Wabunge wetu wanatia aibu sana!! Kigezo cha elimu za wabunge sasa uwe ni mjadala mwafaka

Fumadilu Kalimanzila

JF-Expert Member
Dec 10, 2016
1,651
5,122
Jana ungetazama jinsi wabunge wetu walivyokuwa wakishangilia Bajeti ilipokuwa ikisomwa ungesikitika sana hasa kama una "akili kidogo"!

Watu hamjakaa mkatafakari bajeti lakini kusikia tu hiki kimefutwa basi pwaaa pwaaaa na kujitoa ufahamu kabisa! Hamjui wasomi wanapoandaa Bajeti wanakupa hiki kwa mkono wa kulia na kukunyang'anya kwa mkono wa kushoto!

Mimi ni MwanaCCM lakini wabunge wetu wengi ni "Mizigo" na watia aibu sana! Wengi wao ni upupu tu hawana muda wa kuchambua mambo!

"Haya ndo Mabunge" ambayo yanapitisha sheria zinazoruhusu Wawekezaji kusafirisha Mchanga wenye madini kwa kasi ya Mwanga(Speed of light),kesho yake Rais akizuia kusafirisha Mchanga wa Madini ndiyo tena yanakuwa ya kwanza kumpongeza Rais eti ni Shujaa na Mzalendo! Vichwa vya Mbuzi kabisa!

Ebu sasa tupigieni Hesabu kwa kodi ya magari iliyofutwa na kupelekwa kwenye mafuta kwa Mwaka mwenye Gari atalipa kiasi gani na athari zingine za kiuchumi kwa kupanda kwa bei ya mafuta itakuwaje! hasa gharama za uzalishaji na usafirishaji!

Tunajua kwa sasa kazi iliyo ngumu kabisa katika Taifa hili ambayo inafanywa na watu wachache sana ni KUFIKIRI! Hata wasomi wetu walishaacha kufikiri kitambo! Eti juzi Rais kuwakejeli Wachumi wetu kwa kutofikiri vizuri kuhusu vyanzo vipya vya mapato,Eti wamachinga,mamalishe wapewe vitambulisho kwa Tshs.10,000/= na wao eti wameweka kwenye BAJETI! Hawa ni WASOMI Uchwara kabisa! Mnachukua 4% kama mrabaha kwenye Madini yetu halafu mnakuja kukimbizana na MAMALISHE na WAMACHINGA,kweli!?

Nchi hii ina kila Kitu ila laana ambayo tulipewa ni aina ya WATU tuliopo humu Nchini,Naomba tufanyiwe tafiti kuhusu "Bongo"zetu! Isijekuwa tuliwekewa Bongo za Wanyama wengine na si binadamu! Kama sivyo kwanini Watanzania sisi ni WABABAISHAJI katika kila kitu !? Kwenye Michezo,Uchumi,Siasa,Elimu ni UBABAISHAJI MTUPU!

Wabunge wa S.T.D 7 (kusoma na Kuandika na siyo hata kuhesabu) kwa sasa hawana TIJA!
 
Siyo bungeni bunge lala,tumeweka mpaka wanamuziki,waandishi wa habari,hawana jipya kwenye bajeti hii,kwani ni wote wenye vyombo vya moto?vitu vinapanda bei sisi tunapiga makofi,makampuni yanastemp watu,siasa kila mahali,nawashangaa kwa kweli.
 
Ni ukweli mtupu sisi ni nyumbu tulisha laaniwa kabisa tunakila kitu lakini ndio masikini wa kutupwa yaani hoehae
 
  • Wa kwanza akasema "...mbona mwatukanyaga kama majani?" akachomwa mkuki akafa
  • Wa pili akasema"...kwanini umesema kwasauti kuwa wanakukanyaga kama majani?" naye akachomwa mkuki akafa
  • Wa tatu aliyejificha sehemu salama zaidi akasema kwasauti "...heri mimi sijasema" naye akachomwa mkuki akafa
 
Hayo ndiyo madhara ya kufanya qualification pekee ya kuwa Mbunge wa Tanzania ni ONLY kujua kusoma na kuandika!

Hivi sasa wabunge wa CCM wakiongozwa na 'bingwa' wao wa kuporomosha matusi bungeni Kibajaj wanaendeleza propaganda ya 'kitoto' kabisa kuwa eti wabunge wa upinzani ndiye wanaowakingia kifua wezi wa madini yetu!

Wakati kila mwananchi hapa nchini anajua kuwa wabunge wa upinzani kwa kipindi cha miaka 20 iliyopita wamekuwa wakipigia kelele kwa nguvu zote kuhusu wawekezaji wa kigeni wa uchimbaji madini ya dhahabu kuwa wanatuibia, lakini kutokana na uchache wao bungeni hoja yao hiyo imekuwa ikipuuzwa na wabunge walio wengi ambao ni wa CCM.

Nini kilichotokea?

Wabunge wa CCM kwa kutumia wingi wao Bungeni ndiyo ambao wamepitisha miswada bungeni kwa NDIYOO zao za nguvu humo bungeni ambapo hivi sasa ndiyo Mwenyekiti wao Magufuli anawastua kuwa tumeibiwa kwa kipindi kirefu sana!

Kweli imenenwa ukistaajabu ya Musa utayaona ya Firauni.........

Wabunge wale wale ambao kwa miaka zaidi ya 20 wamekuwa wakiwazomea na kuwakejeli wabunge wa upinzani walioikuwa wanaongea kwa uchungu kuhusu makampuni ya kigeni yanavyoliibia Taifa na kuwaita wabunge hao wazushi......

Leo hii 'wamegeuka' na kubadili gia angani na kumuita Rais wao shujaa kwa kuyatamka yale yale yaliyotamkwa mfululizo kwa miaka 20 iliyopita na wabunge wa upinzani kuwa makampuni ya madini ya kigeni yanatuibia!

Nadhani itakuwa vyema ukafanyika utaratibu wa kuwapima akili hawa wabunge wetu wa Sisiem ili tujue kama kweli bongo zao hazina mushkeli kweli?
 
Hayo ndiyo madhara ya kufanya qualification pekee ya kuwa Mbunge wa Tanzania ni ONLY kujua kusoma na kuandika!

Hivi sasa wabunge wa CCM wakiongozwa na 'bingwa' wao wa kuporomosha matusi bungeni Kibajaj wanaendeleza propaganda ya 'kitoto' kabisa kuwa eti wabunge wa upinzani ndiye wanaowakingia kifua wezi wa madini yetu!

Wakati kila mwananchi hapa nchini anajua kuwa wabunge wa upinzani kwa kipindi cha miaka 20 iliyopita wamekuwa wakipigia kelele kwa nguvu zote kuhusu wawekezaji wa kigeni wa uchimbaji madini ya dhahabu kuwa wanatuibia, lakini kutokana na uchache wao bungeni hoja yao hiyo imekuwa ikipuuzwa na wabunge walio wengi ambao ni wa CCM.

Nini kilichotokea?

Wabunge wa CCM kwa kutumia wingi wao Bungeni ndiyo ambao wamepitisha miswada bungeni kwa NDIYOO zao za nguvu humo bungeni ambapo hivi sasa ndiyo Mwenyekiti wao Magufuli anawastua kuwa tumeibiwa kwa kipindi kirefu sana!

Kweli imenenwa ukistaajabu ya Musa utayaona ya Firauni.........

Wabunge wale wale ambao kwa miaka zaidi ya 20 wamekuwa wakiwazomea na kuwakejeli wabunge wa upinzani walioikuwa wanaongea kwa uchungu kuhusu makampuni ya kigeni yanavyoliibia Taifa na kuwaita wabunge hao wazushi......

Leo hii 'wamegeuka' na kubadili gia angani na kumuita Rais wao shujaa kwa kuyatamka yale yale yaliyotamkwa mfululizo kwa miaka 20 iliyopita na wabunge wa upinzani kuwa makampuni ya madini ya kigeni yanatuibia!

Nadhani itakuwa vyema ukafanyika utaratibu wa kuwapima akili hawa wabunge wetu wa Sisiem ili tujue kama kweli bongo zao hazina mushkeli kweli?
Cha ajabu huyo anaewastua kuwa tumeibiwa na kuitwa shujaa siyo mgeni bungeni, alikuwemo wakati zinapitishwa muda huo akizunguka kwenye wizara mbalimbali.

Ccm wanatuchezea akili sana eti magufuri siyo kama ccm wengine huyu kaletwa na MUNGU, pumbavu zao.
 
Hao Wabunge wa CCM wamepoteza hadhi ya kuitwa Wabunge. Waitwe wabunge kwa lipi walifanyalo? Hao hao ndiyo walisema ndiyoooooo kwenye mikataba yote ya kifisadi na ya kihuni kwa miaka miaka mingi sasa. Badala ya kuihoji Serikali kuhusu kero mbali mbali za Watanzania wamekuwa wasemaji na watetezi wa Serikali hadi kuthubutu kuchukua rushwa ya milioni 10 kila mmoja sawa na 2.7 billioni pesa za walipa kodi ili kupitisha muswaada uchwara wa kuwanyima uhuru wa habari Watanzania. Ni wahuni tu hao, mafisadi na wapokea rushwa.
 
Wazee wazima.,,!! Bongo hakuna sector iliyo hai hata moja.,, Tuuze nchi tuigawane, tuzamie sauz...!!
 
Bajeti imeweka historia yaani hadi wakanogewa, walishindwa kujizuia baada ya mengi waliyoomba miaka ya nyuma mingiiii hawakusikilizwa.

Si uliona pia wamepewa vitabu walivyobeba ili wakasome au hukuwaona? Subiri wakiwa na ya kusema au kupinga lolote kuanzia Jumatatu

Hapa kazi tu

Magufuli oyeeeee
 
Upupu wa Bunge hili unaanza na ujinga wa spika mwenyewe bwana Ndugai. Jinga hili limesikika mara kadhaa likiwaambia mazuzu wenzake huku bajeti ikisomwa kuwa "kuna haja gani ya kuendelea kuisoma bajeti hii...." Kwa uzuzu wake bajeti ni nzuri mno na imeshapita! Yaani hili jinga sana. Amejiondoa ufahamu na kutokuelewa madhara ya maneno yake hayo kama spika.
 
Bajeti imeweka historia yaani hadi wakanogewa, walishindwa kujizuia baada ya mengi waliyoomba miaka ya nyuma mingiiii hawakusikilizwa.

Si uliona pia wamepewa vitabu walivyobeba ili wakasome au hukuona?


Coco wew ni Diwani wa CCM kata gani..??
 
Ndugai ni refalii aliyeamua kushabikia timu fulani na anaenda mbali kwakushangilia akirukaruka juu pale goli linapoingia

Hivi huyu mzee jimboni kwake wanahaligani watu wake?
 
21 Reactions
Reply
Back
Top Bottom