Handsome Boy 2014
JF-Expert Member
- Jul 24, 2014
- 605
- 150
Nchi hii inahitaji viongozi wenye nia njema.
Kila Utakaesoma Hapa Naomba Umtumie Meseji Mbunge Wako Ukimweleza Wizi Huo Na Ukimtaka Apeleke Hoja Bungeni. Kulalamika Kwenye Jamiiforum Hakusaidii.
Utakuwa sio raia wewe, Bima ya Afya ya Taifa unataka data za private ili ujue ishu za masharti ya wategemezi???!!!
Wameweka Masharti Mapya Ya Hovyo Sana.1.Wategemezi Wengine Wamewatoa.Wamebakisha Wazazi Au Wakwe,nafasi Zipo Sita,fikiria Unawazai Wote 2,unawakwe Wote 2,wewe Na Mkeo Mpo 2,halafu Unawatoto 3. Maana Yake Watoto Hawana Nafasi Hapo.2.Ikitokea Huna Mke,wazazi Wala Mtoto,ila Unakaka,shangazi Aliyekusomesha Hawamtaki Umjaze Kwenye Bima Hvy Nafasi Zote 5 Zinapotea Bure Na Gharama Unazochangia Hazipungui.3.Mtoto Wako Akifikisha Miaka 18 Wanamtoa Kwenye Bima Ilihali Umri Huo Yupo Kidato Cha Nne Hajaanza Kujitegemea Hvy Utakuwa Unagharamia Matibabu Yake Na Bima Wanakata Kwa Kiwango Kilekile Cha Mwanzo Hakipungui. JAPO WENGI MMEKAA KIMYA KWA SABABU MLIOWAINGIZA KWENYE BIMA HAWATAONDOLEWA SASA SUBIRINI SK APOTEZE KITAMBULISHO CHAKE CHA BIMA NDO UTAJUA NINACHOKIZUNGUMZA HAPA JAPO UNAKIONA HAKIFAI. WABUNGE WOTE Mtusaidie, RAIS JAKAYA KIKWETE HAPA UNAHUSIKA KUTOA NENO LAKO UTUSAIDIE TUNANYONYWA HAPA.
Wapuuzi nyie, mnataka kutoa fadhila Kwa kutumia bima ya afya?
Kama unampenda huyo shangazi au mjomba si mkatie bima ya jamii.
Kisheria wanaokutegemea wewe ni Wazazi wako na watoto wako wadogo.
Mambo mengine ni kulalamika bure. Kama huna watoto au Wazazi it's tough. Mbona wengine hawana watoto lakini bado wanatoa michango ya shule?
Eti watu sita haitoshi, kama unazaa kama nguruwe, shauri yako,
Bima yenyewe unalipa ngapi mpaka utake kubeba ukoo mzima.
Mbunge atakayepiga kelele kwenye hili na yeye atakuwa mpuuzi tu.
Huo utaratibu ni dunia nzima. Mjomba au shangazi au kaka toka lini na wapi alianza kuwa dependent?
Bima ya jamii ni bei rahisi sana. Kama una uwezo wakatie hao ndugu zako.
i bet hujasoma nini maana ya insurance!!!ndege ikianza safari leo na ikapata ajali,hata kama imechangia bima ya shilingi milioni kumi kwa mwaka,italipwa(indemnity)ya shilingi hata bilioni 100 kama thamani ya ndege ni hiyo.What i am trying to say ni kuwa insurance premiums ni kiasi kidogo kidogo kinachochangiwa na wengi lakini events za loss zinatokea chache...rudi shule!!!!Wapuuzi nyie, mnataka kutoa fadhila Kwa kutumia bima ya afya?
Kama unampenda huyo shangazi au mjomba si mkatie bima ya jamii.
Kisheria wanaokutegemea wewe ni Wazazi wako na watoto wako wadogo.
Mambo mengine ni kulalamika bure. Kama huna watoto au Wazazi it's tough. Mbona wengine hawana watoto lakini bado wanatoa michango ya shule?
Eti watu sita haitoshi, kama unazaa kama nguruwe, shauri yako,
Bima yenyewe unalipa ngapi mpaka utake kubeba ukoo mzima.
Mbunge atakayepiga kelele kwenye hili na yeye atakuwa mpuuzi tu.
Huo utaratibu ni dunia nzima. Mjomba au shangazi au kaka toka lini na wapi alianza kuwa dependent?
Bima ya jamii ni bei rahisi sana. Kama una uwezo wakatie hao ndugu zako.
i bet hujasoma nini maana ya insurance!!!ndege ikianza safari leo na ikapata ajali,hata kama imechangia bima ya shilingi milioni kumi kwa mwaka,italipwa(indemnity)ya shilingi hata bilioni 100 kama thamani ya ndege ni hiyo.What i am trying to say ni kuwa insurance premiums ni kiasi kidogo kidogo kinachochangiwa na wengi lakini events za loss zinatokea chache...rudi shule!!!!
Ni kweli hili la NHIF kubadili aina ya wategemezi litakuwa limetokana na sisi wanachama kutumia nafasi vibaya ya kuruhusiwa kuweka mtu yeyote, nafikiri hili lilifanyika kwa kuangalia mazingira yetu ya kiafrika kuwa mtu achague yeye amweke nani lakini wanachama tukawa tunauza nafasi, sasa wao kama watu waliopewa dhamana ya kulinda na kuhakikisha mfuko unakuwa endelevu wakaja na huo utaratibu, pia hakuna bima duniani ambayo unamweka mtu yeyote ili mradi wewe umependa, suala la kuwapongeza ni kwa kuruhusu wazazi wa mtegemezi ambao hawana bima wawekewe, mimi kama mtu niliesomea mambo ya insurance nakubaliana nao, sio lazima nafasi zijae, ndo maana ya cross subsidization, suala la huduma ni dhana hii kuchukiwa hasa na watumishi wa taasisi za umma kwa hawapati nafasi ya kupiga dili na kuuza dawa zao, lakini lengo ni zuri, hivi ukiwa na ndugu yangu anahitaji huduma za dialysis ambapo session moja ni laki 3 na na kwa wiki n8 mara 3 utamudu kutoa mfukoni kama kipato chako ni laki sita kwa mwezi? Mhimu huduma ziboreshwe na taasisi za umma ziwatendee haki wanachama na dawa ziwepo
Wanachama wanatakiwa kupewa uhuru kuweka wategemezi wao kwani pesa inayokatwa ni ya kwao pia wamelazmishwa kujiunga. Huwezi mkata mtu pesa yake bila hiari yake kisha umwekee mashart asiyo ridhika nayo. NHIF iwe hiari kujiunga ili mtu aamue kukubaliana au kukataa mashart husika vinginevyo bado haki haijatendeka. Nawashangaa watu wanaoshabikia ufisadi huu.
kula 'like' mkuu,kweli iwe ni uamuzi wa mtu kujiunga.isiwe ya lazima kwa kila mtumishi wa serikali.
Mfano mimi nimesomeshwa na anko wangu,baba yangu alifariki lkn mama yupo hai.... Nilimweka anko mmoja wa wanufaika wangu wa nhif sasa anko alipoteza kadi yake ya bima, walichonijibu kuwa sasa hawezi kupata tena kadi kwani siyo mzazi wangu! Na hapo cjabahatika bado kupata
watoto
Raia halali!wapi umeniona napinga mada?!nimeunga mkono na kwa kusema atupe masharti ya bima nyingine najua itafika mahali tutagundua wapi tupigilie msumari wa moto ktk nadai haya tukiwa na ulinganisho