Elections 2010 Wachukuwa T-Shirt za CCM lakini wasema mabadiliko lazima

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
234


Leo kwa kuwa siyo siku ya kazi nilijihimu kwenda soko la Ilala kujipatia mahitaji yangu.

Nilipoteremka stand ya Ilala sokoni (kutokea maeneo ya Buguruni) niliona watu wengi, hasa vijana wameshika T shirt na kofia za CCM (hawajazivaa). Nikakumbuka pale pana ofisi ya CCM ya mkoa – karibu na Kobis petrol station. Walikuwa wanazigawa bure – Takukuru mko wapi?

Lakini kuna kitu kimoja kilinitia moyo sana na naweza kusema bila kujiuma mdomo kwamba Watanzania wanataka mabadiliko – pamoja na hizo hongo za bure za CCM.

Nilipoingia kwenye mvurugano wa watu wanaouza mboga na matunda, nilisikia vijana (wabeba mizigo etc) wakiambizana: “Nendeni mkachukue nguo za bure – lakini mabadiliko lazima.”

Mwingine akijibu: “Umenena – taabu hii tuliyo nayo hadi lini?”

Jamaa mmoja mtu mzima aliyekuwa karibu ananunua majani ya maboga akasema “Mabadiliko lazima mwaka huu – tumechoka kula majani kama mbuzi – kwani nyama haikamatiki.”

Mwingine alimjibu huyo kwa kicheko: “Si alisema yule waziri fisadi kwamba hata ikibidi tule majani, ndege ya rais ni lazima inunuliwe? Mmesahau? Si mnaona majani yalivyotanda hapa? (akionyesha mboga za majani za kila aina zilivyojaa sokoni pale.”

Mwingine mzee mmoja akasema: “Aliyesema si yule waziri mwenye kesi aliyenadiwa na Kikwete kwamba mtu safi?”

Nikaendelea na shughuli zangu – huku nikajawa na mawazo makubwa nikiwaza mabadiliko yaja iwapo watu wengi wanazo fikra za namna hiyo.
 
Ukisema sana Mkuu watakwambia hata 1995 kwa Mrema ilikuwa hivyo na Mkapa akashinda. Ila ndani ya mioyo yao CCM wanajua mwaka huu kampeni hazikuwa rahisi na wanategemea hila katika kushinda
 
Na bado jana waliaanza kwenye wizara ya mambo ya ndani kuwapa elfu 30 kila moja leo wantoa nguo, ila ukweli uko pale pale TUNATAKA MABADILIKO, pesa na nguo vyote ni vya kupita tu ndani ya wiki 4 nguo imechoka, pesa siku 2 imekwisha lakini shida zingine zikopalepale, hima wananchi kesho tukatoe AJIRA MPYA KWA RAIS MPYA WA TANO WA SERIKALI YA JAMUHURI WA MUUNGANO WA TANZANIA atakaye tujali sisi MBAYUWAYU NA FAMILIA ZETU
 
Kwa kweli wananchi hawa wanasema ukweli mtupu. Nyama haikamatiki sasa hivi. Hata majani yenyewe nayo hayakamatiki
 
Ukisema sana Mkuu watakwambia hata 1995 kwa Mrema ilikuwa hivyo na Mkapa akashinda. Ila ndani ya mioyo yao CCM wanajua mwaka huu kampeni hazikuwa rahisi na wanategemea hila katika kushinda

Napenda kukutoa hofu kwamba kushinda kwa ssm kma wanategemea hila basi njama za aina yoyote tunayojua na tusiyojua haitafanikiwa kwa kuwa Mungu yuko kazini kama unaaimani amini hivyo.:nono:
 
Back
Top Bottom