Chakaza
JF-Expert Member
- Mar 10, 2007
- 39,757
- 71,132
Ni kama mtu aliyekuwa amefunikwa blanket gubigubi wakati kumekucha kisha ulitoe akutane na mwanga ndivyo ilivyotokea kwa wabunge wa CCM Jana baada ya kushuhudia viongozi wa zamani wa chama chao waliojiondoa wakitinga na sura za bashasha, afya njema na bila kinyongo wala hofu.
Ndani ya viunga hivyo vya bunge makundi ya baadhi ya wabunge wa ccm walisikika wakisema "maisha haya ya kujipendekeza na kushindwa kuwa huru mpaka lini? Sasa tusimamie ukweli kama ni kufukuzana potelea mbali."
Wamesema mbona ma PM wanaweza kuiacha ccm sisi ni nani hadi tufie ndani ya moto wakati huko nako maisha ya kawaida yapo?
Kuna walio apa kabisa kuwa wameingia bungeni sio kwa msaada au nguvu ya ccm bali kukubalika kwao na wananchi na kuwa hata wakigombea kwa tiketi ya chama kama TLP watapita tuu.
My Take;
Jee kitendo cha Mbunge wa Shinyanga kumwaga ubuyu kuisema serikali huku akishangiliwa na bunge zima ndio uasi umeanza?
Au uongo wa Jenister Mhagana ambao siku za nyuma ungeshangiliwa lakini Jana ulizomewa ndio mwanzo wa kukataa ukondoo?
Kila la kheri kama mtakuwa mmegundua kuwa nje ya ccm nako kuna maisha, tena yaliyo huru. Hakuna kitu kibaya kama mtu mzima kuishi kama mnafiki na kujipendekeza kiasi cha kushindwa kusimamia ukweli na huku unajua kuwa watu na familia yako wanajua umekuwa mnafiki
Ndani ya viunga hivyo vya bunge makundi ya baadhi ya wabunge wa ccm walisikika wakisema "maisha haya ya kujipendekeza na kushindwa kuwa huru mpaka lini? Sasa tusimamie ukweli kama ni kufukuzana potelea mbali."
Wamesema mbona ma PM wanaweza kuiacha ccm sisi ni nani hadi tufie ndani ya moto wakati huko nako maisha ya kawaida yapo?
Kuna walio apa kabisa kuwa wameingia bungeni sio kwa msaada au nguvu ya ccm bali kukubalika kwao na wananchi na kuwa hata wakigombea kwa tiketi ya chama kama TLP watapita tuu.
My Take;
Jee kitendo cha Mbunge wa Shinyanga kumwaga ubuyu kuisema serikali huku akishangiliwa na bunge zima ndio uasi umeanza?
Au uongo wa Jenister Mhagana ambao siku za nyuma ungeshangiliwa lakini Jana ulizomewa ndio mwanzo wa kukataa ukondoo?
Kila la kheri kama mtakuwa mmegundua kuwa nje ya ccm nako kuna maisha, tena yaliyo huru. Hakuna kitu kibaya kama mtu mzima kuishi kama mnafiki na kujipendekeza kiasi cha kushindwa kusimamia ukweli na huku unajua kuwa watu na familia yako wanajua umekuwa mnafiki