Naomba kufahamishwa kuhusu kanblia la Waburunge

mjasiria

JF-Expert Member
Jan 10, 2011
4,156
1,849
Habari wana MMU,

leo nina maswali kidogo kuhusu hili kabila la waburunge. Kwanza kabisa naomba ieleweke kuwa ninauliza maswali haya kwa sababu sikuwahi kujua kuwa kuna kabila linakwenda kwa jina hili hadi hapo jana.

Ni kwamba katika pitapita zangu nimekutana na binti mmoja mrembo sana, sasa katika kuzungumza ikafikia mahali akanijulisha kuwa yeye ni Mburunge na kwa mujibu wa maelezo yake hii kabila inapatikana Manyara. Sasa basi ninaomba kwa wale wenye habari kuhusu hii kabila watusaidie mwanga zaidi hapa hususani katika eneo la mahusiano.

Maswali yangu ni kama ifuatavyo:
  1. Je, tamaduni zao zikoje kwenye suala la mahusiano?
  2. Je, wanafanya tohara kwa wanawake? Na pia wana kitu chochote kinachofanana na jando?
  3. Najua kila mmoja ana tabia zake lakini kuna zile tabia za jumla zinazotokana na tamaduni na malezi yanayopatikana katika kabila fulani. Naomba kujua ni zipi tabia za kabila hili hususani katika mahusiano.
Angalizo:
Najua kuna watu mtasema muulize mwenyewe. Kifupi ni kwamba nimeshamuuliza lakini nimeona niulize na humu maana huenda kuna watu wana habari muhimu na sahihi kuhusu waburunge kuliko hata huyu msichana.

Haya jamani uwanja ni wenu.
 
Haya sasa,...yaani siku hizi MMU imekumbwa na kiwewe cha ukabila,...anyway ngoja waje wale wajuvi mkuu!
Mkuu IGWE wewe ni mmoja wa wanachama ninaowakubali sana hapa MMU. Hebu lipitie tena bandiko langu utaelewa mantiki ya ninachoulizia
 
Mhhhhhhhhhhhh! jamani kama waburunge mpo si mtuambietu, au ndo mnataka muoaji ajifunze hayo baada ya kuoa. Msaidieni ili ndoa yake iwe na furaha, jamani waburunge jitupeni jamvini mpate shemeji. Mbona yule mmaasai alituambie mengi juu ya ngoma yao ya essoto!!!
 
'Ngono inapendwa sana lakini inaogopwa kuongelewa waziwazi'
 
Sidhani kama wanapatkana manyara nijuavyo mimi wanapatkana kwa wingi wilaya kondoa mkoa wa Dom, wanashahibiana sana na warangi kwa muonekano na tabia na hata wengi wao hupendelea kuzungumza kirangi na hata kujtambulisha kwamba ni warangi.
 
Habari wana MMU,

leo nina maswali kidogo kuhusu hili kabila la waburunge. Kwanza kabisa naomba ieleweke kuwa ninauliza maswali haya kwa sababu sikuwahi kujua kuwa kuna kabila linakwenda kwa jina hili hadi hapo jana.

Ni kwamba katika pitapita zangu nimekutana na binti mmoja mrembo sana, sasa katika kuzungumza ikafikia mahali akanijulisha kuwa yeye ni Mburunge na kwa mujibu wa maelezo yake hii kabila inapatikana Manyara. Sasa basi ninaomba kwa wale wenye habari kuhusu hii kabila watusaidie mwanga zaidi hapa hususani katika eneo la mahusiano.

Maswali yangu ni kama ifuatavyo:
  1. Je, tamaduni zao zikoje kwenye suala la mahusiano?
  2. Je, wanafanya tohara kwa wanawake? Na pia wana kitu chochote kinachofanana na jando?
  3. Najua kila mmoja ana tabia zake lakini kuna zile tabia za jumla zinazotokana na tamaduni na malezi yanayopatikana katika kabila fulani. Naomba kujua ni zipi tabia za kabila hili hususani katika mahusiano.
Angalizo:
Najua kuna watu mtasema muulize mwenyewe. Kifupi ni kwamba nimeshamuuliza lakini nimeona niulize na humu maana huenda kuna watu wana habari muhimu na sahihi kuhusu waburunge kuliko hata huyu msichana.

Haya jamani uwanja ni wenu.
kwa ninyo jua kidogo kuhusu hao watu, (maana nimeishi nao kidogo mkoani dodoma)

kigeographia
wanapatikana mkoa wa dodoma, wilaya ya chemba ambapo zamani chemba ilikuwa sehemu ya wilaya ya kondoa

lugha
lugha yao ni kiburunge, inafanana na kiiraki kidogo, kwahiyo muiraki akiongea mburunge anamuelewa kidogo

dini
katika imani, waburunge kwa asilimia fulani ni wakristo wa dhehebu la aglican, kwa dini ya uislam ni wachache sana! pia asilimia kubwa wanaamini katika mila na desturi zao,

kwenye mahusiano
katika tamaduni za kiburunge mwanamke bado anaweza pendekezewa mwanaume wa kumuoa

kitabia
hapa kutokana na maisha niliyo ishi nao, wengi wao nimeona ni waaminifu katika mahusiano na pia wanamsimamo na wanajitunza sana, lakini nilikutana na mmoja tu nikiwa jiji flani nnje na dodoma lakini, alikua hajatulia lakini sio konkodi ile ya kawaida tu ambao mtu akiamua kumrekebisha anarekebishika na nilivyo mchunguza aliisha sana uswazi maeneo kama mwana nyamala na magomeni
 
Back
Top Bottom