BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,011
Waungwana
Kama mnavyofahamu Wabunge wetu wanalipwa mishahara mizuri pamoja na marupurupu manono. Wengi wao hawachangii katika mijadala yoyote inayoendelea bungeni na wengine huwa mahudhurio yao ni madogo sana maana huwa mtaani wakishughulikia shughuli zao binafsi ambazo hazihusiani na wao kuwa wawakilishi wa wale waliowachagua majimboni mwao.
Mimi nafikiri wakati umefika sasa wale Wabunge wote ambao wanaenda bungeni kuchapa usingizi au hawahudhurii vikao vya bunge bila kuwa na sababu zozote za msingi za kukosekana kwao bungeni waanze kukatwa mishahara na marupurupu yao.
Kama Mbunge anakosekana Bungeni kwa wiki mbili katika mwezi bila kuwa na sababu zozote za msingi basi mshahara na marupurupu yake ya wiki mbili yaondolewa katika pay slip yake na kurudishwa hazina. Hii itasaidia sana kupambana na wabunge watoro na wale ambao hawachangii katika mijadala mbali mbali ndani ya bunge.
Kutohudhuria vikao vya bunge bila kuwa na sababu muhimu za kufanya hivyo au kuchapa usingizi ndani ya bunge bila kuchangia mijadala yoyote inayoendelea ndani ya Bunge ni ufisadi. Tunataka kuwa na bunge lenye Wabunge wachapa kazi wanaochangia katika mijadala yote inayoendelea ndani ya Bunge na pia kuhudhuria vikao vyote vya bunge bila kukosa kama hawana sababu za msingi za kufanya hivyo.
Kuna umuhimu wa kuchukua hatua mbali mbali za kuimarisha bunge letu ikiwemo mahudhurio mazuri na kuchangia katika mijadala mbali mbali ndani ya Bunge.
Kama mnavyofahamu Wabunge wetu wanalipwa mishahara mizuri pamoja na marupurupu manono. Wengi wao hawachangii katika mijadala yoyote inayoendelea bungeni na wengine huwa mahudhurio yao ni madogo sana maana huwa mtaani wakishughulikia shughuli zao binafsi ambazo hazihusiani na wao kuwa wawakilishi wa wale waliowachagua majimboni mwao.
Mimi nafikiri wakati umefika sasa wale Wabunge wote ambao wanaenda bungeni kuchapa usingizi au hawahudhurii vikao vya bunge bila kuwa na sababu zozote za msingi za kukosekana kwao bungeni waanze kukatwa mishahara na marupurupu yao.
Kama Mbunge anakosekana Bungeni kwa wiki mbili katika mwezi bila kuwa na sababu zozote za msingi basi mshahara na marupurupu yake ya wiki mbili yaondolewa katika pay slip yake na kurudishwa hazina. Hii itasaidia sana kupambana na wabunge watoro na wale ambao hawachangii katika mijadala mbali mbali ndani ya bunge.
Kutohudhuria vikao vya bunge bila kuwa na sababu muhimu za kufanya hivyo au kuchapa usingizi ndani ya bunge bila kuchangia mijadala yoyote inayoendelea ndani ya Bunge ni ufisadi. Tunataka kuwa na bunge lenye Wabunge wachapa kazi wanaochangia katika mijadala yote inayoendelea ndani ya Bunge na pia kuhudhuria vikao vyote vya bunge bila kukosa kama hawana sababu za msingi za kufanya hivyo.
Kuna umuhimu wa kuchukua hatua mbali mbali za kuimarisha bunge letu ikiwemo mahudhurio mazuri na kuchangia katika mijadala mbali mbali ndani ya Bunge.