Wachimbaji Visima

jashmoe32

JF-Expert Member
Dec 4, 2012
1,087
423
Jamani nlikua naulizia gharama ya kuchimba visima na je uchimbaji ukoje?wanabase na mita au na gharama zikoje?
 
Wanatofautiana. Kwa meter moja shs 50,000.
Kwa maeneo kam Dar kupata maji ya uhakika kabisa bila kuumiza ubongo piga meter 100. Hivyo andaa miliono 5 +.
Lakini hata meter 80 itakutoa pia, na hapa andaa milion 4 +
Sina uhakika hapa kama vifaa kama pump na waya ni vya kwako kununa lakini haya nayo ni makubaliano.

Ukitaka uende super kabisa, uwaite watu wa kukupimia na kutafuta kajieneo gani kana mwaga maji zaidi hapo eneoni kwako. Kufanya hivi unaweza ukajikuta unashauriwa kuchimba sehem fulani meter chache tu labda hata 60 kwenda chini. Lakini mtaalamu wa kukutafutia kajisehem anataka laki nne zake.

So kazi kwako.
 
Back
Top Bottom