Wabunge wataka waongezewe fedha

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,792
287,983
Wabunge wataka waongezewe fedha
Stella Nyemenohi
Daily News; Thursday,March 27, 2008 @00:02


WABUNGE wameishauri serikali iwaongezee bajeti kwa ajili ya Bunge kutoka asilimia 0.07 ya sasa hadi asilimia 0.1 ya bajeti yote.

Mapendekezo hayo, yalitolewa Dar es Salaam jana na Spika wa Bunge, Samuel Sitta katika kikao cha wabunge cha kupata maelezo kuhusu mwongozo wa kutayarisha mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2008/09 hadi 2010/11.

Hoja hiyo ya Sitta, iliungwa na asilimia kubwa ya wabunge waliokuwa wakichangia mada kuhusu mwongozo huo, iliyowasilishwa na Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo.

Katika kikao hicho kilichofunguliwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, baadhi ya wabunge walisema hata kiasi kilichopendekezwa na Spika hakitoshelezi mahitaji.

Miongoni mwao ni Mbunge wa Mlalo (CCM), Hassan Ngwilizi (CCM) aliyependekeza ifikie asilimia 0.5 na Mbunge wa Karagwe, Gosbert Blandes aliyependekeza iwe asilimia 1.5.

Kwa upande wake, Mbunge wa Kongwa, Job Ndugai (CCM), alishauri kiwango kiongezwe huku akitolea mfano wa Kenya, ambayo Bunge linapata asilimia mbili huku Mbunge wa Ubungo, Charles Keenja, akisema utegemezi wa wahisani unadidimiza.

Wengine waliounga mkono mapendekezo hayo (wote wa CCM) ni Mbunge wa Muleba Kusini, Wilson Masilingi, Mbunge wa Handeni, Dk. Abdallah Kigoda, Mbunge wa Iramba Mashariki, Mgana Msindai, na Mbunge wa Viti Maalumu, Lediana Mng'ong'o. "Hili siyo ombi. Bajeti ya wabunge iongezwe. Tumechoka kunyanyasika. Hii ni kauli ya wabunge," alisema Msindai.

Akizungumza na HabariLeo, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto alisema Bunge halina budi kuwezeshwa ili liwe huru. Kwa mujibu wake, Bunge la sasa haliko huru kutokana na utegemezi wa kupangiwa bajeti na Ofisi ya Waziri Mkuu.

Katika hatua nyingine, suala la mikataba mibovu lilijitokeza pia katika majadiliano hayo ya wabunge ambako Mbunge wa Pangani, Mohamed Risherd (CCM), alishauri serikali ifungue kesi katika Mahakama ya Kimataifa kuipinga ili kukuza uchumi.

Naye Mbunge wa Handeni ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Fedha na Uchumi, Dk. Kigoda, alishauri suala la mfumuko wa bei lichunguzwe kwa umakini kwa kile alichodai kuwa upo uwezekano mkubwa kuwa mikataba mibovu ya umeme ndiyo inachangia tatizo.

Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, aliiomba Serikali itoe ufafanuzi juu ya masharti yanayodhaniwa kuwekwa na wahisani yakisema kuwa isipotatua suala la Mwafaka, kashfa ya ufisadi katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) na ile ya Richmond, haitachangia bajeti.

Zitto alihoji hivyo kutokana na kauli iliyotolewa na Waziri Mkulo kuwa katika hali halisi ya bajeti ijayo, haitakuwa na ongezeko ikilinganishwa na ile ya mwaka 2007/08.

Katika taarifa yake, Mkulo alisema serikali itaongeza kima cha chini cha mshahara na Sh bilioni 1.45 zimetengwa kwa mwaka ujao ikilinganishwa na Sh bilioni 1.18 za mwaka 2007/2008.

Alisema katika bajeti hiyo fedha za wahisani na za ndani zimepungua kwa mwaka ujao ikilinganishwa na bajeti ya 2007/2008 kutoka Sh bilioni 2.3 hadi Sh bilioni 1.8. Majadiliano kuhusu mkutano huo wa mwongozo wa kutayarisha Bajeti ya Serikali yanaendelea leo.
 
There is something crazy about MPs discussing their own raises.There is an issue of objectivity and conflict of interest.

Keenja raised an interesting point, with our country being so donor dependent can our MPs afford to ask for raises?

Lets improve our economy and raises will be no issue.No improvement in the economy, no raise for MPs.
 
Yaani wabunge wakisema wananyanyasika sijui wale ndugu zetu wa kule kijiji cha mnyang'anyeniardhinamuyapatiemakampuniyamadini wao watasema nini sasa!
 
These wabunge must understand the issue is not about pay rise; it is about increasing productivity. Kuongeza mishahara bila tija, ni chanzo cha mfumuko wa bei katika uchumi. Every time, these wabunge will demand more and more pay rise as purchasing power falls since there is no TIJA. And if the government is not careful enough, this is a recipe for disaster--inflation spiral. TIJA,TIJA,TIJA ndio mbadala. Kuongeza mishahara isiyoendana na TIJA ni sawa na kubandika plasta juu ya donda ndugu.
 
Kwa bunge letu hili hata hiyo 0.07 bado ni mzigo kwa wananchi. Wabunge ni wawakilishi wa wananchi, sasa unapokuwa na bunge ambalo linakubali utapeli kuwa bunge halina haki wala uwezo wa kuhoji na kuona mikataba inayosainiwa na serikali, kwa mtu mwenye uelewa mdogo kama mimi najiuliza in the first place kuna faida gani ya kuwa na bunge ? Zitto anasema kuwa bunge si huru kwa kuwa linapangiwa bajeti na ofisi ya waziri mkuu, mimi nasema bunge letu si huru kwa kuwa ama wabunge wetu hawajui majukumu yao au kwa wamejawa na tamaa ambayo imefikia kiwango cha kuwapofusha.
 
Hivi hili bunge mimi silielewi,linaishi kwa kufuata muandamo wa mwezi au ni vipi.Kwamba mwezi ukiwa mchanga problem,mwezi ukikomaa kunakua na unafuu.Juzi tu tumewapongeza juu ya Rich'tayari mmekwishaota mapembe.Halafu vitu vingine ukivisikia huwezi kuamini kama vimetamkwa na mtu mwenye akili timam,hivi wabunge mnaweza kweli mkathubutu kusema eti mnanyanyasika,na yule mwalimu wa ulindwanoni kule kwa Kapuya atsemaje ambae hajawahi kwenda likizo hata kwasababu hapewi nauli yake leo wabunge mnasema mnanyanyasika are you serious au mnatania.

Hivi wewe mzee six,unashindwa kupigania upatikanaji wa barabara ya kutoka Manyoni to KGM kupitia Tabora na Urambo kwako leo unawapigania watu walioko peponi,naapa 2010 utaiskia ubunge kwenye vyombo vya habari yaani hamtufai kwa sababu nyie ni wabinafsi hamko hapo kutuwakilisha mafisadi wakubwa.

Wanaume mmekaa eti bajeti ya bunge iongezeke kwa nini msiseme bajeti ya ujenzi wa barabara iongezeke,wabunge wafanyiwe uchunguzi sio bure.Mbona hamueleweki jamani,hivi na A.Kilango na wewe ulikuwemo ktk huo wendawazimu,kama ulikuwemo basi tumekwisha maana wewe ndio kimbilio letu kwa sasa na kama utatugeuka twafwa.
 
Mi napendekeza ili kutia changamoto ku raise GDP Per Capita income ya Watanzania, na ku discourage wanaotaka ubunge kwa kufuata marupurupu, mshahara wa wabunge uwe directly pegged kwenye GDP Per Capitaincome ya Mtanzania.Kwa maana hii GDP Per Capita ya Mtanzania 2006 ilikuwa $ 800 na mshahara wa wabunge uwe $ 800 kwa mwaka,ikishuka mshahara wa wabunge nao ushuke, ikipanda mshahara wa wabunge nao upande.

Si wawakilishi wa wananchi bwana? Inabidi wawawakilishe katika kila kitu, sasa kama wao wanapata marupurupu kibao mwishowe watashindwa hata kuji identify na wananchi, watasahau machungu ya ugumu wa maisha.

This performance based compensation may actually have the positive affect of raising Tanzania's GDP Per Capita income drastically.If the issue of income distribution will be as well addressed we should be in good shape in a couple of decades as opposed to the prospect of centuries we have now.

Seriously.
 
...lack of common sense at any opportunity!


I pray each day that life in TZ will improve, but I wake up knowing we are in a cesspit and presently, there is NO light at the end of the tunnel.Money is wasted left right and centre, nobody sees anything; deception and abuse are common; nobody criticizes anything.

JK and his lap dogs are incapable of governing the people of that country. Funny thing politics, once in power the public has little or no say in the running of the motherland.

Now we have these stupid arrogant MP's who want more money without accounting for what they've been paid

what a bunch of twats!
 


I pray each day that life in TZ will improve, but I wake up knowing we are in a cesspit and presently, there is NO light at the end of the tunnel.Money is wasted left right and centre, nobody sees anything; deception and abuse are common; nobody criticizes anything.

JK and his lap dogs are incapable of governing the people of that country. Funny thing politics, once in power the public has little or no say in the running of the motherland.

Now we have these stupid arrogant MP's who want more money without accounting for what they've been paid

what a bunch of twats!

wow.........you eat twat ? hahaaaaaaaaa.... mi simo !
 
there is NO light at the end of the tunnel

GT,

It would have been better if there was no light at the end of the tunnel, there is light at the end of the tunnel but it is an oncoming train.

Prepare for catastrophy!
 
GT,

It would have been better if there was no light at the end of the tunnel, there is light at the end of the tunnel but it is an oncoming train.

Prepare for catastrophy!


By the time of the CCM conference in Dodoma, JK's gormless groupies had whipped themselves into such a frenzy of onanistic self-congratulation that they were convinced their man was the Master of the Universe.


When JK took over, though, the political pundits assured us this was "New JK era" - a strong, listening, inclusive, supercompetent President, who would lead us all to a Land of Hope and Dreams.

well, not me, I've always relied on what happens on the pitch.

The so-called "JK,aka MZEE WA PAMBA aka MUUNGWANA" has been exposed as a weak, cowardly, easily rattled, selfobsessed, buck-passing fraud - as some Jambo Forums posters told us from Day One.

Like our national coach MAXIMO, he's a loser. Unlike MAXIMO, he doesn't even have a brolly to shelter under. Even his staunchest supporters are leaving before the final whistle. Soon, (not sure though)they'll be calling for his head.
 

Like our national coach MAXIMO, he's a loser. Unlike MAXIMO, he doesn't even have a brolly to shelter under. Even his staunchest supporters are leaving before the final whistle. Soon, (not sure though)they'll be calling for his head.


Actually, the sooner this guy goes the better. We need to breath jamani, we are tired with this incompetence every where. Huyu bora atuachie vijana wetu waendelee kwenda zao Bagamoyo na hayo mahela anayolipwa huenda yakafanya jambo la maana zaidi kama hataingia kwenye mikono ya wale jamaa!
 
Hivi kuna uwezekano wa kubadili katiba nchi iongozwe bila bunge kwa miaka 5. Kuwe na kamati tu za maendeleo kwa kila wilaya basi. Huu kwa kweli ni uchuro wa wabunge sasa. Watu wanakufa kwa kukosa hela za matibabu na chakula wao wanataka kuzidisha ukubwa wa vitambi vyao bila aibu. Jamani!!
 
Hivi kuna uwezekano wa kubadili katiba nchi iongozwe bila bunge kwa miaka 5. Kuwe na kamati tu za maendeleo kwa kila wilaya basi.

Mkuu Nurujamii,

Respect mkuu, I love this one yaaani ndio utamu wa JF huu!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom