Wabunge waanze kuombana radhi kabla ya waziri wa nishati kuwaomba radhi

thatha

JF-Expert Member
Apr 29, 2011
15,340
1,566
Ripoti ya Kamati iliyoundwa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Anne Makinda inaonesha kuwa Wabunge waliotuhumiwa kwa rushwa ndani ya TANESCO hawana hatia na kumtaka Waziri wa Nishati na Madini na Katibu wake mkuu kuwaomba radhi wabunge hao.

Sote tunakumbuka kwamba wapo wabunge waliojitokeza wazi wazi na kuwashambulia wabunge waliotuhumiwa huku wakitamka kuwa wanaoushahidi wa kutosha kuwa walikula rushwa. Mmoja wa Wabunge hao ni TINDU LISSU, JOSEPH SELASINI na wengine. Katika ripoti hiyo ni JOSEPH SELASINI aliyetajwa kuwa alisema uongo huku kamati ikipendekeza apewe adhabu ya kukosa vikao 10 vya bunge, wakati huo ikishindwa kutaja hatua ya kumchukulia TINDU LISSU.

Lakini ni jambo la kushangaza kuwa Ripoti hiyo inawataka watendaji wa Serikali kuwaomba radhi Wabunge waliotuhumiwa badala ya kuanza na wabunge walichochea moto hadi kamati hiyo ikaundwa.

Lakini pia kuna jambo la kujiuliza hapa kama kweli kamati hiyo imekuja na matokeo yatakayowaridhisha watanzania na wasiamini kuwa Wabunge wanalindana, jambo ambalo linaweza kuibua mjadala hasa wakati huu wa mchakato wa Katiba Mpya, kwani kunaweza kuwa na haja ya kuwa na tume huru ya kuwachunguza Wabunge pale watakapotuhumiwa kwa makosa mbalimbali.
 
Pitia kwanza uzi huu:

Toleo la 262 10 Oct 2012


  • Bodi ya Jenerali Mbona yatishia kujiuzulu
  • Bandari nako si shwari, mengine yafichuka

….. aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania, William Mhando, ambaye naye alisimamishwa kazi ili kupisha uchunguzi, mambo yanazidi kumuelemea, Raia Mwema, limebaini.

Mhando na wenzake walisimamishwa kazi TANESCO ili kupisha uchunguzi wa tuhuma mbalimbali zikiwamo za matumizi mabaya ya madaraka na hususan kuwapo kwa mgongano wa kimaslahi, uchunguzi ulioendeshwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ambao umebaini mgongano wa maslahi kwa kiongozi huyo.

…… Mhando amebainika kuwa na mgongano wa kimaslahi na Kampuni ya MC Donald Live Line Technology Ltd.

…..taarifa ya uchunguzi huo inamuweka katika mazingira magumu zaidi Mhando…….Pamoja na kashfa hiyo .….Raia Mwema umebaini kuwapo pia kwa kashfa nyingine ambayo pia inaonyesha matumizi mabaya ya madaraka, ikiwa nayo inathibitishwa na nyaraka, ikihusu kujipa kazi za shirika analoliongoza hivyo kujiingiza katika mgongano wa kimaslahi.

“Yupi ni mzalendo kati ya Maselle aliyepewa unaibu waziri hivi karibuni na Mkuu wa Majeshi Mstaafu, Jenerali Mboma aliyepigania nchi hii?” anahoji mmoja wa wajumbe wa bodi hiyo na kuongeza:

“Hawa vijana wasilewe madaraka, huwezi kijana umepata unaibu waziri juzi tu unamwambia Jenerali Mboma eti hana uzalendo, hana weledi, hii si sawa. Ni kukosa adabu, huu si utamaduni wetu Waafrika.”.
 
thatha ukipewa kazi ya kuchunguza familia yako mfano baba mkubwa; baba mdogo au shangazi zako utatoa taarifa ya kuwatia hatiani au ya kuwasafisha?
 
Last edited by a moderator:
Ripoti ya Kamati iliyoundwa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Anne Makinda inaonesha kuwa Wabunge waliotuhumiwa kwa rushwa ndani ya TANESCO hawana hatia na kumtaka Waziri wa Nishati na Madini na Katibu wake mkuu kuwaomba radhi wabunge hao.

Sote tunakumbuka kwamba wapo wabunge waliojitokeza wazi wazi na kuwashambulia wabunge waliotuhumiwa huku wakitamka kuwa wanaoushahidi wa kutosha kuwa walikula rushwa. Mmoja wa Wabunge hao ni TINDU LISSU, JOSEPH SELASINI na wengine. Katika ripoti hiyo ni JOSEPH SELASINI aliyetajwa kuwa alisema uongo huku kamati ikipendekeza apewe adhabu ya kukosa vikao 10 vya bunge, wakati huo ikishindwa kutaja hatua ya kumchukulia TINDU LISSU.

Lakini ni jambo la kushangaza kuwa Ripoti hiyo inawataka watendaji wa Serikali kuwaomba radhi Wabunge waliotuhumiwa badala ya kuanza na wabunge walichochea moto hadi kamati hiyo ikaundwa.

Lakini pia kuna jambo la kujiuliza hapa kama kweli kamati hiyo imekuja na matokeo yatakayowaridhisha watanzania na wasiamini kuwa Wabunge wanalindana, jambo ambalo linaweza kuibua mjadala hasa wakati huu wa mchakato wa Katiba Mpya, kwani kunaweza kuwa na haja ya kuwa na tume huru ya kuwachunguza Wabunge pale watakapotuhumiwa kwa makosa mbalimbali.

Sichangii nimekasirika sana!
 
Thatha ni kilaza sana!
Mkuu, mbona umemuhukum thatha, kwa kiasi hicho? ama kwa kuwa kashindwa kuandika vizuri jina la mwanzo la Lissu?
mbona kaongea point? wabunge watuombe radhi sisi wapiga kura kabla ya huyo waziri kuwaomba radhi, pia kapendekeza wabunge wakituhumiwa iundewe tume huru kuwachunguza!

Nakubaliana nae pamoja na mgomba101 kesi ya ngedere kwenda kwa Nyani.
 
Last edited by a moderator:
Thatha ni kilaza sana!

kwanini mkuu,nadhani ungejibu hoja kuliko kushambulia mtu,kwani kitendo ulichofanya kinadhihirisha kuwa umebeba kichwa kama mzigo na sio kiungo cha mwili kinachokusaidia kufikiri
 
Thatha ni kilaza sana!

Kwanza Tundu Lissu hakusema kuna wabunge wamekula rushwa ila aliwataja wabunge wenye mgongano wa kimaslahi na TANESCO mgongano wa maslahi siyo rushwa! Huyu thatha hawezi kujenga hoja, maana hata hajui historia ya swala lenyewe! Ulitegemea ukweli gani kwenye hiyo kamati inayojichunguza yenyewe?
 
Last edited by a moderator:
1.jpg


Huyo nae amepona? kweli Bunge la kulindana
kama Fisadi ZZK ni msafi ni balaa...
 
Kwanza Tundu Lissu hakusema kuna wabunge wamekula rushwa ila aliwataja wabunge wenye mgongano wa kimaslahi na TANESCO mgongano wa maslahi siyo rushwa! Huyu thatha hawezi kujenga hoja, maana hata hajui historia ya swala lenyewe! Ulitegemea ukweli gani kwenye hiyo kamati inayojichunguza yenyewe?

Nini maslahi ya Olesendeka ndani ya TANESCO?
 
Masikini shamba la bibi, kamati ya bunge hola, Kamati ya Nchimbi hola. Afadhili ile kamati ya Richmond..!
 
Kitendo cha wabunge kujichunguza na hatimaye kujisafisha kimedhihirisha kuwa wabunge wetu hawana nia ya dhati ya kupambana na rushwa na kujenga utawala bora katika nchi yetu,wanajua wazi kuwa rushwa huombwa katika mazingira ya siri kuu ambayo anayetakiwa kuyafichua ni anayeomba au anayeomba.sasa kwa namna hii muhongo nae anaweza kukata tamaa akaungana nao
 
Hii ilikuwa ni vita kati ya mihimili miwili yaani bunge na mawaziri/serikali, sasa bunge limepiga bao moja takatifu sana
 
Back
Top Bottom