Wachina watano wadakwa wakisafirisha makinikia

Replica

JF-Expert Member
Aug 28, 2017
1,444
7,800
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mara limewakamata raia watano kutoka China wanaomiliki mgodi wa Zem Tanzania Limeted katika kijiji cha Nyasirori wilayani Butiama, wakitorosha mchanga wenye madini mbalimbali maarufu kama makinikia.

Raia hao wa China wamekamatwa wakiwa katika harakati za kusafirisha mchanga huo kwenda Jijini Dar es Salaam kinyume na taratibu na sheria za nchi.

china2.jpg


Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mara Kamishina Msaidizi wa Jeshi la Polisi ACP Japhary Mohamed, amesema walipata taarifa kuhusu wawekezaji hao kuandaa mpango wa kutorosha mchanga huo wa madini na ndipo Jeshi la Polisi lilipolazimika kuweka mtego ambao umewezesha kukamatwa.

Anasema kuwa walifanikiwa kukamata magari mawili katika barabara kuu ya Mwanza-Musoma yakiwa na masanduku 14 yenye mchanga huo wenye madini ya aina mbalimbali.
 
Eti wanampango wa kusafirisha hapa watakuwa wamekosea

Waseme hao wachina wamekuwa wakisafirisha mchanga huo wa madini mara nyingi
 
Tuna urafiki wa 'damu' na wachina ulio wekewa 'amini' wakati wa awamu ya nne. Hayo si makinikia, ni dhahabu ndani ya makinikia. Makampuni ya ujenzi ya wachina ni wachuuzi wa mbao, magogo, asali, nta na mengineyo. wakati hawana leseni za shughuli hizo. Ni wizi, wakitumia 'amini' tuliyolishana.
 
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mara limewakamata raia watano kutoka China wanaomiliki mgodi wa Zem Tanzania Limeted katika kijiji cha Nyasirori wilayani Butiama, wakitorosha mchanga wenye madini mbalimbali maarufu kama makinikia.

Raia hao wa China wamekamatwa wakiwa katika harakati za kusafirisha mchanga huo kwenda Jijini Dar es Salaam kinyume na taratibu na sheria za nchi.

Polisi wakishaacha tabia ya unafiki kama ule wa anadhani sisi tungejuaje si fulani ndo katwambia mbona uhalifu wa aina zote hapa nchini utakwisha kwasababu kila uhalifu utajulikana kabla haujatoakea watu watatafuta kazi za kufanya na siyo uhalifu. Sasa wengi wa polisi hawana siri wanawambia whalifu fulani ndo katutonya wahalifu wanamdhuru mtoa taarifa...ni shidaaaaa...

china2.jpg


Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mara Kamishina Msaidizi wa Jeshi la Polisi ACP Japhary Mohamed, amesema walipata taarifa kuhusu wawekezaji hao kuandaa mpango wa kutorosha mchanga huo wa madini na ndipo Jeshi la Polisi lilipolazimika kuweka mtego ambao umewezesha kukamatwa.

Anasema kuwa walifanikiwa kukamata magari mawili katika barabara kuu ya Mwanza-Musoma yakiwa na masanduku 14 yenye mchanga huo wenye madini ya aina mbalimbali.
 
Back
Top Bottom