kimbendengu
JF-Expert Member
- Jun 7, 2013
- 6,079
- 10,386
DUNIANI KOTE MPIRA NI BIASHARA HAYA WEWE AKILIMALI LETE MAJINI YAKO TULIPE MSHAHARA
Shauri zao si ajira zao, wapuuzi!WAMUONYESHA LWANDAMINA NGUVU YAO
Kocha George Lwandamina alipigwa na bumbuazi leo asubuhi baada ya wachezaji wake kugoma kuingia na kufanya mazoezi.
Wachezaji wa Yanga hawakufanya mazoezi kwa kuwa inaelezwa wanadai mishahara yao ya mwezi Novemba.
Mara baada ya wachezaji kutua kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam, walishindwa kuanza mazoezi.
Baada ya uchunguzi, iligundulika kwamba wachezaji hao walitaka kulipwa mishahara yao ya Novemba.
“Wachezaji hawajalipwa mishahara yao ya Novemba, hawataki kufanya mazoezi na kocha ameshindwa la kufanya,” alisema mmoja wa viongozi waliokuwa eneo hilo akithibitisha hilo na kusisitiza yeye si msemaji.
Juhudi za kumpata Katibu Mkuu, Barala Deusdedit ziligonga mwamba, kama ada simu yake huita bila ya kupokelewa hata pale anapotumiwa ujumbe kuelezwa kusaidia kutoa ufafanuzi wa jambo, huwa hajibu.
Wachezaji Yanga wamefanya hivyo ikiwa ni siku moja tokea waanze Ligi Kuu Bara hatua ya mzunguko wa pili kwa kishindo wakiitwanga JKT Ruvu kwa mabao 3-0.
Ha ha ha... Bwihi..! Bwihi..!Mechi yao na Simba ni lini? Wangeweza kupigwa 10 O'clock
Mind game?Ndio nini?Wacha kuchezea lugha za watu.Mind game
Mmemlipa lini yule mama hadi Leo anawalani kwa pesa yake ya chapatu kama familia ya marehemu Mafisango pesa ya rambirambi na ndio maana amfanikiwi kwa kudhurumu watuTumeshamlipa. Umeshakwenda kupiga magoti.? Wenzako wameshakusanyika klabu unangojewa wewe tu.Mazoezi ya kupiga magoti karibu yataanza. Mzee Rashid Matunda alichangangisha maharage na unga wachezaji wale. Sijui safari hii mtachangisha nini?Bora mpige magoti.
Mimi ni Simba lakini kwa hili nashauri Yanga wavamie kwa Akilimali wakidai awalipe wachezaji ili liwe funzo kwa watu kama Kilomoni. Mi najua Manji kafanya makusudi ili Yanga wajue umuhimu wakeDUNIANI KOTE MPIRA NI BIASHARA HAYA WEWE AKILIMALI LETE MAJINI YAKO TULIPE MSHAHARA
Jifunze kuandika kiswahilieml
Mmemlipa lini yule mama hadi Leo anawalani kwa pesa yake ya chapatu kama familia ya marehemu Mafisango pesa ya rambirambi na ndio maana amfanikiwi kwa kudhurumu watu
Heri yako wewe mswahili ila nashangaa mswahili gani anaipenda Simba au ulikuwa mfanyakazi wa Ramesh PatelJifunze kuandika kiswahili
Chapatu
Anawalani
Kudhurumu
Halafu rudi ujaribu tena kuandika unachokusudia. Sio wote wanaelewa kilugha.
Huyo mnayempigia magoti kwani ni mkurya?Si ndio hao hao kina Ramesh Patel?Au naye anaipenda Simba???Heri yako wewe mswahili ila nashangaa mswahili gani anaipenda Simba au ulikuwa mfanyakazi wa Ramesh Patel