Wabunge waibua ufisadi Sh25 bilioni Maliasili

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,299
33,080
pac-waandish.jpg
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali, John Cheyo (Kushoto) akizungumza na wajumbe kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii walipokuwa wakiwasilisha taarifa za Wizara hiyo katika Osifi ndogo za Bunge jijini Dar ES Salaam jana.Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati,Zainab Vullu.Picha na Venance Nestory​
Patricia Kimelemeta
KAMATI ya Bunge ya Hesabu za Serikali Kuu (PAC) imebaini utata wa matumizi ya zaidi ya Sh25 bilioni katika Wizara ya Maliasili na Utalii, huku watendaji wa wizara hiyo wakikosa takwimu za idadi ya wanyamapori na vitalu vya uwindaji.

Kashfa hiyo imezidi kuitikisa wizara hiyo kwani hivi karibuni ilikumbwa na kashfa nyingine ya utoroshaji nje twiga wakiwa hai, kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).

Jana, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa PAC, John Cheyo alisema fedha hizo zinatokana na mapato kutoka vyanzo mbalimbali vya wizara hiyo.

PAC kwa muda wa wiki nzima imekuwa ikipokea taarifa za wizara mbalimbali za Serikali, ikiwamo Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ambako iliibua ukata katika balozi za Tanzania nje na juzi, ilikutana na watendaji wa Ofisi ya Waziri Mkuu na kubaini utata wa matumizi ya Sh1.5 bilioni za mafuriko ya Kilosa.

Cheyo alisema kamati yake katika Wizara ya Maliasili na Utalii pia ilibaini watendaji wa wizara hiyo kutokuwa na takwimu za wanyama, vitalu vya uwindaji, takwimu za watalii wanaoingia na kutoka pamoja na rasilimali mbalimbali zinazoweza kuiingizia nchi mapato, jambo ambalo limesababisha kupata hati chafu kwa miaka mitatu mfululizo.

“Nashindwa kujua mnafanyaje kazi wakati hamna hata takwimu za wanyama wala watalii wanaoingia nchini, jambo hili linaisababishia Serikali kushindwa kuingiza mapato na kuweka mianya ya wizi, kutokana na hali hiyo mnapaswa kubadilika na kufanya kazi zenu kwa kufuata sheria na taratibu zilizowekwa na nchi,”alisema na kuongeza.


“Kutokana na ripoti iliyowasilishwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), imebaini kuwa zaidi ya Sh25 bilioni zimetumika kinyume na taratibu katika kipindi cha mwaka jana, na kwamba matumizi hayo hayako kwenye vitabu vya Serikali wala hazina,” alisema Cheyo.

Alisema hilo ni kosa kwani watendaji walipaswa kuwasilisha fedha hizo hazina ikiwa ni pamoja na kuandika mchanganuo wa matumizi ili taarifa zake ziwekwe kwenye vitabu vya Serikali.

Lakini, Cheyo alisema kilichofanyika ni kuchukua uamuzi mkononi wakati wakijua kuwa wanachokifanya ni kinyume na sheria.

“Huwezi kuchukua fedha za Serikali bila ya kutoa maelezo, fedha zinazoingia kwenye wizara zinapaswa kuwasilishwa hazina ili ziweze kuhakikiwa ndipo ziweze kurudishwa kwenye wizara husika kwa ajili ya matumizi husika. Lakini, kilichofanyika wizara hii ni kuchukua mgawo wao mapema huku wakijua wanachokifanya ni kosa,”alibainisha.

Alisema kutokana na hali hiyo, mapato ya wizara hiyo yamekuwa yakishuka kila mwaka kutokana na watendaji wake kutokuwa makini, hali ambayo inaonyesha wazi kuwa, wanashindwa kutimiza majukumu yao ipasavyo.

Kwa mujibu wa Cheyo, makadirio ya ukusanyaji wa mapato ya wizara hiyo kwa mwaka 2010 yalikuwa ni Sh1.7trilioni, lakini walikusanya Sh79bilioni, mwaka 2011 mapato yalishuka na kufikia 52bilioni na sasa hawana hata shilingi.

Alisema idadi ya watalii wanaoingia nchini ni kubwa, lakini fedha zinazowasilishwa serikalini ni ndogo ambazo hazilingani na idadi hiyo, hali ambayo inaonyesha wazi fedha hizo zinapotea kinyume na taratibu.

Alisema idadi ya watalii wanaolala kwenye hoteli za hapa nchini ni kubwa, lakini fedha zinazowasilishwa serikalini ni ndogo na hazilingani na idadi hiyo ya watalii, jambo ambalo linaonyesha wazi kuna wajanja wanatumia nafasi hiyo kuiba mapato ya Serikali.

Cheyo aliongeza kwamba wizara hiyo ni nyeti kwa ajili ya kuongeza mapato ya Serikali, lakini watendaji wake wanashindwa kuwajibika ipasavyo jambo ambalo limesabababisha fedha nyingi kutumika kinyume na utaratibu.

Alifafanua kwamba kutokana na hali hiyo, watendaji hao wa wizara wanapaswa kuweka mifumo ya uwazi ya ukusanyaji wa mapato ili kila mtu aweze kubaini kiasi kilichoingia, kilichotoka na matumizi yake na si kuweka usiri ambao unasababisha mianya ya wizi.

Kamati hiyo imewaagiza watendaji hao kukaa na hazina ili waweze kuhakiki mapato na kuwasilisha taarifa hizo kwenye vitabu ya Serikali.

Mbali na hilo, pia PAC imewataka watendaji wa wizara hiyo kuweka utaratibu wa kuwataka watalii wanaoingia nchini kulipa fedha za Kitanzania na si kutumia fedha za kigeni kama ilivyo sasa.

Kauli ya Katibu Mkuu
Hata hivyo, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Maimuna Tarishi alikiri kuwepo kwa wafanyabiashara wajanja wa hoteli wanaokwepa kulipa kodi na kusababisha wizara hiyo kukusanya kiasi kidogo cha fedha kila mwaka.

“Ni kweli, kuna baadhi ya wafanyabiashara wa hoteli kuwa wajanja na kushindwa kodi stahiki, lakini sasa hivi tunabadili mfumo na kuwepo mfumo wa kielectronic ili tuweze kujua idadi ya watalii walioingia nchini,”alisema Tarishi.

chanzo.
Wabunge waibua ufisadi Sh25 bilioni Maliasili
 
Hivi wabunge ndio huwa wanaibua au huwa utata/matumizi mabaya yamebainishwa kwenye taarifa ya Makaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Serikali?
 
Hizi stori kila siku tu tunazisikia, mi nadhani ni jinsi tu ya kuhalalisha posho zao tu, maana baada ya hapo hutasikia chochote kimefanyika!
hivi ile ishu ya TCRA imeishia wapi? Impact ya hizi kamati za bunge mia bado kuiona kabisa
 
pac-waandish.jpg
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali, John Cheyo (Kushoto) akizungumza na wajumbe kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii walipokuwa wakiwasilisha taarifa za Wizara hiyo katika Osifi ndogo za Bunge jijini Dar ES Salaam jana.Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati,Zainab Vullu.Picha na Venance Nestory​

Patricia Kimelemeta
KAMATI ya Bunge ya Hesabu za Serikali Kuu (PAC) imebaini utata wa matumizi ya zaidi ya Sh25 bilioni katika Wizara ya Maliasili na Utalii, huku watendaji wa wizara hiyo wakikosa takwimu za idadi ya wanyamapori na vitalu vya uwindaji.

Kashfa hiyo imezidi kuitikisa wizara hiyo kwani hivi karibuni ilikumbwa na kashfa nyingine ya utoroshaji nje twiga wakiwa hai, kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).

Jana, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa PAC, John Cheyo alisema fedha hizo zinatokana na mapato kutoka vyanzo mbalimbali vya wizara hiyo.

PAC kwa muda wa wiki nzima imekuwa ikipokea taarifa za wizara mbalimbali za Serikali, ikiwamo Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ambako iliibua ukata katika balozi za Tanzania nje na juzi, ilikutana na watendaji wa Ofisi ya Waziri Mkuu na kubaini utata wa matumizi ya Sh1.5 bilioni za mafuriko ya Kilosa.

Cheyo alisema kamati yake katika Wizara ya Maliasili na Utalii pia ilibaini watendaji wa wizara hiyo kutokuwa na takwimu za wanyama, vitalu vya uwindaji, takwimu za watalii wanaoingia na kutoka pamoja na rasilimali mbalimbali zinazoweza kuiingizia nchi mapato, jambo ambalo limesababisha kupata hati chafu kwa miaka mitatu mfululizo.

“Nashindwa kujua mnafanyaje kazi wakati hamna hata takwimu za wanyama wala watalii wanaoingia nchini, jambo hili linaisababishia Serikali kushindwa kuingiza mapato na kuweka mianya ya wizi, kutokana na hali hiyo mnapaswa kubadilika na kufanya kazi zenu kwa kufuata sheria na taratibu zilizowekwa na nchi,”alisema na kuongeza.


“Kutokana na ripoti iliyowasilishwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), imebaini kuwa zaidi ya Sh25 bilioni zimetumika kinyume na taratibu katika kipindi cha mwaka jana, na kwamba matumizi hayo hayako kwenye vitabu vya Serikali wala hazina,” alisema Cheyo.

Alisema hilo ni kosa kwani watendaji walipaswa kuwasilisha fedha hizo hazina ikiwa ni pamoja na kuandika mchanganuo wa matumizi ili taarifa zake ziwekwe kwenye vitabu vya Serikali.

Lakini, Cheyo alisema kilichofanyika ni kuchukua uamuzi mkononi wakati wakijua kuwa wanachokifanya ni kinyume na sheria.

“Huwezi kuchukua fedha za Serikali bila ya kutoa maelezo, fedha zinazoingia kwenye wizara zinapaswa kuwasilishwa hazina ili ziweze kuhakikiwa ndipo ziweze kurudishwa kwenye wizara husika kwa ajili ya matumizi husika. Lakini, kilichofanyika wizara hii ni kuchukua mgawo wao mapema huku wakijua wanachokifanya ni kosa,”alibainisha.

Alisema kutokana na hali hiyo, mapato ya wizara hiyo yamekuwa yakishuka kila mwaka kutokana na watendaji wake kutokuwa makini, hali ambayo inaonyesha wazi kuwa, wanashindwa kutimiza majukumu yao ipasavyo.

Kwa mujibu wa Cheyo, makadirio ya ukusanyaji wa mapato ya wizara hiyo kwa mwaka 2010 yalikuwa ni Sh1.7trilioni, lakini walikusanya Sh79bilioni, mwaka 2011 mapato yalishuka na kufikia 52bilioni na sasa hawana hata shilingi.

Alisema idadi ya watalii wanaoingia nchini ni kubwa, lakini fedha zinazowasilishwa serikalini ni ndogo ambazo hazilingani na idadi hiyo, hali ambayo inaonyesha wazi fedha hizo zinapotea kinyume na taratibu.

Alisema idadi ya watalii wanaolala kwenye hoteli za hapa nchini ni kubwa, lakini fedha zinazowasilishwa serikalini ni ndogo na hazilingani na idadi hiyo ya watalii, jambo ambalo linaonyesha wazi kuna wajanja wanatumia nafasi hiyo kuiba mapato ya Serikali.

Cheyo aliongeza kwamba wizara hiyo ni nyeti kwa ajili ya kuongeza mapato ya Serikali, lakini watendaji wake wanashindwa kuwajibika ipasavyo jambo ambalo limesabababisha fedha nyingi kutumika kinyume na utaratibu.

Alifafanua kwamba kutokana na hali hiyo, watendaji hao wa wizara wanapaswa kuweka mifumo ya uwazi ya ukusanyaji wa mapato ili kila mtu aweze kubaini kiasi kilichoingia, kilichotoka na matumizi yake na si kuweka usiri ambao unasababisha mianya ya wizi.

Kamati hiyo imewaagiza watendaji hao kukaa na hazina ili waweze kuhakiki mapato na kuwasilisha taarifa hizo kwenye vitabu ya Serikali.

Mbali na hilo, pia PAC imewataka watendaji wa wizara hiyo kuweka utaratibu wa kuwataka watalii wanaoingia nchini kulipa fedha za Kitanzania na si kutumia fedha za kigeni kama ilivyo sasa.

Kauli ya Katibu Mkuu
Hata hivyo, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Maimuna Tarishi alikiri kuwepo kwa wafanyabiashara wajanja wa hoteli wanaokwepa kulipa kodi na kusababisha wizara hiyo kukusanya kiasi kidogo cha fedha kila mwaka.

“Ni kweli, kuna baadhi ya wafanyabiashara wa hoteli kuwa wajanja na kushindwa kodi stahiki, lakini sasa hivi tunabadili mfumo na kuwepo mfumo wa kielectronic ili tuweze kujua idadi ya watalii walioingia nchini,”alisema Tarishi.

chanzo.
Wabunge waibua ufisadi Sh25 bilioni Maliasili
Tuliisha wahi kuandika hapa kuwa huko wizara ya maliasili na vitengo vyake kama TANAPA na vingine matumizi ya fedha za umma zimekuwa kama zao!!!! Tulimuomba Mheshimiwa Lema afutile kwa maana hilo ni eneo, kujua vyanzo vya mapato mkoa wa ARUSHA North Tourist Zone !!!! Hiyo itakuwa ni kidogo miaka yote ni fedha ngapi zilizo potea kwa njia hiyo?????

 
Hivi wakishaibua then wanachukua hatua gani???
Mkuu unajua wabunge siyo executive ila wakati mwingine huwa wanataka kuwa executive. wanachotakiwa si kutoa tu maneno ya sijui hela zatafunwa sijui nini na makelele mengine kibao bila matendo. Mimi naona ni kama usanii tu; wanatakiwa wawabane wanasiasa (mawaziri) ndani y bunge hadi wapate maelezo ya kutosha juu ya tuhuma wanaziona kwenye repoti za wakaguzi. Lakini hizi kauli za naunga mkono kwa asilimia mia hututafika kokote!
 
Nashukuru Mh Spika kwa kunipa nafasi hii adimu. Najua pesa zimeliwa lakini naunga mkono kwa asilimia mia. Ahsante. Magamba style!!
 
Tuliisha wahi kuandika hapa kuwa huko wizara ya maliasili na vitengo vyake kama TANAPA na vingine matumizi ya fedha za umma zimekuwa kama zao!!!! Tulimuomba Mheshimiwa Lema afutile kwa maana hilo ni eneo, kujua vyanzo vya mapato mkoa wa ARUSHA North Tourist Zone !!!! Hiyo itakuwa ni kidogo miaka yote ni fedha ngapi zilizo potea kwa njia hiyo?????


Lema akaja na jibu gani?
 
Tanzania ya kesho itajengwa leo na hasa vijana tuchukue hatua ya vitendo na si maneno matupu
 
Kwa kweli haya mambo sasa yametosha!Wizara hii inaonekana ina mabo kweli,kwani ni wizara ni miongoni mwa wizara chache zisizo na naibu waziri!Pia mwisho mwa mwaka jana Mh.waziri( Maige) alitamba kwamba huko jimboni mwake amechangia shughuli za kimaendeleo zenye dhamani ya karibu shilingi za Kitanzania milioni mia tano(5M),je hizi alizipata wapi?Je mshahara na marupurupu yake vina hiyo dhamani?Nafikiri hapo ndipo tume inatakiwa ianzie kufanya uchunguzi wake ktk kutafuta ukweli wa mambo!
 
Bunge na kamati zisizokua na meno!! Hao wezi ndio wameshikiria uchumi wa nchi,wakikamatwa uchumi utayumba bwana,bora waendelee kuiba!
 
Kamati inaenda kumchunguza sugu na mnyika hahaaaa kazi kweli kweli,kina chenga,lowassa,shimbo,kikwete,legal ofisa(rz1) etc wanadunda tuuuu kweli tz shamba la bibi,hii nchi haitakomboka mpaka kiongozi(fisadi) apigwe risasi adharani na mwananchi hili iwe fundisho!
 
Mh ukistaajabu hili hujui lile! Nchi hii tajiri bwana haiwezi kwisha wiki hujasikia billions of money zimegundulika kuibiwa then hakuna kinachofata. Toka saa hii siwezi ita Tanzania maskini, ni tajiri mjinga, wenyewe mnasema babu jinga kaa ufikiri mali zako zinaliwa.
 
Ivi kila siku hii kamati inaibua utata juu ya matumizi ya mabaya ya fedha za umma...na hakuna kitu kinafanyika...
maana cjawahi sikia taarifa ya kuwa waliosababisha hiyo hasara wamechukuliwa hatua wala nini..
kila sku ni taarifa ya ''TUMEIBUA UFISADI".......ETC..
Then what next...
 
Back
Top Bottom