Wachimbaji wadogo wilayani Mbogwe kupata umeme ndani ya siku kumi

mamayoyo1

JF-Expert Member
Jul 25, 2018
1,011
1,019
Wachimbaji wadogo katika machimbo ya Nyakafuru yaliyo katika Kijiji cha Nyakafuru wilayani Mbogwe wameonesha kufurahishwa na ahadi ya Waziri wa Nishati, Dkt Medard Kalemani ya kufikisha umeme katika machimbo hayo ndani ya siku kumi.

Ahadi hiyo aliitoa jana mara baada ya kufanya ziara ya kikazi wilayani Mbogwe mkoani Geita ambapo akiwa katika machimbo hayo, wachimbaji hao walilalamika kuhusu gharama kubwa wanazotumia katika kununua mafuta ya kuendesha mitambo mbalimbali ikiwemo ya kuchenjulia ya madini.
KLM-2.png
Waziri wa Nishati, Dkt Medard Kalemani (katikati) akikata utepe kuashiria uzinduzi wa umeme katika Kijiji cha Kasosobe, Kitongoji cha Mkolani wilayani Mbogwe. Wa Tatu kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Mbogwe, Martha Mkupasi na wa kwanza kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Amos Maganga.

Kwa nyakati tofauti walieleza kuwa, mchimbaji mmoja anaweza kutumia zaidi ya shilingi milioni 1.5 kwa ajili ya mafuta ya kuendeshea mitambo suala ambalo linawafanya kutopata faida inayostahiki katika shughuli zao.

Kutokana na hilo, Dkt Kalemani alisema kuwa, “kutoka umeme unapoishia hadi hapa ni kilometa 1.5 tu, na hapa kuna wachimbaji wadogo zaidi ya Elfu Nne na mashine za kuchenjulia madini zaidi ya 200, hivyo nakuagiza Meneja wa TANESCO kuleta umeme hapa ndani ya siku Kumi na pia muwafungie transfoma itakayohudumia eneo hili,”.
KLM-3.png
 
Back
Top Bottom