Wabunge Wataka Gongo Ihalalishwe!

Tatizo lingine ni kupata kidhibiti wakati wahusika watengenezaji na wanywaji wa gongo wanapokamatwa na kuburuzwa kortini.Uzoefu unaonyesha askari polisi hunywa gongo yote wanapoikamata na hivyo kupoteza ushahidi kwa watuhumiwa.
 
Leo hii inapita kabisa muda katika bunge letu tukufu linajadili kama gongo kuhalalishwa ni sahihi au la. Mwisho wa siku kila mtu anavuta mshiko wake anaelekea nyumbani. Haya hebu tuangalie mambo ya maana yanayowalenga wananchi ambayo yalihitaji muda pale bungeni......
1. Hivi jamani last time nilipocheki nyumbani, umeme ulikuwa bado ni agenda ya nani amfunge paka kengele, watu wanaogopana kuelezana ukweli kuhusu mambo muhimu ya maendeleo ya nchi yetu.

2. Usafiri ndo kizungumkuti kabisa, hata barabara za hiyo tunayoisema miji mikubwa bado ni kichekesho. Sijataja huko kunakoliletea Taifa hili maendeleo, 'vijijini'. Ukisikia Kilo moja ya mahindi inavyopata shida kupatikana utaona huruma. Kwanza mkulima hana pembejeo, akijikamua kupata angalau zinahosika, kasheshe kuisafirisha, kuileta kwa walaji, akijikamua kuileta analanguliwa bei na wajanja wa mjini.

3.Kazi hazipatikani, kama huna mjomba, shangazi, mtoto wa baba mdogo au jamaa basi wewe kibarua ni kupiga malapa na kuchapisha CV nyingi tu.

4.Ubadhirifu wa mali za umma ndo imekuwa fasheni, kama hujatafuna mali ya umma wewe si mwanasiasa mahiri, basi almuradi ni udhia tu.
Anyway nisiendeleze lawama zaidi ila leo kuhalalisha Gongo ndo muhimu....haya tena yangu macho tu...
 
Kisha kuna mnazi nao...sisi jamaa za Digo lazima naswi tupige
debe tu!

Hizi pombe mbili zikifanyiwa mambo ya teknolojia kidogo tu, amini usiamini tunauza Europe.Kama unaona utani basi acha nikupe ishu ya utalii mitaa ya Mombasa.Kuna Hoteli moja hua inaserve kidaka.(code name for mnazi) wakati wa Desemba to tourists kama wanaona poa! Gongo na Mnazi zinachukuliwa duni just because ziko associated na low lifes.Naamini one day ngoma itatiki na ajira zitafunguka angalau hata kama nichache.

P.S.
Vodka inakuja katika dizaini tofauti na nyengine are even more potent and deadly kuliko Gongo lakini kwa vile zinauzwa katika 'clear bottles' basi rukhsa!​
 
Mtu wa Pwani:
Kule Chukwani kwenye kambi ya Jeshi ipo Gongo nzuri sana.... Then unakunywa pasipo bughuza yoyote...

Ghuba napo ni moto katika vilabu vya Gongo...

vipi kuhusu ubago nnaamini nako hakuko nyuma kwa mambo hayo ulabu
 
Kwenye gongo kuna Ethanol ambayo ndo Ulabu wenyewe na kuna Methanol ambayo ni sumu japo ina test na kunukia kama ulabu.http://en.wikipedia.org/wiki/Methanol

Ili kuhalalisha Gongo ni lazima kufanya Fractional Distillation ili kuiondoa methanol na kuiacha ethanol.
Kitu kikubwa cha kuongezea kwenye mtambo wa gongo asilia ili kufanya Fractional Distillation ni Thermometer tu.

Mafisadi wanajiuliza Gongo likitolewa sumu huko mitaani na kuuzwa kila kona nani atakunywa Konyagi?


Methanol itumike kama Biofuel na Ethanol itumike kama ulabu.

Kangara inabakiza Step 1 au 2 kuwa Bia, vilevile Gongo ambayo inajulikana kama Machozi ya simba, supu ya mawe, chang'aa, moonshine au pombe ya moshi nayo inabakiza step moja tu ili iingie kwenye kundi la Vodka Konyagi na Martin.

Waganda tayari wanabadiri gongo kuwa pombe isiyokuwa na madhara.

Uharamu wa Gongo ni kile kiwango cha Methanol kilichomo na si vinginevyo. Kama kuna sababu nyingine ni za kisiasa.
 
Gongo ni pombe kama pombe zingine. Hakuna sababu za msingi za kuagiza vodka toka nje ya nchi na wakati huo huo gonga aka kikali cha taifa kikapigwa vita. Halalisha gonga taifa lipate kodi na tujenge taifa.

Mtambo A Mtambo (Jitu la mahasira)
 
nasikia kuna aina moja ya pombe inaitwa PINGU ukinywa hiyo lazima ufunge suruali chini kwenye ugoko la sivyo.....!!
 
ingekuwa anayetetea hii pombe ni mlalahoi ningesema kuwa labda hela ya bia inamshinda.
ila sasa kinachonishangaza ni kuwa anayetetea hii haraqmu ilwe halali ni mtu ambaye kwa namna 1 au nyingine anamudu kununua bia so hapa sijui kunani.......
 
nasikia kuna aina moja ya pombe inaitwa PINGU ukinywa hiyo lazima ufunge suruali chini kwenye ugoko la sivyo.....!!


Hiyo PINGU noma ndugu yangu ,suruali miguni hufungi wewe anakufunga mama muuza usije mchafulia ukumbi wake.
 
Wacha Hiyo Juzi Kati Nimeenda Sehemu Ya Kilaji Nikakuta Kila Ukiingia Wanapouza Gongo Unapewa Mfuko Wa Plastic Wa Nini Aliewahi Kuutumia Tusaidiane Hapa Jamani.....tuweze Kuangalia Jinsi Ya Kuihahalilisha
 
Mwisho Nawapongeza Wote Waliotoa Mada Hii Na Kwa Kuangalia Wingi Wa Wachangiaji Wanaokubalia Kuhalalisha Gongo Naona Wengi Tumekubaliana Na Hili Ila Iboreshwe.....mwisho Tunapendekeza Kuwepo Na::""gongo Bottlers Company Ltd Pale Kilwa Road Pembeni Ya Kambi Ya
Jeshi...waweze Kuwalinda Watakaofanay Fujo

Wabunge Komaeni Jamani...wengine Tumedanganywa Na Dodoma Wine Matokeo Yake Doodoma Wankunywa Wakubwa Pekeyao Hivyo Lazima Watu Wa Hali Ya Chini Wakumbukwe Jamani...samahani Kama Ntawagusa Wenye Ajira Za Tbl...nk,ila Tunahakika Kiwanda Hiki Kikianzishwa Tutapata Soko Sana Sana Hasa Uarabuni Nk.....nina Marafiki Wengi Sana Wanaulizia...tusiwakatishe Tamaa....babu Malecela Sijakusikia Mpe Ya Kisigino Mama Asononeke Nalo.....hilo Watu Tushangilie....tushachoka Kuona Watu Wa Aina Moja Haohao Wanakaa Kwenye Bar Hawabadiliki........
Big Up Bunge La Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania
 
Mutu Just For Ur Info:::::
Ile Suruali Ikifungwa ...ukizidiwa Wanifungua Wanchukua Ule Mmminiko Wanaurudisha Kwenye Jiko Chombo Kitakachotoka Hapo Babu Kubwa Ndio Maana Wanashauri Ukinywa Usiende Mbali Sana Na Uliponywea;;;;;
Hizi Ndio Pombe Za Kup
 
Mi Nina Nafasi Ya Kukutana Na Huyu Mkuu Sasa Nafikiri Umefika Wakti Watu Tutoe Msaada Nini Kifanyike Kuiboresha Ili Ifikiwe Kiwango Cha Kimataifa Hata Ikishindwa Basi Ikaribie Kiwango Cha Inter.....mwanakijiji Pombe Yako Naona Unaikana Leo Hii.....toeni Formula Za Kuchanganya Na Kuchuja Watu Wasonge Mbele Wapate Ajira....
 
Back
Top Bottom