Wachezaji wa Yanga wamkataa Nadir Haroub (Cannavaro) kwa kuwa ni mbea na mnafiki

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,054
107,538
Wachezaji wa Yanga kwa umoja wao wameamua kumkataa Mchezaji mwenzao na ambaye pia ni Nahodha wa Klabu hiyo Nadir Haroub ' Cannavaro ' kwa madai kuwa amezidi na kukithiri kwa Umbea na kuwagawa Wachezaji.

Wachezaji hao wameenda mbali zaidi na kusema kuwa Mchezaji huyo Nadir Haroub ' Cannavaro ' amekuwa ni mpika majungu, mbea, mnafiki na mpelelezi wa Uongozi wa Yanga kitu ambacho amekuwa kila mara akipeleka maneno kwa Uongozi dhidi ya Wachezaji wa Yanga.

Wakizungumza na Mimi GENTAMYCINE asubuhi hii hii hapa maeneo ya Leaders Club ambapo sisi Wachezaji wa zamani huwa tunacheza Kiveterani zaidi kila Jumamosi na Jumapili na hawa Wachezaji huja kupata mawaidha yetu Wachezaji wapatao watano ( 5 ) ila kwa kutowaharibia huko Klabuni kwao sitowataja majina yao walikuwa wakizungumza na Mimi huku wakiwa wamefura ( kukasirika ) kabisa juu ya Vitendo vya Kinafiki vya Nahodha wao Cannavaro.

Wamesema kuwa tayari wameshakubaliana na wenzao wote kuwa kuanzia sasa hawamtaki huyo Mchezaji na kwamba hawatampa ushirikiano wowote ule na kuutaka Uongozi wa Yanga kama wameamua kuwawekea Mpelelezi basi ni vyema huyu Cannavaro awe anawekwa pale Magetini Uwanja wa Uhuru ili awe Mpelelezi kwa Viongozi wa Yanga ambao huwa wanapiga Hela za Viingilio na kwamba wakiendelea kumwacha awe nao kile walichomfanyia jana pale Uwanja wa Uhuru baada ya kumalizika kwa ile mechi dhidi ya African Lyon basi watamfanyia kitu mbaya zaidi na kwamba wamemchoka.

Ikumbukwe kuwa hii tabia ya Vilabu hivi viwili vya Simba na Yanga kumchagua Mchezaji mmoja kuwa Mpelelezi kwa wenzake haijaanza tu leo kwani huko nyuma Mchezaji na Kipa wa Simba Kelvin Mhagama nae alishawahi kupigwa mno na Wachezaji wa Simba akina Madaraka Selemani na Fikiri Magosso kwa tabia kama hizi anazofanya leo Nadir Haroub ' Cannavaro ' na kama haitoshi japo inafichwa fichwa hata Meneja wa sasa wa Simba Sports Club Mussa Hassan ' Mgosi ' hapendwi na Wachezaji wa Simba kwakuwa na yeye ni Mpelelezi wa Uongozi wa Simba kwani hata alipokuwa Mchezaji mwandamizi wa Simba alikuwa na tabia ya kuwapeleleza wenzake na kuwachoma kwa Uongozi na moja ya sababu kubwa ya kupewa Umeneja wa Klabu ya Simba ni baada ya kuwa mbea aliyetukuka kwa Vitendo vya Wachezaji wenzake.

Naomba kuwasilisha.
 
Figisu tu! Watanzania badala ya kucheza mpira tunakuwa na vijisababu vya ovyo.kupelelezwa ni jambo mhimu maana wapo wanaohujumu timu.
 
Kwani waliompiga jana ni wachezaji au mashabiki

Jana kapigwa na Simon Msuva halafu wakiwa ndani Deus Kaseke nae akamtukana na ilibidi Mohamed Binda aingilie kati kuwatuliza Vijana wake. Na kama hiyo haitoshi kwakuwa umechokoza na sasa nakupa NYETI nyingine ni kwamba jana hiyo hiyo pia Kocha wa Yanga Lwandamina aligombana na hadi kurushiana maneno ya Kocha wa Makipa wa Yanga Juma Pondamali ' Mensah ' kwakuwa Kocha alichukizwa sana goli alilofungwa Deogratius Munishi ' Dida ' na kwamba Kocha anavutiwa sana na Kipa Ben Kakolanyi na Ally Mustafa ' Barthez ' ila Kocha huyo wa Makipa wa Yanga Pondamali ana BIFU lisiloisha na Ally Mustafa ' Barthez '. Nimalizie tu kwa kukuambia muda wowote Kocha wa Makipa wa Yanga Juma Pondamali ' Mensah ' anafungashiwa virago vyake kwani Lwandamina amechukizwa nae kwa mabishano yao ya jana.
 
Jana kapigwa na Simon Msuva halafu wakiwa ndani Deus Kaseke nae akamtukana na ilibidi Mohamed Binda aingilie kati kuwatuliza Vijana wake. Na kama hiyo haitoshi kwakuwa umechokoza na sasa nakupa NYETI nyingine ni kwamba jana hiyo hiyo pia Kocha wa Yanga Lwandamina aligombana na hadi kurushiana maneno ya Kocha wa Makipa wa Yanga Juma Pondamali ' Mensah ' kwakuwa Kocha alichukizwa sana goli alilofungwa Deogratius Munishi ' Dida ' na kwamba Kocha anavutiwa sana na Kipa Ben Kakolanyi na Ally Mustafa ' Barthez ' ila Kocha huyo wa Makipa wa Yanga Pondamali ana BIFU lisiloisha na Ally Mustafa ' Barthez '. Nimalizie tu kwa kukuambia muda wowote Kocha wa Makipa wa Yanga Juma Pondamali ' Mensah ' anafungashiwa virago vyake kwani Lwandamina amechukizwa nae kwa mabishano yao ya jana.
lile goli nila kipa au Mabeki walifanya makosa
 
Kweli simba mmejizatiti kama chama cha kijani kwa propaganda jana nilikuwepo mwanzo hadi mwisho wa vurumai la mashabiki na wachezaji hakuna mchezaji aliopigwa nimeshuhudia mpaka wachezaji wanaingia vyumbani hakuna hata alioguswa na kidole zaidi ya kurushiwa maneno machafu na mashabiki
 
Wachezaji wa Yanga kwa umoja wao wameamua kumkataa Mchezaji mwenzao na ambaye pia ni Nahodha wa Klabu hiyo Nadir Haroub ' Cannavaro ' kwa madai kuwa amezidi na kukithiri kwa Umbea na kuwagawa Wachezaji.

Wachezaji hao wameenda mbali zaidi na kusema kuwa Mchezaji huyo Nadir Haroub ' Cannavaro ' amekuwa ni mpika majungu, mbea, mnafiki na mpelelezi wa Uongozi wa Yanga kitu ambacho amekuwa kila mara akipeleka maneno kwa Uongozi dhidi ya Wachezaji wa Yanga.

Wakizungumza na Mimi GENTAMYCINE asubuhi hii hii hapa maeneo ya Leaders Club ambapo sisi Wachezaji wa zamani huwa tunacheza Kiveterani zaidi kila Jumamosi na Jumapili na hawa Wachezaji huja kupata mawaidha yetu Wachezaji wapatao watano ( 5 ) ila kwa kutowaharibia huko Klabuni kwao sitowataja majina yao walikuwa wakizungumza na Mimi huku wakiwa wamefura ( kukasirika ) kabisa juu ya Vitendo vya Kinafiki vya Nahodha wao Cannavaro.

Wamesema kuwa tayari wameshakubaliana na wenzao wote kuwa kuanzia sasa hawamtaki huyo Mchezaji na kwamba hawatampa ushirikiano wowote ule na kuutaka Uongozi wa Yanga kama wameamua kuwawekea Mpelelezi basi ni vyema huyu Cannavaro awe anawekwa pale Magetini Uwanja wa Uhuru ili awe Mpelelezi kwa Viongozi wa Yanga ambao huwa wanapiga Hela za Viingilio na kwamba wakiendelea kumwacha awe nao kile walichomfanyia jana pale Uwanja wa Uhuru baada ya kumalizika kwa ile mechi dhidi ya African Lyon basi watamfanyia kitu mbaya zaidi na kwamba wamemchoka.

Ikumbukwe kuwa hii tabia ya Vilabu hivi viwili vya Simba na Yanga kumchagua Mchezaji mmoja kuwa Mpelelezi kwa wenzake haijaanza tu leo kwani huko nyuma Mchezaji na Kipa wa Simba Kelvin Mhagama nae alishawahi kupigwa mno na Wachezaji wa Simba akina Madaraka Selemani na Fikiri Magosso kwa tabia kama hizi anazofanya leo Nadir Haroub ' Cannavaro ' na kama haitoshi japo inafichwa fichwa hata Meneja wa sasa wa Simba Sports Club Mussa Hassan ' Mgosi ' hapendwi na Wachezaji wa Simba kwakuwa na yeye ni Mpelelezi wa Uongozi wa Simba kwani hata alipokuwa Mchezaji mwandamizi wa Simba alikuwa na tabia ya kuwapeleleza wenzake na kuwachoma kwa Uongozi na moja ya sababu kubwa ya kupewa Umeneja wa Klabu ya Simba ni baada ya kuwa mbea aliyetukuka kwa Vitendo vya Wachezaji wenzake.

Naomba kuwasilisha.
Ww jamaa fala sana
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom