idumu
Member
- Jun 5, 2009
- 44
- 1
Ramadhan Semtawa na Tausi Mbowe, Dodoma
WABUNGE wameendelea kuichambua Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2009/10, huku mbunge akihoji uamuzi wa serikali kutenga Sh19 bilioni kwa ajili ya chai na vitafunwa kwa wizara mbalimbali.
Kiasi hicho cha fedha kilichotengwa kwa ajili ya chai na vitafunwa, kimewekwa katika kipindi ambacho nchi inapita katika wakati mgumu kiuchumi kufuatia mtikisiko wa uchumi duniani.
Akichangia hotuba hiyo katika siku ya tatu ya mjadala wa hotuba bajeti, Mbunge wa Kojan, Salimu Yusuph Mohamed (CUF) alisema kiasi hicho cha fedha ni kikubwa ikizingatiwa kwamba, Watanzania walio wengi wanaishi katika dimbwi la umaskini.
Tumeona bajeti ya safari za nje ni Sh34 bilioni na leo nimepitia bajeti hii naona kuna Sh19 bilioni ambazo zimetengwa kwa ajili ya bajeti ya chai kwa wizara mbalimbali, hii inashangaza sana. Iko wapi huruma ya serikali au ndiyo ile style (mbinu) ya mamba, ambaye anamuua na kumla binadamu huku machozi yakimtoka; utafikiri analia kumbe anafurahi. Kwa hiyo serikali nayo inafanya style ya mamba kwa wananchi.
Akitoa mchanganuo huo kwa baadhi ya ya fungu la chai za wizara, alisema Wizara ya Fedha na Uchumi imetengewa Sh500 milioni huku wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika ikitengewa Sh 226.3 milioni.
Chai siyo mbaya, lakini tunapaswa kuangalia nchi yetu iko katika kipindi gani kwani sasa tuko katika wakati mgumu, hivyo kutenga kiasi hicho kwa ajili ya chai tu, nafikiri si sahihi, alisisitiza mbunge huyo.
Alikumbusha bunge kwamba, limepunguzwa muda kukutana ili kubana matumizi, hivyo hakuna sababu za kuwa na matumizi makubwa katika mambo yasiyo muhimu sana kwa taifa.
Mbunge huyo alihoji: Tumepunguza muda wa mkutano wa Bunge ili kubana matumizi, sasa haya mambo mengine ambayo tumeona kama safari za serikali kutengewa Sh34 bilioni yana maana gani?
Kwa ufafanuzi, alisema Watanzania walio wengi kwa sasa wanaishi katika hali ngumu ya umaskini kutokana na kuwa na kipato kidogo, ambacho hakiwezi kukidhi mahitaji ya maisha.
Mbunge huyo akisisitiza hilo, alisema hata takwimu za kimataifa (Malengo ya Maendeleo ya Milenia MDGs) zinataka nchi zote duniani kupunguza idadi ya watu maskini wanaopata dola moja kwa siku.
Hata hapa ndani tulipo, hebu kwa mfano chukua Sh 2,000 umpe mtu, unafikiri ataishi vipi, ataigawa na kuitumia vipi fedha kama hiyo? alihoji.
Kwa upande wake Mbunge wa Kasulu Magharibi Profesa, Kilontsi Mporogomyi (CCM), aliwashambulia baadhi ya wabunge ambao wanaisifia serikali badala ya kukaa na kuikosoa kwa kuipa changamoto.
Hebu wabunge tuache utani hapa ndani, hatuko hapa kuisifia serikali ni kweli tunaangalia Progress (maendeleo), lakini hata Marekani wabunge wakiingia bungeni wanaiambia serikali fanyeni hivi, alisema na kuongeza:
Sasa hapa, sisi tunataka kuisifia serikali, unaisifia serikali wakati baba na mama yako wanaishi kwa umaskini wa kutisha vijijini kule? Huu ni utani!
Profesa Mporogomyi ambaye aliwahi kuwa Naibu Waziri miaka ya nyuma, alisema kuna umuhimu wa kuwekwa miundombinu imara ya kiuchumi ili kuwaondolea Watanzania umaskini.
Kuhusu bandari, alisema ni aibu kuzungumzia suala hilo kwani zipo nchi ambazo uchumi wake unaendeshwa kwa bandari tu.
Huku akionekana kuchukizwa na utendaji mbovu wa bandari, alishauri iwepo wizara itakayohusika na bandari kwani wizara ya sasa ya Miundombinu imeshindwa kazi.
Kwa upande wake Mbunge wa Iringa Mjini, Monica Mbega (CCM), alisema ni vema serikali ikaangalia upya kodi katika vinywaji baridi kwani kitendo cha kupandisha kodi kitapunguza wanywaji tofauti na serikali inavyofikiria.
Nafikiri uamuzi huu wa serikali kupandisha kodi katika vinywaji baridi unaweza kupunguza idadi ya wanywaji, maana kama ni soda zitanywewa kwenye harusi na misiba tu au mtu akilazwa hospitali, alifafanua.
WABUNGE wameendelea kuichambua Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2009/10, huku mbunge akihoji uamuzi wa serikali kutenga Sh19 bilioni kwa ajili ya chai na vitafunwa kwa wizara mbalimbali.
Kiasi hicho cha fedha kilichotengwa kwa ajili ya chai na vitafunwa, kimewekwa katika kipindi ambacho nchi inapita katika wakati mgumu kiuchumi kufuatia mtikisiko wa uchumi duniani.
Akichangia hotuba hiyo katika siku ya tatu ya mjadala wa hotuba bajeti, Mbunge wa Kojan, Salimu Yusuph Mohamed (CUF) alisema kiasi hicho cha fedha ni kikubwa ikizingatiwa kwamba, Watanzania walio wengi wanaishi katika dimbwi la umaskini.
Tumeona bajeti ya safari za nje ni Sh34 bilioni na leo nimepitia bajeti hii naona kuna Sh19 bilioni ambazo zimetengwa kwa ajili ya bajeti ya chai kwa wizara mbalimbali, hii inashangaza sana. Iko wapi huruma ya serikali au ndiyo ile style (mbinu) ya mamba, ambaye anamuua na kumla binadamu huku machozi yakimtoka; utafikiri analia kumbe anafurahi. Kwa hiyo serikali nayo inafanya style ya mamba kwa wananchi.
Akitoa mchanganuo huo kwa baadhi ya ya fungu la chai za wizara, alisema Wizara ya Fedha na Uchumi imetengewa Sh500 milioni huku wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika ikitengewa Sh 226.3 milioni.
Chai siyo mbaya, lakini tunapaswa kuangalia nchi yetu iko katika kipindi gani kwani sasa tuko katika wakati mgumu, hivyo kutenga kiasi hicho kwa ajili ya chai tu, nafikiri si sahihi, alisisitiza mbunge huyo.
Alikumbusha bunge kwamba, limepunguzwa muda kukutana ili kubana matumizi, hivyo hakuna sababu za kuwa na matumizi makubwa katika mambo yasiyo muhimu sana kwa taifa.
Mbunge huyo alihoji: Tumepunguza muda wa mkutano wa Bunge ili kubana matumizi, sasa haya mambo mengine ambayo tumeona kama safari za serikali kutengewa Sh34 bilioni yana maana gani?
Kwa ufafanuzi, alisema Watanzania walio wengi kwa sasa wanaishi katika hali ngumu ya umaskini kutokana na kuwa na kipato kidogo, ambacho hakiwezi kukidhi mahitaji ya maisha.
Mbunge huyo akisisitiza hilo, alisema hata takwimu za kimataifa (Malengo ya Maendeleo ya Milenia MDGs) zinataka nchi zote duniani kupunguza idadi ya watu maskini wanaopata dola moja kwa siku.
Hata hapa ndani tulipo, hebu kwa mfano chukua Sh 2,000 umpe mtu, unafikiri ataishi vipi, ataigawa na kuitumia vipi fedha kama hiyo? alihoji.
Kwa upande wake Mbunge wa Kasulu Magharibi Profesa, Kilontsi Mporogomyi (CCM), aliwashambulia baadhi ya wabunge ambao wanaisifia serikali badala ya kukaa na kuikosoa kwa kuipa changamoto.
Hebu wabunge tuache utani hapa ndani, hatuko hapa kuisifia serikali ni kweli tunaangalia Progress (maendeleo), lakini hata Marekani wabunge wakiingia bungeni wanaiambia serikali fanyeni hivi, alisema na kuongeza:
Sasa hapa, sisi tunataka kuisifia serikali, unaisifia serikali wakati baba na mama yako wanaishi kwa umaskini wa kutisha vijijini kule? Huu ni utani!
Profesa Mporogomyi ambaye aliwahi kuwa Naibu Waziri miaka ya nyuma, alisema kuna umuhimu wa kuwekwa miundombinu imara ya kiuchumi ili kuwaondolea Watanzania umaskini.
Kuhusu bandari, alisema ni aibu kuzungumzia suala hilo kwani zipo nchi ambazo uchumi wake unaendeshwa kwa bandari tu.
Huku akionekana kuchukizwa na utendaji mbovu wa bandari, alishauri iwepo wizara itakayohusika na bandari kwani wizara ya sasa ya Miundombinu imeshindwa kazi.
Kwa upande wake Mbunge wa Iringa Mjini, Monica Mbega (CCM), alisema ni vema serikali ikaangalia upya kodi katika vinywaji baridi kwani kitendo cha kupandisha kodi kitapunguza wanywaji tofauti na serikali inavyofikiria.
Nafikiri uamuzi huu wa serikali kupandisha kodi katika vinywaji baridi unaweza kupunguza idadi ya wanywaji, maana kama ni soda zitanywewa kwenye harusi na misiba tu au mtu akilazwa hospitali, alifafanua.
Tuma maoni kwa Mhariri