Wabunge wa Tanzania poleni sana! Mnakaa kujadili na kupitisha bajeti inayoenda kupanguliwa panguliwa kienyeji?

G Sam

JF-Expert Member
Apr 20, 2013
11,555
35,880
Wabunge wa Tanzania poleni sana!

Natanguliza pole kwa kuwa hapo bungeni mmekaa tu kama watu wanajadili huku wakiwa kwenye sherehe. Mnakaa na kupitisha bajeti, mnajadili hadi mishipa ya shingo inawatoka kisha ikienda kwa bwana mkubwa anaipanga upya!

Baada ya mwaka mnaletewa taarifa kuwa fedha za afya zilienda kukomboa ndege! Sehemu ya fedha za kilimo ilibidi zimalizie ikulu ya dharura Dodoma. Bajeti yote ya michezo ilibidi ihamishwe kubomoa jengo la Tanesco Ubungo.

Mbaya zaidi mnaletewa ripoti na Sii Ei Jiii kuwa kuna matrilioni yalitumika ila hayana taarifa yoyote na mbaya zaidi wala hayakuidhinishwa na nyie "wabunge wa sherehe"

Sisi watanzania tunatakiwa tuwazodoe kwelikweli wabunge! Tuwatukane matusi ya kila aina ili warudi na wautambue wajibu wao! Waelewe kuwa kwa umoja wao wana nguvu kuliko "BWANA YULE"

Tusipofanya hivyo kwa hakika wataendelea kukaliwa kichwani na kuacha mambo ili mradi yaende. Kwakweli huenda kwa sasa hawaujui wajibu wao! Tuwasimange hadi wautafakari upya wajibu wao.

Haya kwa mara nyingine pitisheni tena kisha ikifika kwenye meza takatifu inapangwa upya tena na kichwa kimoja huku nyie mkibakia tu hoi bin taabani. Naona na siku hizi mmehamia Jf kujificha nyuma ya kiibodi pamoja na sisi pangu pakavu. Sisi na nyie tunahemea jamvi moja la malalamiko hatimaye. Karibuni tena maana mlipasahau kwa muda.Mumegawanywa mkagawanyika haswaa.

Maajabu kwelikweli na yapo huku kwetu Tz.
 
Wasipo simama wamoja kusimamia wajibu wao, naona dalili akipunguza idadi abakize kwa idadi mikoa@2 genda .Atawahadaa chama chake wapitishe sheria kujipunguza kwa ahadi atawapangia kazi nyingine.
 
Wabunge wa Tanzania poleni sana!

Natanguliza pole kwa kuwa hapo bungeni mmekaa tu kama watu wanajadili huku wakiwa kwenye sherehe. Mnakaa na kupitisha bajeti, mnajadili hadi mishipa ya shingo inawatoka kisha ikienda kwa bwana mkubwa anaipanga upya!

Baada ya mwaka mnaletewa taarifa kuwa fedha za afya zilienda kukomboa ndege! Sehemu ya fedha za kilimo ilibidi zimalizie ikulu ya dharura Dodoma. Bajeti yote ya michezo ilibidi ihamishwe kubomoa jengo la Tanesco Ubungo.

Mbaya zaidi mnaletewa ripoti na Sii Ei Jiii kuwa kuna matrilioni yalitumika ila hayana taarifa yoyote na mbaya zaidi wala hayakuidhinishwa na nyie "wabunge wa sherehe"

Sisi watanzania tunatakiwa tuwazodoe kwelikweli wabunge! Tuwatukane matusi ya kila aina ili warudi na wautambue wajibu wao! Waelewe kuwa kwa umoja wao wana nguvu kuliko "BWANA YULE"

Tusipofanya hivyo kwa hakika wataendelea kukaliwa kichwani na kuacha mambo ili mradi yaende. Kwakweli huenda kwa sasa hawaujui wajibu wao! Tuwasimange hadi wautafakari upya wajibu wao.

Haya kwa mara nyingine pitisheni tena kisha ikifika kwenye meza takatifu inapangwa upya tena na kichwa kimoja huku nyie mkibakia tu hoi bin taabani. Naona na siku hizi mmehamia Jf kujificha nyuma ya kiibodi pamoja na sisi pangu pakavu. Sisi na nyie tunahemea jamvi moja la malalamiko hatimaye. Karibuni tena maana mlipasahau kwa muda.Mumegawanywa mkagawanyika haswaa.

Maajabu kwelikweli na yapo huku kwetu Tz.
Usiwape pole, waambie waongeze nguvu ya kufikiri kuliko mwanzo. Bunge lilifikia hatua ya kutenga 'pesa za chai' nyingi kuliko za maendeleo. Ikiwa hivyo kwa nini maamuzi yao yasipanguliwe?
 
Jamaa tayari ana budget yake kichwani. Wabunge wanapoteza muda wao. Tunahitaji kumthibiti anadhani hela ni za kwake binafsi.
 
Wabunge ni wabinafsi na mambumbumbu. Wanachojali ni mishahara na posho zao tu, wengi wao hata hawajui majukumu ya bunge ni yapi. Magufuri amewatia mfukoni, it's a shame
 
Shida kubwa ni kuvifanya vyama kuwadhibiti wabunge hata baada ya kuchaguliwa!!
Hapo ndipo mzizi wa fitina ulipo. Siku ibara inayolazimisha wabunge kuvitii vyama vyao kitakapoondolewa kwenye Katiba ya nchi yetu, ndipo tutakapopata bunge imara na lenye kujitegemea!!
 
Nilikua najiuliza Jamaa kila akisimama utasikia kesho billion 10 ziende sehemu flani, Sasa zinatoka kwenye bajet ipi?

Inabidi waondoke tu huko Dodoma hakuna wanachofanya zaidi ya kula posho tu!

Haiwezekani bajet ya nchi ipanguliwe na mtu mmoja kama vile anafanya bajet ya familia yake!
.......


!
!
Acha Tu Mkuu. Mzee Ana Mihela Mno
 
Wabunge wa Tanzania poleni sana!

Natanguliza pole kwa kuwa hapo bungeni mmekaa tu kama watu wanajadili huku wakiwa kwenye sherehe. Mnakaa na kupitisha bajeti, mnajadili hadi mishipa ya shingo inawatoka kisha ikienda kwa bwana mkubwa anaipanga upya!

Baada ya mwaka mnaletewa taarifa kuwa fedha za afya zilienda kukomboa ndege! Sehemu ya fedha za kilimo ilibidi zimalizie ikulu ya dharura Dodoma. Bajeti yote ya michezo ilibidi ihamishwe kubomoa jengo la Tanesco Ubungo.

Mbaya zaidi mnaletewa ripoti na Sii Ei Jiii kuwa kuna matrilioni yalitumika ila hayana taarifa yoyote na mbaya zaidi wala hayakuidhinishwa na nyie "wabunge wa sherehe"

Sisi watanzania tunatakiwa tuwazodoe kwelikweli wabunge! Tuwatukane matusi ya kila aina ili warudi na wautambue wajibu wao! Waelewe kuwa kwa umoja wao wana nguvu kuliko "BWANA YULE"

Tusipofanya hivyo kwa hakika wataendelea kukaliwa kichwani na kuacha mambo ili mradi yaende. Kwakweli huenda kwa sasa hawaujui wajibu wao! Tuwasimange hadi wautafakari upya wajibu wao.

Haya kwa mara nyingine pitisheni tena kisha ikifika kwenye meza takatifu inapangwa upya tena na kichwa kimoja huku nyie mkibakia tu hoi bin taabani. Naona na siku hizi mmehamia Jf kujificha nyuma ya kiibodi pamoja na sisi pangu pakavu. Sisi na nyie tunahemea jamvi moja la malalamiko hatimaye. Karibuni tena maana mlipasahau kwa muda.Mumegawanywa mkagawanyika haswaa.

Maajabu kwelikweli na yapo huku kwetu Tz.
Wewe jamaa una kazi ya kufanya nini
 
Jamaa tayari ana budget yake kichwani. Wabunge wanapoteza muda wao. Tunahitaji kumthibiti anadhani hela ni za kwake binafsi.
Acha kabisa mkuu. Anawauzisha chai muda ukifika anafanya yake
 
Back
Top Bottom