Lituye
JF-Expert Member
- Dec 27, 2015
- 1,862
- 5,679
Ni hivi karibuni tuliona tamko lenu mkiwatisha wagombea kuwa Mtu atakaye mpinga mgombea mnaye muunga ninyi mkono mtu huyo atakiona cha mtema kuni. Uzuri matamko yenu mliyatoa hadharani kabisa na tena mchana kweupee bila ya hofu mara mbili. Hii ina maana matendo yenu ninyi wachawi na mliye muunga mkono yalikuwa yana fanana kwa kuwa ndege wa aina moja huruka pamoja.
Sasa tunawaulizeni Maswali yupo wapi yule mliye muunga mkono na kuwatisha watu wengine? Mlifikiri Mungu anatishwa na wanadamu? Yaani sisi wacha Mungu na wenye akili tuwepo hai halafu niyi wachawi na vigagula ndio mtuchagulie kiongozi? Yaani wachawi na vigagula mlifikia hatua hii kweli kujiona sasa na ninyi mnatawala. Hakika Mungu ni Mkuu na matendo yake yanatisha kama nini.
Mungu hadhihakiwi chochote apandacho MTU ndicho atakacho vuna.Hata mfalme Daud alipo mpora mke wa askari wake Mungu hakumuacha alimpiga sembuse Mchawi tuu atishe watu? Mungu hapendi uonevu anataka haki wachawi muwe mnaelewa. Wanasiasa mtegemeeni Mungu.
Kazi ziendelee.
Sasa tunawaulizeni Maswali yupo wapi yule mliye muunga mkono na kuwatisha watu wengine? Mlifikiri Mungu anatishwa na wanadamu? Yaani sisi wacha Mungu na wenye akili tuwepo hai halafu niyi wachawi na vigagula ndio mtuchagulie kiongozi? Yaani wachawi na vigagula mlifikia hatua hii kweli kujiona sasa na ninyi mnatawala. Hakika Mungu ni Mkuu na matendo yake yanatisha kama nini.
Mungu hadhihakiwi chochote apandacho MTU ndicho atakacho vuna.Hata mfalme Daud alipo mpora mke wa askari wake Mungu hakumuacha alimpiga sembuse Mchawi tuu atishe watu? Mungu hapendi uonevu anataka haki wachawi muwe mnaelewa. Wanasiasa mtegemeeni Mungu.
Kazi ziendelee.