samstevie
JF-Expert Member
- Nov 11, 2011
- 202
- 31
Kidumu chama cha Mapinduzi.
Ndugu Makada wenzangu, kama mjuavyo siku zinazidi kupepea na mwaka 2015 ndio huo unatunyemelea kwa kwasi.
Hali ya kisiasa ndani ya nchi yetu ni shwari licha ya changamoto za hapa na pale tunazokumbana nazo, mathalan kutokana na udhaifu wa baadhi ya wadau tuliowapa jukumu la kuendesha serikali.
Nadhani imefika wakati tuanze KUANDAA mazingira mazuri ya atakayepokea kijiti cha Urais 2015. Hii haimaanishi kwamba kuacha kuwatumikia wananchi na kutekeleza ilani ya chama la hasha, ni sehemu ya mchakato.
Kwa maoni yangu nadhani hakuna mtu tunayepaswa kumuachia kijiti zaidi Lowassa. Nchi yetu inahitaji mtendaji atakayesukuma gurudumu kwa ustadi na kasi pasipo kuhatarisha umoja wetu. Nadhani tumfariji na kumpa ushirikiano ktk kipindi hiki kigumu anachopitia ili kuitimiza azma hii.
Wenu,
Kada.
Mimi CUF naona hujatuwekea objection pengine unaogopa sana CHADEMA lakini nakushauri uwaombe mods wawawekee jukwaa lenu tu wanaCCM aka magamba ful mafisadi. Hivi aliyekudanganya CCM wapo JF ni nani watu wenyewe wote wazee hawajui hata Computer ni nini kawatafute huko Nanjilinji, Liwale na Masasi amabako nako kushaingiliwa sijui mtakimbilia wapi. Mwaka huo mbona hamna mtu wa kumimamisha kukabiliana na presha ya wapinzani?