
Unajua tatizo tunalolalamikia hapa ni si haki kufungisha ndoa za wenye mimba na wasio na mimba at the same tyme lazima tuwaheshimu hawa wanaokuja kanisani hawajakutana kimwili......ukisoma kwenye biblia

Tuwaheshimu vipi? Na je tutawajuaje?
 
Hivi ndoa nini haswa? Je kama mmefanya mambo yote ya kimila kwa mfano mwanaume amepeleka posa na mahari upande wa mwanamke. Na pande zote za kike na kiume wamejua kwamba watu hawa ni wachumba. Je hapo kama mkiamua kula tunda kuna dhambi au tayari imekuwa halali kwa kuwa ndoa ya kimila imefanyika?

well said, swali ni kwa nini watu wanalazimisha waende kanisani? wakati ndoa ya kimila ni ndoa, ndoa ya serikali ni ndoa!

Mkuu wangu Waberoya ( Mhandisi na Mchungaji) wewe ni Mchungaji kama status yako inavyoonyesha!

Jee unataka Wachungaji wa control vipi hii ishu? Kwa Kutaa kufungisha Ndoa zao?

Imagine wamekuja watu with round belled stomach ( Namaanisha wajawazito) kwako wewe Mchungaji, watu hawa walishatubu dhambi yao ya Uzinzi na Mungu aliyesirini amewasamehe. Sasa kama Mungu mwenyewe amewasamehe wewe mchungaji unapata wapi mamlaka ya Kukataa kutumika na Mungu kuwaunganisha Wawili hawa?

Labda ungeeleza ni namna gani wachungaji na Mapadre wanavyoweza kuli control hili jambo pasipo kumkwaza mungu aliyesamehe na kuvitakasa Viumbe hivi!



Mkuu swali lako ni jepesi sana, uwe mpole tujuvyane

Kwanza biblia inakataza swala kwa kufanya mapenzi kabla ya ndoa, ni agano la kundi na Mungu, unapoamua kuwa mkristo unaamua kuendana na sheria na taratibu zake.

Mkuu unajua kuna tatizo sana na dini za kurithi; dini za wazazi!

Wamekosea? ndiyo

Huyo Mungu unayesema anasamehe hujaeleza pia kuwa anahasira, anaadhibu, hataki kabisa dhambi, anakasirishwa na dhambi, uko upande mmoja tu wa shilingi kuwa anasamehe!

Wachungaji huwa wanachukua hatua gani kwa watu waliofanya dhambi hizi za uzinzi, kumbuka uzinzi sio bahati mbaya, just imagine all processes, mpaka mtu anafanya mara moja, mbili, tatu, maana yake haji-feel guilty, kwa maana nyingine automatically kuwa kwenye kundi ambalo linaamini anachofanya ni dhambi, ameshajitoa!! Pozi hapo

Ni kweli binadamu huwa tunafanya dhambi tunazo jua fika ni dhambi, je utajuaje huyu mtu amefanya toba ya kweli? Uhusiano wa muumini na Mungu hauanzii pale anapotaka kufunga ndoa au anapokuwa na Mimba! Inatakiwa kila siku!!!

Mtu hajaenda kanisani miaka 2, leo anataka kuoa mchungaji anamwambia alipe mafungu ya kumi then anawafungisha ndoa! Hii haikubaliki

Taratibu ya biblia kwa wale waumini waaminifu, walioanguka kwa ‘bahati mbaya’ siyo lazima wawe wajawazito, ili mradi wamejulikana, wakaulizwa wakakubali, WANATENGWA na kanisa, kutengwa ni alama ya kumpa muda wa muumini kutubia kosa lake, kutafakari na pia ni FIMBO kwa waumini wengine wasije wakafanya makosa kama hayo

Ndugu, tatizo tumejaa unafiki, kuwa mkristo lakini haufuati taratibu za kikristo, hakukufanyi kuwa mkristo! Hata kama unajiona wewe ni mkristo

Tunaogopa wazazi na jamii inayotuzunguka, ndiyo maana the same ndoa zilizofungwa kwa style hii, huwaoni tena kanisani mpaka wanapokuja kubatiza mtoto!

Je wachungaji huwa wanawatenga waumini? Hapana , kwa nini?

Kumbuka hapa hawalaumiwi waumini, bali wachungaji!

  • Je waumini wanajua kuwa wakifanya makosa wanaweza kutengwa?? NO
  • Je wanajua kuwa Mungu siyo anasamehe tu bali pia anahadhibu? NO
  • Je huyu muumini unayetaka kumfungisha ndoa akiwa na mimba unamjua siku zote , au leo tu unapotaka kufunga ndoa –No

Just imagine maana ya mchungaji ni-kutrack tabia ya waumini!
Kila maswali ni NO, hata wewe pengine hujui kuwa kuna kutengwa na aliyen-institute hili ni Yesu mwenyewe!

(Matthew 18:15,18) (1 Corinthians 5:11; 1 Timothy 1:20; Titus 3:10 comp. (2 Corinthians 1:23; 13:10) (1 Corinthians 5:5 (2 Timothy 3:17) (1 Timothy 1:20) (1 Corinthians 5:1 (Matthew 18:18) (1 Corinthians 5:3; Titus 3:10) (1 Corinthians 5:4) (2 Corinthians 2:9) (2 Corinthians 2:6-10)


Unaweza usisome hiyo mistari ukasoma hii article, inafunua uhusiano wa Mungu na dhambi!

http://bibletools.org/index.cfm/fuseaction/Topical.show/RTD/CGG/ID/2922/Excommunication.htm


Ni lazima kufungia ndoa kanisani??

Kuna ndoa za kimila,za kiserikali, after all marriage certificate ni ya serikali!

Kwa nini watu wanalazimisha kwenda kanisani, na wanavunja kabisa sheria za kanisa?

Kesho wakija gay na lesbian na wakatoa visingizio hivyo hivyo utakataa??

Nimeuliza mbona hili swala halikuwepo miaka iliyopita??biblia imebadilika?

Biblia haikuacha kitu, inasema na athari zake ni kukwepa kuchafua kanisa zima, mkuu usipopatajibu hapa na kukubali, basi kubali makanisa yetu ni social clubs, you can no anything by the name that God forgives!!!!,

Kwa hiyo, tuue, tuibe, tufanye uchafu woote, simply Mungu anasamehe, this is crazy, and believe me christianity is not like that.

BIBLIA INASEMA WAZI ILE ADHABU YA KUTENGWA ANAYOPEWA MTU, NI KWA FAIDA YAKE, ILI AMRUDIE MUNGU, hatuzioni hizi adhabu!

Wachungaji leo ni washikaji, you can give them anything, and they can do anything!

Mkuu hivi ni lazima kweli kulazimisha kuwa mkristo kama hutaki kufuata ‘katiba zake’ kweli sisi ni wenye dhambi, tunakosea, then are ready to receive punishment ngau kidogo tu ya kutengwa , ili kufurahia uamuzi wetu wa kuwa wakristo??
Kama wachungaji wangekuwa wakali, leo usingeona haya,

Lingine kama mmeisha peana mamba, ndoa maana yake ni nini?? NANI ALIWAFUNGISHA NDOA ADAM NA HAWA?? Kitendo cha kukutana kimwili tayari ndoa kabisa then kanisani wakishatubu na kufuta taratibu nilizoeleza basi ni kubariki ndoa! Siyo kufunga ndoa!!!! they can do even after birth! kwa nini mtu na mtumbo anasimama madhabahuni , what are we teaching this generation?

Tuache unafiki siyo lazima kuwa mkristo, kama huuwezi, ukienda jeshini unafuta taratibu zote za jeshi ikiwa na kukubali adhabu utakayopewa na jeshi ukienda kinyume, kwa Mungu ni zaidi

Ukristo ni kiapo, ni uamuzi, si mazoea kama tunavyoona hapa, wala kujipa moyo.

Nadhani umeelewa sasa wajibu wa mchungaji

Nimesali kanisa la TAG-songea mjini miaka 2, sijawah kuona hik kitu
Nimesali mnazi mmoja EAGT mika 7 sijawahi kuona hii kitu

Nimesali All nationa church -Canada, miaka 2, ndoa 7 zimefungwa sijaona hii kitu



Nimealikwa harusi za marafiki zangu Lutheran, RC, Moravian, sabato n.k this is so common! japo si yote

JUST IMAGINE UKISHAANZA NA MMOJA WA MIMBA UKAFUNGISHA THEN TABIA HIYO ITAKITHIRI KATIKA HILO KANISA, THEN TUNASEMAJE WASIOPATA MIMBA? TUSEMEJE JUU YA UKIMWI? VIJANA WANAAACHANA KILA SIKU KISA WAMESHAONJANA hawa wachungaji si wana promote hii hali?

Kosa kama ulilifanya sema nilikosa , kemea vizazi vijavyo visirithi huu uchafu, how can you tell them, usifanye mapenzi kabla ya ndoa?? au tulifute hili??
 
Waberoya sina cha kujazia usikuu huu mungu akubariki na usiku mwema wacha mwenye masikio na asikie maneno ya manabii

hovyo basi ni wajibu wetu jf kuchagua lipi jema unaloliona linafaa kwako na baya kuliacha hapa.....

Kila la kheri
 
Tatizo ni kwamba the whole enterprise is a fraudulent monopoly. The bigger problem here is the fact that god does not exist and therefore the bible cannot be the word of god, and from there everything based on the bible as "the word of god" is confusingly incosinstent and naturally it falls short of godlike wisdom.

Huku tunaambiwa anayezini apigwe mawe, kule tunaambiwa asiye na dhambi awe wa kwanza kurusha jiwe, kitabu hicho hicho.

Halafu unataka kuniambia hiki kitabu cha mungu?

Mimi ndiyo maana nishajinyofoa kutoka katika minyororo ya utumwa huu, utumwa wa dini na institutions zake.
 
Ndoa ziwe za wenye mimba au la..ni ishu ya wahusika na Mungu wao.Hao wanaoshangaa kitendo hicho, ina maana wao wako na haki asilimia 100? Utakuta wao ndio wa kwanza kuzini na kushiriki utoaji mimba mradi waonekane kwa nje kuwa hawana dhambi kwa vile matumbo yako flat!
ACHENI HIZO....MNA DHAMBI KUBWA ZAIDI YA KUPATA MIMBA NA KUFUNGA NDOA!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom