Wabunge wanataka kodi za wanyonge ili wakajilipe Posho na Mishahara minono

Zero IQ

JF-Expert Member
Dec 21, 2016
13,917
24,674
Nchi imekuwa ya kusadikika kweli, kila siku wanabuni mbinu mpya ya kuwakamua wasiojiweza, wenye uwezo mdogo wa kuendesha maisha yao ili matumbo yao yaneemeke.

Baada ya kubuni mbinu za kuwainua wananchi ili wapate walipa kodi wengi wao ndio wanazidi kuwakamua na kuwatia umaskini

Wawakilishi wetu (wabunge) wamekuwa sio wawakilishi tena bali ni watafutia Tumbo hawajari chochote kuhusu wananchi walio chini yao.

Leo hii baada ya kujadili jinsi ya kushusha mishahara yao, posho na kiinua mgongo chao pale bungeni ili pesa zikasaidie wananchi wa kima cha chini.

Wanaishia kupiga meza na kutaka mishahara yao minono iongezwe, "sio kuongezwa tu iongozwe na tena ilipwe kwa dora"
Hawa watu wana akili kweli? Wanawaza ata vizazi vyao vya tatu vitakavyokuja kutoka wao vitaishije?

Leo hii Vocha "Kiwanda kinachotengeza kinalipa kodi serikarini, mfanyabiashara wa jumla akienda kununua analipa kodi Mwenye duka la reja reja akienda kununua vocha kwa mfanyabishara wa jumla analipa kodi Mwanachi akienda kununua vocha dukani analipa kodi
Hiyo hiyo vocha akiikwangua na kuweka kwenye simu inakatwa kodi".

Bado kuna mtu na PHD yake akaona isiishie hapo kwenye hiyo hiyo vocha ambayo ilishalipiwa kodi kama mara nne punde tu ikimfikia mtu wa mwisho nae akiweka serikari ikishakata chao ile asilimia kadhaa, bado pia itataka imkate kiasi cha shilingi 100--200 cash mwananchi mnyonge ili ikalipe posho, mishahara na kiinua mgongo kwa aliyeleta hiyo dhahama kwa wananchi wa chini.

Nchi ina Rasilimali kibao, ina madini, mafuta, gas, mbuga za wanyama, Ardhi yenye Rutuba, bahari na N.k. Bado Mawazo ya viongozi wetu wenye PHD kama wanavyojinasibu yameganda mgando wakitegemea Rasilimali watu pekee tena wananchi wa hali ya chini kuendesha nchi.

Dubai ina mafuta pekee lakini kila mtu anatamani kwenda kula bata huko

Viongozi wetu waache kutegemea rasilimali watu pekee Wajikite zaidi kwenye kutanua wigo mzuri kwa wawekezaji Waweke sera rafiki,wapunguze masharti na mrundikano mkubwa wa kodi ila wawavutie wawekezaji.

Wakalibishwe ata ikibidi bila masharti na punguzo kubwa la kodi ili tufanye mapinduzi ya viwanda, ili watu ambao ni Rasilimali wajikite kwenye kufanya kazi ili kuinua taifa letu

Kama taifa tunatakiwa kuwa na sera, sheria dhabiti ya uwekezaji isiyohadhiriwa na uongozi uliopo madarakani ili tupate wawekezaji.

Tukiendelea kutegemea Rasilimali watu pekee hatutavuka hatua yeyote kama Taifa, siku zote tutabakia hapa hapa na pengine kuwa chini zaidi ya hapa.

Cc Zero IQ
 
Wao hawana maumivu,mawasiliano yao ofisi inawalipia.

"WANANCHI TUFUNGE MKANDA"
2025 TWENDE NA MWIGULU ATAENDELEA KUTULETEA KODI YA KUKU.
 
Ubunge Africa ni biashara kubwa yenye mtaji kidogo sana na masharti yake ni rahisi.Baadhi ya Wananchi wanavyoishi kwa mlo mmoja alafu mbwa koko kwa mgongo wa bunge analia eti ni pesa ndogo waongezewe,huyo aliyesema aongezwe mshahara hata akifa leo afe tu kwani ni hasara kwa bunge letu.
 
Mbona Kodi hizo hizo zinawalipa wale covid-19 kununua gari la rais mstafu na kujenga nyumba ya rais mstafu

Wabunge kazeni buti kabisa Mpaka serikali iongeze mishahara na posho CCM oyeeeeeeee
 
Ubunge Africa ni biashara kubwa yenye mtaji kidogo sana na masharti yake ni rahisi.Baadhi ya Wananchi wanavyoishi kwa mlo mmoja alafu mbwa koko kwa mgongo wa bunge analia eti ni pesa ndogo waongezewe,huyo alisema aongezwe mshahara hata akifa leo afe ni tu kwani ni hasara kwa bunge letu.
Congo rais kawapa wabunge magari ya kifahari
 
Kwa upande wangu siwalaumu wabunge.
Kila mtu aliyekatika utumishi wa umma anatamani kupanda mshahara na ni haki yake kuomba kuongezwa mshahara. Kama kigezo ni mshahara wao kuwa mkubwa basi hata madaktari hawapaswi kuomba kuongezwa mshahara kwasababu walimu wanalipwa nusu ya mshahara wao.

Kila mtu adai kuongezwa mshahara na siyo kumkataza mtu kuomba nyongeza kwa sababu eti mshahara wako ni asilimia 10 ya mshahara wake. Kila mtu adai kuongezwa mshahara pale alipo.

Kama unaamini wabunge wanakula pesa nyingi bila kufanya kazi ya maana basi gombea ubunge ili ukapate hiyo salary.
 
Hili bunge ni la kuvunjwa tu,tangu waingie hakuna cha maana kinachojadiliwa ni ubinafsi na kuwaibia wananchi tu,tutaishi kwa majuto sana miaka hii na bunge hili
 
Hawana akili hao, wabunge wana akili ya mbu. Bunge liko Dodoma karibu na Mirembe Hodpital. Hao wote wanatKiwa kuwa Mirembe siyo Bungeni. Yamekaa Dodoma for 6 months kila siku hatuna zao ni kupongeza Rais Badala ya kujadili hali zetu. They are imbeciles at the top level.
 
Wale waliingia kwa hisani za mwendazake, hawana ubavu wa kushinda uchaguzi huru. Wanatafuta utajiri wa kusepa nao maana hawana uhakika wa kurudi sababu mbeleko ya mwendazake haipo tena...
 
Hao ni kuwatengenezea petitions za kutosha, na hashtags, za
#wabunge_walipe_kodi
#wabunge_wasilipwe_pension
#wabunge_wapunguziwe_mishahara

Everyday is Saturday............................... 😎
 
Wabunge wakisoma hizi komenti za wananchi lazima watajibu mapigo kwa kuomba kutoa hoja bungeni kupinga maoni ya wananchi kuwa mshahara wao ni mdogo, badala ya kujisahihisha wawe Wazalendo wajipunguzie mshahara, marupurupu pia kuweka azimio waanze kulipa kodi.
 
Hao ni kuwatengenezea petitions za kutosha, na hashtags, za
#wabunge_walipe_kodi
#wabunge_wasilipwe_pension
#wabunge_wapunguziwe_mishahara

Everyday is Saturday............................... 😎
Hilo hawatapitisha. Nchi inaliwa for the next 15 years. Wizi wa hali ya kuku unaendelea. Magufuli kafa tumerudi enzi za Kikwete.
 
Hilo hawatapitisha. Nchi inaliwa for the next 15 years. Wizi wa hali ya kuku unaendelea. Magufuli kafa tumerudi enzi za Kikwete.
Huyo Magufuli mwenyewe hakuwahi kuwagusia kodi hao wabunge, na kupeleka wabunge vibogoyo wa kusifia na kuabudu sanaa zake za maigizo, mbaya SANA kawaweka na UVIKO-19 wale kodi za wanyonge.
Nchi hii inatakiwa kuumbwa upya...

Everyday is Saturday.............................. 😎
 
Back
Top Bottom