Wabunge wote wa CCM wameitwa dharura kikao cha DOWANS kesho

TAARIFA KWA WABUNGE WA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA


Ofisi ya Bunge inapenda kuwatangazia Waheshimiwa Wabunge wote kuwa kutakuwa na mafunzo ya awali (Orientation Course) yatakayotolewa kwao kuanzia tarehe 25 Januari, 2011 mpaka tarehe 3 Februari, 2011.
Mafunzo hayo yatatanguliwa na vikao rasmi vya Vyama vya Siasa kikiwemo CCM ambacho kitakuwa na semina kuanzia tarehe 22 – 24 Januari, 2011. Kikao cha Wabunge wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kitafanyika katika Ukumbi wa Ubungo Plaza, Dar es Salaam.
Kwa taarifa hii, Waheshimiwa Wabunge wanaombwa kuwasili Dar es Salaam kwa kuzingatia tarehe ya vikao hivyo vya mafunzo.
Eliakim P. M. Mrema
KAIMU KATIBU WA BUNGE
 
Mmmh! Haka ka-Nchi kananuka rushwa. 2005 India wakaleta magari kwa sisi "M", wananchi tukafaidi mkataba bomu wa RITES na kupanda kwa gharama karibu zote kwa asilimia 200 hadi 500. 2010 tukaona helkopta tatu za hicho chama zikipishana angani kama maonyesho ya vita na suzuki tele kwa watendaji wake; wananchi tunachomekewa malipo ya "Do-Once" na ongezeko la umeme na kupanda kwa gharama mbalimbali. Natamani kufa! Mnisamehe jamani ni hasira tu.

Usife kifo cha mwoga, kufa na wachache utabaki shujaa na wakukumbukwa.
Ndiyo maana ya ushindi lazima na kulazimisha wakurugenzi na madc wawapitihe wana sisiemu.
Tuchukue hatua gani sasa? Hire a sniper?
 
Wanapewa vitisho vya hali ya juu hawa ikiwemo kufukuzwa chamani na hivyo kupoteza ubunge. Msiseme chochote katika kikao kinachokuja cha Bunge kupinga malipo ya $69 million kwa DOWANS au malipo ya $87 million kwa RITES, ole wake atakayejaribu kusema lolote ili kupinga malipo hayo. Ndiyo Tanzania yetu hiyo inavyoliwa na mafisadi.
 
Mbunge yeyote atakayekubaliana na huo upuuzi hasiruhusiwe kurudi jimboni. Hatuwezi kukubali kufanywa kama MAZOBA. Tumechoka.
 
Natamani mkusanyiko wao huo upigwe na radi!!Sidhani kama kuna atakaethubutu kupinga watakachoelezwa hata kama hasupport hayo malipo!!Tuombe tu Mungu awasaidie Wapinzani wao kuwawashia moto utakao wafanya angalau waogope kulipa kirahisi kwa kuogopa kitakachotokea wakifanya hivyo!
 
My Prodigal Son me your father am with you that is why you are wise.

You have made me understand it is a normal bunge anouncement that "MPs for all political Parties have time to meet before the Bunge session"

If CCM will discuss Dowans other parties can discuss dowans also. If they come up with crap undermining our national interests we will have been equiped with ammunition to put them to task.

Thank you Prodigal Son. I your father was also a Prodigal Son keep it up and i am still one in this country which has never known a "father"
 
Hili ndiyo tatizo la kuwa na serikali ya kununuliwa. JK sasa hivi anasukumwa tu kwa manufaa ya genge la watu wachache akiwemo yeye na mkewe. Kinara wa hili genge ni mbunge lakini anamwendesha Prezidaa anashindwa kusimamia kile alichoapa kwenye katiba. Pamoja na kwamba Katiba yetu ni mbovu lakini bado inamtaka JK kulinda maslahi ya Taifa, na hii DOWANS si maslahi ya nchi hata kwa nusu sekunde.
 
Ni mbunge mjinga na mpumbavu tu ndiye anayeweza kuunga mkono uamuzi wa serikali kuilipa dowans na kusababisha mateso kwa wapiga kura wake.
 
Hivi hakuna njia ya kumfukuza mbunge baada ya kumchagua?? Wajuzi wa katiba tusaidieni.................... Nafikiri some of these MPs have to be recalled.

Hiyo mdogo wangu imekula kwetu tusubiri mpaka 2015 au labda kama ataitwa mbele ya haki au kushindwa katika kesi ya uchaguzi itakayofunguliwa mahakamani. Katiba yetu haina kipengele kinachoturuhusu sisi wananchi kumvua madaraka Mbunge akishachaguliwa.
 
Habari za kuaminika sasa hivi wabunge wote wa CCM wameitwa Dodoma kuandaa na kuweka mkakati wa pamoja juu ya Dowans. Nia ni kuzibwa midomo na imetamkwa kwamba DOWANS ina masilahi gani na kila jimbo la mbunge.

BARAZA la mawaziri limeazimia hakuna kujadili suala hilo.

Taarifa hizi nimepata toka kwa mmoja wa wabunge akiwa anajiandaa kuelekea DODOMA.

Wameitwa na nani? i think bunge linakaribia kuanza sidhani ni issue ya Dowans, maana
it is impossible to pay this lump sum of money, its repercussions will possibly lead to
impeachment of JK, hii ni hatari mno, kila mtu anajua, na ujue wabunge hata wa
CCM hawakubali kulipa, mmmhh hivi walikuwa wanatumia Chopa 3 eehh, like millitary
air show
 
Wameitwa na nani? i think bunge linakaribia kuanza sidhani ni issue ya Dowans, maana
it is impossible to pay this lump sum of money, its repercussions will possibly lead to
impeachment of JK, hii ni hatari mno, kila mtu anajua, na ujue wabunge hata wa
CCM hawakubali kulipa, mmmhh hivi walikuwa wanatumia Chopa 3 eehh, like millitary
air show

Katibu wa bunge ametangaza kuatakuwa na semina ya wabunge wa ccm siku 3 kabla
 
Habari za kuaminika sasa hivi wabunge wote wa CCM wameitwa Dodoma kuandaa na kuweka mkakati wa pamoja juu ya Dowans. Nia ni kuzibwa midomo na imetamkwa kwamba DOWANS ina masilahi gani na kila jimbo la mbunge.

BARAZA la mawaziri limeazimia hakuna kujadili suala hilo.

Taarifa hizi nimepata toka kwa mmoja wa wabunge akiwa anajiandaa kuelekea DODOMA.

Mambo mazito sana hayo. Tunaomba atakayepata update atujuze tafadhali.
 
Ndio watakuwa wanapalilia vizuri njia ya kupoteza majimbo zaidi 2015. Ili CCM ianguke vizuri lazima iendelee kufanya madudu. Sikio la kufa huwa halisikii dawa. Labda Mungu anataka kutukomboa watanzania ndio maana kawapa CCM upofu na uziwi ili wananchi wengi wafumbuke macho na kuamka. Ninaamini Ukombozi hauko mbali.
 
Kwa kweli inatishaaa!! Ila naamini kati yao kutakuwemo na wacha MUNGU! Wabunge wetu wapendwa msikubali kuendeshwa kama bodabodaa!! Tambueni kuwa nanyi mnapaswa kusikilizwa na hao wanaowaiteni!katu msiendeshwe jaribun kutambua thamani yenu vinginevyo mtaonekana TABULA LASA na waliowachagueni!!


Maaskofu wenyewe wanashiriki UUaji wizi na uzinzi sembuse wabunge??
Tunamtaja Mungu tunasahau jambo moja kwamba Mimi na wewe ni Miungu vile vile tunalitaka hapa Duniani ndilo linalotendeka.
Tatuzo kubwa tulilolivaa kama joho ni kuwaacha Wendawazimu na washenzi kutoa maamuzi kwa niaba yetu na kuyatekeleza kwa niaba yetu.
Huu ndiyo wakati sahihi wa kusema basi, kila siku tunajidanganya kwa kusema wakati sahihi ni ule karibu ya uchaguzi.
Huu ni wakati sahihi Mwizi ni lazima aitwe mwizi na ikibidi sheria ichukuliwe mikononi mwetu.
 
Nshakasirika sijui kama mechi ya leo uck ya washika bnduki ntaiangalia manake hiki chama kishanivurugia mood!
 
Waacheni wafanye wanayotaka lakini wakumbuke hata kule Tunisia ilianza hivi hivi mwisho wananchi wakachoka wakingia mitaani polisi wakawapiga weeee wakashindwa Wakamtoa rais madarakani kama vile haikutosha wakaingia tena kukitoa cha Tawala. Sasa nyie CCM hamjajifunza tu kutoka Tunisia kuwa umma ukichoka huwa hakuna suluhu? Wanasema ni rahisi kuwadanganya watu wote lakini huwezi kuwadanganya siku zote.
 
Ndege wa rangi moja huruka pamoja, ni vema tujiulize je tunafanana rangi na hawa viongozi tunaowachagua? Binafsi nadhani hawa si wenzetu ila wapo kwa ajili ya matumbo yao na hao wapendwa wao wachache,
Ni werevu sana kwa kuficha kutu za rushwa kwenye nyuso zao kipindi cha uchaguzi, na pindi tunaposhinda ndio wanaanza kuonyesha rangi zao,,,
Huwa binafsi naamini muda ni mwamuzi mzuri na siku zote huleta matokeo fulani, wanatufanya wapumbavu tusioweza chukua hatua yoyote dhiti yao, wanatumaia udhaifu wetu wa kutojua sheria kutudhulumu haki zeti haya yote ni tisa, kumi tunataka wajue sasa tumeamka na kamwe hawatatufanya punda wakubeba mizigo yao mizito kwa manufaa yao binafsi!
Acha waende kujadili ufisadi wao, ila ipo siku tena si mbali tutaingia mitaani kupinga waziwazi. Nawachukia mafisadi kama kulamba kinyesi
 
Back
Top Bottom