Wabunge Wataka Gongo Ihalalishwe!

Kwenye gongo kuna Ethanol ambayo ndo Ulabu wenyewe na kuna Methanol ambayo ni sumu japo ina test na kunukia kama ulabu.http://en.wikipedia.org/wiki/Methanol

Ili kuhalalisha Gongo ni lazima kufanya Fractional Distillation ili kuiondoa methanol na kuiacha ethanol.
Kitu kikubwa cha kuongezea kwenye mtambo wa gongo asilia ili kufanya Fractional Distillation ni Thermometer tu.

Mafisadi wanajiuliza Gongo likitolewa sumu huko mitaani na kuuzwa kila kona nani atakunywa Konyagi?


Methanol itumike kama Biofuel na Ethanol itumike kama ulabu.

Kangara inabakiza Step 1 au 2 kuwa Bia, vilevile Gongo ambayo inajulikana kama Machozi ya simba, supu ya mawe, chang'aa, moonshine au pombe ya moshi nayo inabakiza step moja tu ili iingie kwenye kundi la Vodka Konyagi na Martin.

Waganda tayari wanabadiri gongo kuwa pombe isiyokuwa na madhara.

Uharamu wa Gongo ni kile kiwango cha Methanol kilichomo na si vinginevyo. Kama kuna sababu nyingine ni za kisiasa.

Sasa huo utalaamu wote! Mbona Marmo amesema kuwa gongo inakatazwa kwa sababu inatengenezwa katika mazingira ya uchafu? Wala hakugusia masuala ya methanol na ethanol!
 
Leo hii inapita kabisa muda katika bunge letu tukufu linajadili kama gongo kuhalalishwa ni sahihi au la. Mwisho wa siku kila mtu anavuta mshiko wake anaelekea nyumbani. Haya hebu tuangalie mambo ya maana yanayowalenga wananchi ambayo yalihitaji muda pale bungeni......
1. Hivi jamani last time nilipocheki nyumbani, umeme ulikuwa bado ni agenda ya nani amfunge paka kengele, watu wanaogopana kuelezana ukweli kuhusu mambo muhimu ya maendeleo ya nchi yetu.

2. Usafiri ndo kizungumkuti kabisa, hata barabara za hiyo tunayoisema miji mikubwa bado ni kichekesho. Sijataja huko kunakoliletea Taifa hili maendeleo, 'vijijini'. Ukisikia Kilo moja ya mahindi inavyopata shida kupatikana utaona huruma. Kwanza mkulima hana pembejeo, akijikamua kupata angalau zinahosika, kasheshe kuisafirisha, kuileta kwa walaji, akijikamua kuileta analanguliwa bei na wajanja wa mjini.

3.Kazi hazipatikani, kama huna mjomba, shangazi, mtoto wa baba mdogo au jamaa basi wewe kibarua ni kupiga malapa na kuchapisha CV nyingi tu.

4.Ubadhirifu wa mali za umma ndo imekuwa fasheni, kama hujatafuna mali ya umma wewe si mwanasiasa mahiri, basi almuradi ni udhia tu.
Anyway nisiendeleze lawama zaidi ila leo kuhalalisha Gongo ndo muhimu....haya tena yangu macho tu...



Uloyataja ni muhimu lakini na hili la gongo nalo si dogo kwani idadi ya watumiaji kwa sample ndogo niloifanya mtaani kwetu ni kuwa asilimia 40 ya wakazi wake ni wanywaji na kati yao asilimia 70 wanatumia gongo au pombe nyengine za kiengeji, sasa kama hivyo inaweza kuchukuliwa kama representation ya population utaona umuhimu wake kwa hivyo mimi naona hakuna ubaya wa kujadili gongo bungeni na wa mawazo yangu ni vizuri ikahalalishwa na wajasiria mali wakapata elimu ya kutengeneza kisasa kwa formula inayotakiwa na faida zake ni nyingi tu. wanywaji na watengenezaji ni Wtz wana haki ya kuangaliwa matatizo yao - hujui huyo mbunge alowakilisha hoja hii pengine wapiga kura wake wengi ni kutoka katika kundi hilo jee ? Usisnangae iko siku atasimama Mbunge kutetea biashara ya mwili na haina haja ya kumlaumu - kwa vyovyote vile ni watu katika jamii na wana haki ya kuwakilishwa.
 
Mutu Just For Ur Info:::::
Ile Suruali Ikifungwa ...ukizidiwa Wanifungua Wanchukua Ule Mmminiko Wanaurudisha Kwenye Jiko Chombo Kitakachotoka Hapo Babu Kubwa Ndio Maana Wanashauri Ukinywa Usiende Mbali Sana Na Uliponywea;;;;;
Hizi Ndio Pombe Za Kup


Duh mkuu hiyo kali tehe tehe ! hii kiboko hapana sikia ila nakubali inawezekana.
Ila isije kuwa mkuu unafurahisha baraza tu.
 
Shabashi, mwenye $1M anapeta hawa tena ndani............

Kaaz kweli kweli!!

Msako wa polisi wanasa wawili
2008-04-15 17:59:57
Na Mwanaidi Swedi, Pwani

Watu wawili wanashikiliwa na Polisi mkoani Pwani kwa tuhuma za kukutwa na pombe haramu ya gongo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Henry Salewi, amesema tukio hilo limetokea jana majira ya saa 5:30 asubuhi katika msako uliokuwa kwenye eneo la Sanza wilayani Bagamoyo.

Kamanda Salewi amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Mariam Shaban, 40, mkazi wa Majani Mapana na mwingine ni Wema Abdalah, 43 mkazi wa Kidongo Chekundu.

Kamanda Salewi amesema pombe hiyo ilikuwa kwenye madumu na kupakizwa kwenye pikipiki yenye namba za usajili T 732 ATN tayari kwa kusafirishwa.

Amesema kuwa pombe hiyo ilikuwa inasafirishwa kwenda Bagamoyo mjini.

Amesema watuhumiwa watafikishwa mahakamani wakati wowote ili kujibu tuhuma zinazowakabili.

SOURCE: Alasiri
 
Jamani huyu waziri anasubiri nini au amechngangyikiwa gongo yetu ikwapi au alalishe piwa basi ile ya kujifunga chini ukiarisha inabaki kwenye nguo
 
Back
Top Bottom