Ustaadh
JF-Expert Member
- Oct 25, 2009
- 413
- 19
Zitto akwama bungeni
na Sauli Giliard, Dodoma
MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (CHADEMA), jana alikumbana na wakati mgumu baada ya wabunge kugoma kuunga mkono hoja yake ya kutaka kuwazuia wabunge kuwamo katika bodi za mashirika ya umma.
Zitto alitaka yafanyike marekebisho katika muswada wa korosho uliowasilishwa jana bungeni na Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Stephen Wasira, ambapo alibainisha kuwa ni vema kipengele cha kuwazuia wabunge kikajumuishwa.
Alisema kuna umuhimu mkubwa kwa wanasiasa kutoingizwa katika bodi za mashirika ya umma, ikiwamo korosho, ili kuepusha migongano ya kimasilahi.
Pendekezo hilo aliliwasilisha jana asubuhi, lakini jioni wakati wa uhitimishaji, wabunge hawakumuunga mkono, hali iliyofanya kutupwa kwa marekebisho hayo.
Katika utetezi wa kutaka kukubalika kwa hoja yake, Zitto alibainisha kuwa katika Bunge kuna wabunge 322, lakini waliomo kwenye mashirika hayo ni 35 tu, ambao wengine wamekuwa wakizunguka katika bodi zaidi ya moja. Alisema madhara ya wanasiasa kuwamo katika bodi hizo kuna sababisha mgongano wa kimasilahi wakati wanapofanya maamuzi kadhaa katika mashirika ya umma, jambo ambalo kimsingi linaathiri ufanisi wa chombo husika.
Kuna umuhimu wa wanasiasa kuondolewa katika bodi hizi. Huwa tunapopita katika mashirika ya umma tunapata matatizo makubwa kwa Kamati yetu ya Ukaguzi wa Mahesabu ya Mashirika ya Umma, alilieleza Bunge. Zitto alisema Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utoah, alishawahi kupendekeza jambo hilo ili kuleta ufanisi katika mashirika hayo. Hili jambo si geni, ni ukweli usiopingika kuwa kuwapo kwa wabunge katika bodi za mashirika ya umma kwa namna moja au nyingine kunashusha uwajibikaji wa mashirika hayo, alisema Zitto.
Pamoja na utetezi huo, bado Zitto hakuweza kupata uungwaji mkono wa wabunge.
Mwenyekiti wa Bunge, Job Ndugai, ambaye alikuwa akiendesha kikao hicho cha jioni, alimtaka Zitto akubaliane na matokeo, kwa kuwa hoja yake haikuungwa mkono na wabunge. Mheshimiwa Zitto, ulitoa hoja ya kuwapo kwa marekebisho katika muswada wa korosho lakini kutokana na kutoungwa mkono na wabunge, pendekezo hilo haliwezi kuwa halali, alisema Ndugai.
Awali, Zitto alibainisha kuwa anashangazwa na muswada huo mpya kutoweka bayana kuhusu suala hilo ambalo kwa muda mrefu limekuwa likisababisha mkanganyiko wa utendaji kazi, hasa unapofika wakati wa kufanya maamuzi yenye kuiwajibisha bodi ya shirika fulani.
......................................................
Kama kawaida maslahi binafsi mbele.......ya taifa baadaye....
na Sauli Giliard, Dodoma
MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (CHADEMA), jana alikumbana na wakati mgumu baada ya wabunge kugoma kuunga mkono hoja yake ya kutaka kuwazuia wabunge kuwamo katika bodi za mashirika ya umma.
Zitto alitaka yafanyike marekebisho katika muswada wa korosho uliowasilishwa jana bungeni na Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Stephen Wasira, ambapo alibainisha kuwa ni vema kipengele cha kuwazuia wabunge kikajumuishwa.
Alisema kuna umuhimu mkubwa kwa wanasiasa kutoingizwa katika bodi za mashirika ya umma, ikiwamo korosho, ili kuepusha migongano ya kimasilahi.
Pendekezo hilo aliliwasilisha jana asubuhi, lakini jioni wakati wa uhitimishaji, wabunge hawakumuunga mkono, hali iliyofanya kutupwa kwa marekebisho hayo.
Katika utetezi wa kutaka kukubalika kwa hoja yake, Zitto alibainisha kuwa katika Bunge kuna wabunge 322, lakini waliomo kwenye mashirika hayo ni 35 tu, ambao wengine wamekuwa wakizunguka katika bodi zaidi ya moja. Alisema madhara ya wanasiasa kuwamo katika bodi hizo kuna sababisha mgongano wa kimasilahi wakati wanapofanya maamuzi kadhaa katika mashirika ya umma, jambo ambalo kimsingi linaathiri ufanisi wa chombo husika.
Kuna umuhimu wa wanasiasa kuondolewa katika bodi hizi. Huwa tunapopita katika mashirika ya umma tunapata matatizo makubwa kwa Kamati yetu ya Ukaguzi wa Mahesabu ya Mashirika ya Umma, alilieleza Bunge. Zitto alisema Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utoah, alishawahi kupendekeza jambo hilo ili kuleta ufanisi katika mashirika hayo. Hili jambo si geni, ni ukweli usiopingika kuwa kuwapo kwa wabunge katika bodi za mashirika ya umma kwa namna moja au nyingine kunashusha uwajibikaji wa mashirika hayo, alisema Zitto.
Pamoja na utetezi huo, bado Zitto hakuweza kupata uungwaji mkono wa wabunge.
Mwenyekiti wa Bunge, Job Ndugai, ambaye alikuwa akiendesha kikao hicho cha jioni, alimtaka Zitto akubaliane na matokeo, kwa kuwa hoja yake haikuungwa mkono na wabunge. Mheshimiwa Zitto, ulitoa hoja ya kuwapo kwa marekebisho katika muswada wa korosho lakini kutokana na kutoungwa mkono na wabunge, pendekezo hilo haliwezi kuwa halali, alisema Ndugai.
Awali, Zitto alibainisha kuwa anashangazwa na muswada huo mpya kutoweka bayana kuhusu suala hilo ambalo kwa muda mrefu limekuwa likisababisha mkanganyiko wa utendaji kazi, hasa unapofika wakati wa kufanya maamuzi yenye kuiwajibisha bodi ya shirika fulani.
......................................................
Kama kawaida maslahi binafsi mbele.......ya taifa baadaye....