Elections 2010 Wabunge wa Znz na bunge la Jamhuri ya muungano Tz

muchetz

JF-Expert Member
Aug 16, 2010
943
732
Mbunge anayetoka zanzibar anaingia kwenye bunge la jamhuri ya muungano kujadili mambo yanayo husu muungano tu? na kama ndivyo inapofika kwenye masuala ya Tanzania bara kuna mpaka gani unaowazuia kujadili au kushiriki katika masuala yasiyo kwenye muungano??
hii huwa siielewi kabisa maana naona kuna uwezekano mkubwa wa bara kuamuliwa mambo yasiyo ya muungano na znz.
 
Mbunge anayetoka zanzibar anaingia kwenye bunge la jamhuri ya muungano kujadili mambo yanayo husu muungano tu? na kama ndivyo inapofika kwenye masuala ya Tanzania bara kuna mpaka gani unaowazuia kujadili au kushiriki katika masuala yasiyo kwenye muungano??
hii huwa siielewi kabisa maana naona kuna uwezekano mkubwa wa bara kuamuliwa mambo yasiyo ya muungano na znz.


Mkuu Muchetz inaelekea una hoja ya maana lakini umeshindwa kunishawishi ebu nitajie kifungu cha katiba mbunge wa Zanzibar anapokatazwa kujadili masuala ya Tanzania bara.Tuanzie hapo mjandala utakuwa umewasaidia wengi nikiwemo mimi.
 
Mkuu Muchetz inaelekea una hoja ya maana lakini umeshindwa kunishawishi ebu nitajie kifungu cha katiba mbunge wa Zanzibar anapokatazwa kujadili masuala ya Tanzania bara.Tuanzie hapo mjandala utakuwa umewasaidia wengi nikiwemo mimi.

Kama umesoma vizuri post nimeuliza maswali na sikutoa conclusion ili lijadiliwe na kutolewa maoni!!
 
Mkuu Muchetz inaelekea una hoja ya maana lakini umeshindwa kunishawishi ebu nitajie kifungu cha katiba mbunge wa Zanzibar anapokatazwa kujadili masuala ya Tanzania bara.Tuanzie hapo mjandala utakuwa umewasaidia wengi nikiwemo mimi.

ngongo

Hivi ni kwanini kuna baraza la wakilishi zanzibar na hakuna baraza la wawakilishi Tanganyika?
 
Mbunge anayetoka zanzibar anaingia kwenye bunge la jamhuri ya muungano kujadili mambo yanayo husu muungano tu? na kama ndivyo inapofika kwenye masuala ya Tanzania bara kuna mpaka gani unaowazuia kujadili au kushiriki katika masuala yasiyo kwenye muungano??
hii huwa siielewi kabisa maana naona kuna uwezekano mkubwa wa bara kuamuliwa mambo yasiyo ya muungano na znz.

Mkuu hoja yako ni ya msingi sana ila naona wachangiaji wanataka kuleta upotoshaji na malumbano bila kujibu hoja.

Kwenye muungano wetu kuna masuala yanayohusu muungano (mfano ulinzi, mambo ya ndani, elimu ya juu, etc) na yasiyohusu muungano (mfano elimu ya msingi, ardhi, uchumi na biashara).

Kwenye masuala ya muungano ni sahihi kabisa kwa pande zote kukutana na kuamua kwa pamoja, lakini yakija masuala ambayo hayahusu muungano nadhani hapa ndipo kuna tatizo kwani Zanzibar ina wabunge takribani 70 kwenye bunge la muungano na hawa wanaweza kuwa na maamuzi yasiyo na manufaa kwa watu wa bara kama wakitumiwa na kundi fulani, mfano kama kundi la wabunge 120 wa bara wakawa wanataka jambo lenye manufaa kwao na wakawashawishi hawa 70 wa Znz (wanaweza hata kupewa rushwa) hivyo wanakuwa 190 na hawa wanaweza kupitisha muswada au kitu chochote bungeni ingawaje kama hawa 70 wasingepiga kura hawa 120 wasingefikia ile 50% inayotakiwa kupitisha muswada au jambo
 
Mbunge anayetoka zanzibar anaingia kwenye bunge la jamhuri ya muungano kujadili mambo yanayo husu muungano tu? na kama ndivyo inapofika kwenye masuala ya Tanzania bara kuna mpaka gani unaowazuia kujadili au kushiriki katika masuala yasiyo kwenye muungano??
hii huwa siielewi kabisa maana naona kuna uwezekano mkubwa wa bara kuamuliwa mambo yasiyo ya muungano na znz.

1 ) Unaposema bara huwa umekusudia nani ??
2 ) Ni wapi au sehemu gani imeandikwa Tanzania bara katika katiba ya Jamhuri wa Muungano.
3 ) Umeandika Tanzania bara ,kwenye bunge hujadili mambo ya Jamhuri wa Mungano wa Tanganyika na Zanzibar na si ya Tanzania Bara.
4 ) Napenda ufahamu tu Mambo yote yahusuyo Tanzania yanaihusu Zanzibar lakini si yote ya Zanzibar yanaihusu Tanzania.
Hivyo Wabunge kutoka Zanzibar wanawajibika kikamilifu kuhoji,kuchangia,kupinga au kuunga mguu jambo lolote lile ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano.
Hivyo Wabunge kutoka Zanzibar hawazuiliki kuchangia jambo lolote lile na hakuna kipengele chochote kinachothubutu kuwazuia.
 
Mbunge anayetoka zanzibar anaingia kwenye bunge la jamhuri ya muungano kujadili mambo yanayo husu muungano tu? na kama ndivyo inapofika kwenye masuala ya Tanzania bara kuna mpaka gani unaowazuia kujadili au kushiriki katika masuala yasiyo kwenye muungano??
hii huwa siielewi kabisa maana naona kuna uwezekano mkubwa wa bara kuamuliwa mambo yasiyo ya muungano na znz.
nahisi bado anahusika kwa vile Tanzania bara ingelikuwa ya Tanganyika basi tungeendelea kujadili, kwani hayo hayawahusu, kama wa Tanganyika yasivyo wahusu ya Zanzibar.
 
1 ) Unaposema bara huwa umekusudia nani ??
2 ) Ni wapi au sehemu gani imeandikwa Tanzania bara katika katiba ya Jamhuri wa Muungano.
3 ) Umeandika Tanzania bara ,kwenye bunge hujadili mambo ya Jamhuri wa Mungano wa Tanganyika na Zanzibar na si ya Tanzania Bara.
4 ) Napenda ufahamu tu Mambo yote yahusuyo Tanzania yanaihusu Zanzibar lakini si yote ya Zanzibar yanaihusu Tanzania.
Hivyo Wabunge kutoka Zanzibar wanawajibika kikamilifu kuhoji,kuchangia,kupinga au kuunga mguu jambo lolote lile ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano.
Hivyo Wabunge kutoka Zanzibar hawazuiliki kuchangia jambo lolote lile na hakuna kipengele chochote kinachothubutu kuwazuia.

Maelezo yako hayatoshelezi; kama wanakuja kwa ajili ya mambo yahusuyo muungano tu kwanini wanaruhusiwa kujadili mambo yasiyohusu muungano? Je katika bunge lao la mapinduzi/wawakilishi wanajadili mambo yanayohusu muungano? kama wanajadili ni kwa nini hatuna wabunge wa bara wanaowakilisha huko zanzibar??
 
Maelezo yako hayatoshelezi; kama wanakuja kwa ajili ya mambo yahusuyo muungano tu kwanini wanaruhusiwa kujadili mambo yasiyohusu muungano? Je katika bunge lao la mapinduzi/wawakilishi wanajadili mambo yanayohusu muungano? kama wanajadili ni kwa nini hatuna wabunge wa bara wanaowakilisha huko zanzibar??

Ni kwa sababu wao ni wawakilishi wa zanzibar ktk serikali ya muungano...muungano wetu una sehemu mbili tu zanzibar na serikali ya muungano..hakuna kitu kama bara hivyo wawakilishi hujadili, kuchangia pia kutoa maamuzi ktk bunge la muungano..hii ni kutokana na katiba ilivyo kwa sasa!
 
Ni kwa sababu wao ni wawakilishi wa zanzibar ktk serikali ya muungano...muungano wetu una sehemu mbili tu zanzibar na serikali ya muungano..hakuna kitu kama bara hivyo wawakilishi hujadili, kuchangia pia kutoa maamuzi ktk bunge la muungano..hii ni kutokana na katiba ilivyo kwa sasa!

Asante kwa maelezo mazuri, naona sasa umuhimu wa kubadilisha katiba au kuwa na serikali tatu otherwise hawa wazenj watakuwa wanatuendesha sana nakushiriki katika maamuzi mengine yasiyowahusu. Ona sasa cuf si chama cha upinzani huko zanzibar kwani wako katika serikali na wanatekeleza ilani ya ccm huko kwao, vipi huku bara ambapo serikali ya muungano inaongozwa na ccm?? haijakaa vizuri hata kidogo hii
 
Asante kwa maelezo mazuri, naona sasa umuhimu wa kubadilisha katiba au kuwa na serikali tatu otherwise hawa wazenj watakuwa wanatuendesha sana nakushiriki katika maamuzi mengine yasiyowahusu. Ona sasa cuf si chama cha upinzani huko zanzibar kwani wako katika serikali na wanatekeleza ilani ya ccm huko kwao, vipi huku bara ambapo serikali ya muungano inaongozwa na ccm?? haijakaa vizuri hata kidogo hii
Karibu ya waZanzibari 90% wanataka tuwe na serikali tatu...hata katiba ya CUF inaeleza hivyo...Tatizo hapa Tanganyika watu hawana muamko wa kisiasa. Wanao lazimisha Muungano wa serekali mbili ni Tanganyika.
 
ngongo

Hivi ni kwanini kuna baraza la wakilishi zanzibar na hakuna baraza la wawakilishi Tanganyika?

Mimi kama Nyerere angefufuka leo ningemuuliza sababu ya kuiua Tanganyika maana nimesoma kitabu chake cha "uongozi wetu na hatma ya nchi yetu" nilichoona ni yeye kupinga utanganyika bila sababu yoyote yenye nguvu.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom