jogi
JF-Expert Member
- Sep 25, 2010
- 25,558
- 25,322
Chonde chonde wabunge, hasa wa CCM.
Tunawaasa msiipitishe budget ya Wizara ya nishati na madini, mkilogwa au kuhongwa mkaipitisha mtakuwa mmetangaza mgogoro kati ya wabunge wa CCM na wananchi.
Kumbukeni yule mgiriki aliyesema serikali ya Tanzania iko mfukoni mwake enzi za Nyerere, lugha hiyo ilitafsirika kuwepo uwezekano wa hongo, simulizi za Nyerere zinabainisha kuwa japo hawakupata uthibitisho wa hongo, ilimgharimu mgiriki kufukuzwa nchini baada kuswekwa rumande, watu wengi walimuombea upatanisho bila mafanikio, alifukuzwa na kuonywa asikanyage tena afrika mashariki.
Waziri ama chama cha CCM aki/kikiwalaghai mkaipitisha bajeti ambayo kwa mwendelezo wake kwa mfululizo wa miaka kadhaa sasa tunaelekea kuweka rekodi ya dunia ya kuwa taifa huru la kwanza tena lenye amani tele na utajiri wa maliasili nyingi lakini kuishi gizani totoro kwenye karne ya 21!!!
Hatutawaelewa, mtakuwa mmehongwa, na hongo ya kwanza ni sitting allowance ambayo sisi wapiga kura hatukupeni bali bunge lawapa pasipo ridhaa yetu. OLE OLE WENU!!!
Tunawaasa msiipitishe budget ya Wizara ya nishati na madini, mkilogwa au kuhongwa mkaipitisha mtakuwa mmetangaza mgogoro kati ya wabunge wa CCM na wananchi.
Kumbukeni yule mgiriki aliyesema serikali ya Tanzania iko mfukoni mwake enzi za Nyerere, lugha hiyo ilitafsirika kuwepo uwezekano wa hongo, simulizi za Nyerere zinabainisha kuwa japo hawakupata uthibitisho wa hongo, ilimgharimu mgiriki kufukuzwa nchini baada kuswekwa rumande, watu wengi walimuombea upatanisho bila mafanikio, alifukuzwa na kuonywa asikanyage tena afrika mashariki.
Waziri ama chama cha CCM aki/kikiwalaghai mkaipitisha bajeti ambayo kwa mwendelezo wake kwa mfululizo wa miaka kadhaa sasa tunaelekea kuweka rekodi ya dunia ya kuwa taifa huru la kwanza tena lenye amani tele na utajiri wa maliasili nyingi lakini kuishi gizani totoro kwenye karne ya 21!!!
Hatutawaelewa, mtakuwa mmehongwa, na hongo ya kwanza ni sitting allowance ambayo sisi wapiga kura hatukupeni bali bunge lawapa pasipo ridhaa yetu. OLE OLE WENU!!!